JIKO LA USHAURI

Itambue Injili Ya Maji Na Roho. Ushiriki Ufalme wa Mungu, pata kitabu cha bure. Wasiliana nasi kwa sadikila65@gmail.com.

  • NYUMBANI
  • KUFURAHIA MAISHA
    • ushauri
    • KUHUSU SISI
    • MAISHA NDANI YA YESU
  • MAWASILIANO
    • NAMBA YA SIMU
      • Sub 0687000768
      • Sub Child Category 2
      • facebook
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • NJOZI
  • SAIDIA HUDUMA HII
    • Childcare
    • Doctors
  • NYUMBANI
  • KUFURAHIA MAISHA
    • Stock
  • TAFAKARI YA ROHO
    • HEKIMA ZA WAZEE
    • Games
    • AFYA
      • Office
  • MAHUSIANO
    • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI
      • Sub Child Category 1
      • Sub Child Category 2
      • Sub Child Category 3
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • USHAURI
  • TAFAKARI NENO YA SIKU
    • Childcare
    • Doctors
  • PATA BLOGU

Friday, September 21, 2018

Kuijua Imani Na Kuishi Maisha Ya Ushindi.

 Sadick Kilasi     September 21, 2018     TAFAKARI YA ROHO     No comments   

KANUNI YA  IMANI.

Cha kwanza kabisa kila kitu ambacho kipo duniani huendeshwa kwa imani tu. Vitu vyote vyenye sura ya kueleweka huwa havieleweki. Sasa kwa sababu havieleweki basi lazima lugha yenye mipaka lazima itumike. Vitu vyote vyenye mwili huendeshwa kwa imani tu na sio ukweli halisi. Majina yao ni majina ya kukalili au majina ya kuzoea, wasomi wanaita mantiki. Na ndiomaana ni rahisi mtu kubadili jina lake lakini uhalisia wa sura yake haupotei, naweza kubadili jina langu la Sadick labda kwenda jina la Antoni na baadae jina hilo likazoeleka na watu wakawa wanalitumia vizuri kama jina la mwanzo lakini mwanzo nilikuwa naitwa Sadick na watu walikuwa wamelizoea jina hilo. Ili ukweli wa majina uwe ukweli lazima nitumie imani. Imani huwa inabadilika lakini ukweli huwa haubadiliki. Kwa kadili ambavyo unajua kitu ndivyo ambavyo utazidi kubadili imani yako. Imani yako inawezekana ikawa inaongezeka au inapungua kutokana na ukamili wa taarifa na jinsi ambavyo unachukulia hilo jambo. Ni muhimu sana kuelewa juu ya imani kwani vitu vyote nyenye mwili huendeshwa kwa imani tu kwani kila kitu chenye mwili hakieleweki kilikotoka. Dunia hujaza sehemu ambayo inautupu na ikisha kujaza mwanadamu atakipa jina kile kitu; mfano, mti, nyasi, watu na kila kitu chenye mwili. Imani ni maoni ya mtu juu ya jambo fulani.

Imani ni kuwa na hakika na mambo yajayo, hii ni maana ya kibiblia. Waebrania 11:1, Kuwa na imani ni kuwa na hakika na mambo tunayotumainia; kusadiki kabisa mambo tusiyoyaona. Ikiwa tupo duniani na tunaona kila kitu, je, tutakuwaje na imani? Na kwa sababu imani ni kuwa na hakika na mambo usiyoyajua basi ni wazi kwamba kila kilichopo duniani hakina ukweli ulio sahihi. Na tunaamini kwamba hii ndio dunia ya kueleweka, mambo yote hapa yapo waziwazi tofauti na rohoni ambako kwa imani inasemekana kwamba huko hakuna vitu vyenye mwili.
Waebrania 11:3, Kwa imani sisi tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, vitu vinavyoonekana kutoka vitu visivyoonekana. Kwa sasa tupo katika dunia ya vitu vinavyoonekana na tumaini letu ni kuona uso wa Mungu ambapo ndipo mwanzo wa dunia kuumbwa kwani dunia iliubwa kwa neno la Mungu. Kwa sasa tupo kwenye vitu vinavyoonekana tunarudi sasa kwenye vitu visivyoonekana. Lakini kwa kuwa bado tupo safarini katika dunia hii tunaweza kuwa na hakika kutoka vitu visivyoonekana kwenda kwenye vitu vinavyoonekana, hiyo nayo ni imani. Waebrania 11:11, Kwa imani hata Sara aliamini kwamba Mungu hutimiza ahadi zake, kwa hiyo akajaliwa kuchukua mimba ingawaje alikuwa amepita umri. Imani ni kupata haki ya jambo ambalo halipo. Na hivyo ndivyo dunia inakwenda kwa imani. Watu wote tunaishi kwa imani, kutoka kwenye kitu kisichoonekana kwenda kwenywe kitu kinachoonekana na kutoka kitu kinachoonekana kwenda kwenye kitu kisichoonekana. Haya yote ni matumaini ambayo tunayo. Imani ni kufanya jambo kuwa haki amblo halina hakika kuwa kweli. Kila jambo limefichwa, ukiona unacho basi tambua wakati wote kile kitu ambacho unacho kinaweza kuchukuliwa na ukiona huna basi tambua kwamba ukiwa na imani tu na kupata haki ya kile ambacho huna utapokea kutoka kwa Mungu. Katika dunia tunaishi ndani ya wakati, vitu vyote vyenye mwili kwa kadili wkati unavokwenda hupoteza ubora wake na mwisho hupotea kabisa lakini hivyohivyo tena sehemu ambayo ipo wazi ni lazima ijazwe kutoka kwenye vitu visivyoonekana kwenda kwenda kwenye vitu vinavyoonekana na hii ndio imani. Lazima utambue kwamba vitu vya mwili na vya rohoni haviwezi kukaa kwa pamoja, ni jambo ambalo haliwezekani ni lazima mwili utumainie rohoni na rohoni kutumainie mwilini. Sasa  kutokana na kutokuwepo kwa ukamirifu huo basi imani lazima itumike, na hapo ndipo ambapo mtu anajenga picha kichwani mwake ya jambo ambalo halipo katika uwepo wa macho.
UMUHIMU WA IMANI KATIKA MAISHA.

Ikiwa umetambua tayari kwamba maisha ya hapa duniani hayana ukamirifu basi ni wazi kabisa tayari umeuona umuhimu wa imani. Kama chenye mwili huingia duniani na kuanza kupoteza kila wakati, kutoka kwenywe kwenye kuwepo kwenda kwenye kutokuwepo basi ni wazi kwamba ni muhimu sana kujali wakati au muda. Ni muhimu sana kujali wakati, kwa sababu kila sekunde kwako ni gharama ya maisha yako inapungua. Ikiwa kila sekunde unamegwa na kuondolewa sehemu fulani ya uzima wako basi mwisho uzima utakuishia na wewe utabaki huna cha kuishi katika ulimwengu, mwili wote umeisha. Sasa kama wakati sio kipaumbele chako basi tambua kwamba utaenda kama ulivokuja bila kuacha alama yoyote hapa duniani.

 Kitu kingine cha muhimu katika imani ni kutambua mazingira na kujitambua mwenyewe. Unajua, unavojielewa kwamba wewe ni mwili na unamatumaini ya kurudi rohoni ni wazi kwamba tayari utaishi kwa matumaini ya kwenda rohoni. Hivi sasa watu wengi wanaishi maisha ya kutumainia kwenda rohoni. Kwa kuwa unatambua abisa kwamba utakwenda rohoni basi bi wazi kwamba lazima ubaki kwenye njia ya kwenda rohoni, njia ambayo itakurudisha ulikotoka na sio kwenda jehanamu ambako hujatoka huko, hana, ni lazima ubaki katika njia kuu.

Kitu kingine cha muhimu kwenye imani, ikiwa tayari umeelewa imani ni nini? Tayari unaweza kutambua kwamba, hapa, hapa, duniani kama ulikuwa umekosa kitu fulani ni wazi kwamba unaweza kumwomba  Mungu na akakupatia kile kitu ambacho huna na ukakipata kwa sababu chochote kile ambacho huna ukimwomba Mungu anakupa. Mwanzo  15:1-6, Baada ya mambo hayo neno la Mwenyezi Mungu lilimjia Abramu katika maono, Abramu! usiogope! Mimi ni ngao yako. Tuzo alko litakuwa kubwa! Lakini Abramu akasema, Ee Mwenyezi Mungu, utanipa nini hali naendelea kuishi bila mtoto, na urithi wangu ni Eliezeri wa Damasko? Tazama! Hujanijalia mtoto; mtumwa aliyezaliwa nyumabani mwangu ndiye atakaye kuwa mrithi wangu! Ndipo Mwenyezi Mungu akamwambia, Huyu hatakua mrithi wako! Mwanao halisi nndiye atakayekuwa mrithi wako. Hapo Mwenyezi Mungu akamleta Abramu nje na kumwambia, Tazama mbinguni, zihesabu nyota, kama kweli utaweza  kuzihesabu! Hivyo ndivyo wazawa wako watakavokuwa wengi! Abramu akamwamini Mwenyezi Mungu, naye mwenyezi Mungu akamkubali Abramu kuwa mwadilifu.
Mungu alimkubali Abramu kwa imani na alimkubali Abramu kuwa mwadilifu kwa imani tu kabla ya matukio kutukia na Abramu alimwamini Mungu kwa imani tu kwani Abramu alikuwa bado hana uzao wa kumrithi na wala Mungu alikuwa hajamtimizia ahadi. Unapo amini, unapokea haki na ukisha kupokea ndipo matokeo nje huonekana. Leo hii hata sisi Abramu ni Baba yetu wa imani kwani yeye ndiye mwanzo waimani. Waisraeli pekee ndiyo waliokuwa taifa teule la Mungu lakini hata sisi tunashiriki kuwa watoto wa Mungu kwa imani. Maisha ya Abramu yalikuwa hayana tumaini lakini kwa imani akapata tumaini jipya ambalo Mungu alimuahidi.

Lakini faida nyingine ndiyo hii, ni njia nzuri zaidi ya kuondoa uchungu moyoni mwako ikiwa unamatatizo fulani. Ni rahisi kumsamehe mtu moyoni mwako kuliko kumkabili nje. Ikiwa utaanza kuwasamehe watu na kujisamehe mwenyewe basi tayari unakuwa unaukomavu wa ndani. Ni rahisi kuomba maombi mengi rohoni mwako, laakini pia ni rahisi kutimiza jambo ambolo linaanzia ndani na kutoka nje. Ikiwa unataka kutimiza mapenzi yako kwa matokeo ya nje basi ni wazi kwamba ndani mwako uwe unahamu zaidi ya mara mbili ya matokeo ya nje, ili utimize vizuri. Mathayo 5:20, Ndiomaana nawambieni, wema usipozidi ule wa walimu wa sheria na wa mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni. Ikiwa unataka kufanya jambo lolote basi inatakiwa uwe na hamu kubwa ndani yako harafu nje utatimiza kwa ubora zaidi kwa kadili ya imani yako. Mafarisayo na walimu wa sheria ni walikuwa watu ambao hutimiza mambo yao kwa kinafki kwa sababu walikuwa hawana imani ndani yao, sasa Yesu alimbia watu msipozidi kuwa na hamu kubwa zaidi ya walimu wa sheria na mafarisayo hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni. Ni lazima uwe na hamu kubwa ndani mwako ya kutaka kuwa bora, ni lazima ndani mwako uwe na hamu kubwa ya kutaka kuishi na watu vizuri na watu, ni lazima ndani mwako uwe na utayari wa kutaka kujijenga zaidi hata kama watu nje wanakuonyesha na kukukatisha tamaa.

Hii ni sheria, kwamba lazima uwe na imani ndani mwako na ndipo utimize mapenzi yako. Ikiwa unajengeka ndani mwako kwa imani kwa mtu ambaye hawezi kuona basi ni rahisi kujengeka kwa nje ambako watu huona. Kama ukiwa tayari kujielewa wewe mwenyewe basi ni rahisi kuwaelewa wengine. Kama ukiwa tayari kujihimili wewe mwenyewe basi ni rahisi kuwahili wengine. Ukitimiza haya basi huo ni utajiri. Lao Tsu.  Ni ukweli mtu, ukiweza kujijenga wewe mwenyewe binafsi basi rahisi kuwajenga wengine na ukiweza kujielewa wewe mwenyewe binafsi basi rahisi kuwaelewa wengine. Kama umejielewa kunamaeneo upo vizuri katika utendaji na kunamaeneo haupo vizuri katika utendaji basi katika maisha yako utaelewa kwamba kila mtu anaudhaifu maeneo fulani na kwenye maeneo fulani yupo bora. Wakati fulani huwa nafanya maamuzi haya bila kutegemea basi utaelewa kabisa hata mwenzangu hivo hivo, kwahiyo na imani hiyo inakuwa ni rahisi kutekeleza msamaha.

Ikiwa Ibramu alipata haki kwa imani basi Ibrahimu aliamini kwamba Mungu hawezi kushindwa kufanya lolote lile analolitaka. Imani inahitaji utambuzi ili kupata haki ya kutenda lile jambo unalotaka kutenda. Kama unataka kutimiza jambo ukiwa unafahamu mamlaka yako nni rahisi kutimiza jambo kwa imani. Kwa imani sisi tunavikubali vitu alivyoviumba Mungu, Kwa imani sisi tunakubali kwamba Mungu alimtoa mwanae Yesu Kristo ili achukue dhambi ya ulimwengu pale alipobatizwa na Yohana katika mto Yordani walifanya tendo la kikuhani na sisi kwa sasa hatuna dhambi. Kwa imani tunaamini Yesu aliteswa msalabani kwa sababu ya dhambi zetu na damu ya agano ikamwagika na sisi tukafanyika, kwa imani tunaamini kwambaYesu alikufa baada ya mateso na kufufuka kutoka kwa wafu na sasa yupo hai juu mbinguni. Kwa imani tunaamini kwamba ametubatiza kwa roho mtakatifu na sasa tunafurahia maisha. Imani hii inatupa haki sisi ya kufanyika wana wa Mungu. Kwa imani sasa  tunatekeleza upendo wa Mungu kwa sababu tayari hata sisi tumefanyika pendo kwa kuitwa wana wa Mungu na kujazwa Roho ya Mungu.
Imani inakupa wewe haki ya kutaka unachotaka ili mladi tu unijijenga mwenyewe au la unawajenga wengine. Imani hiyo inakufanya uchukue hatu ya kile ambacho unakiamini. Kwa hiyo rafiki yangu kazana kujijenga ndani mwako na kwa kadili ambavyo unajua zaidi ndivyo unapata haki ya kutaka kile kitu, utambuzi wa ndani ni muhimu zaidi.

Na cha mwisho ambacho ni muhimu  ni hiki, kila kitu mwanzo wake ni Mungu, na ndiomaana kila wazo huja kwako bila wewe kutambua na kinachofuata ni utayari wa kupokea kile ulichopokea kwa Mungu huku ukimtumainia yeye. Kwa hiyo imani ni kuishi tumaini wakati wa hivi sasa. Katika ndani ya maisha hayo kuna, imani, utayari na matumaini. Hivi vyote hufanya kazi kwa pamoja.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.

  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg
Email ThisBlogThis!Share to XShare to Facebook
Newer Post Older Post Home

0 comments:

Post a Comment

Search This Blog

Translate

Total Pageviews

About Me

Sadick Kilasi
View my complete profile

Followers

Kurasa

  • Nyumbani
  • Saidia Huduma Hii Kuwafikia Wengi Zaidi.

Search This Blog

Blog Archive

  • ►  2020 (5)
    • ►  January (5)
  • ►  2019 (46)
    • ►  December (4)
    • ►  October (1)
    • ►  July (8)
    • ►  June (1)
    • ►  May (2)
    • ►  March (14)
    • ►  February (11)
    • ►  January (5)
  • ▼  2018 (275)
    • ►  December (17)
    • ►  November (25)
    • ►  October (29)
    • ▼  September (43)
      • Toa Ulichonacho, Anzia Hapo Ulipo.
      • Panda Mti Leo.
      • [TAFAKARI NENO YA LEO..13] Hatupokei Haki Ya Mungu...
      • Saidia Huduma Hii Kuwafikia Wengi Zaidi.
      • Usijikinai Ndugu, Utaoza.
      • [TAFAKARI NENO YA LEO..12] Injili Ya Maji Na ROHO....
      • Utukufu Ni Wa Mungu.
      • [TAFAKARI NENO YA LEO..11] Je! Ufanye Nini Wakati ...
      • Watu Hawatakosa La Kusema, Endelea Kufanya Unachop...
      • [TAFAKARI NENO YA LEO...10] Hamna Namna, Mshangaze...
      • Endelea Kufanya Yanayofaa.
      • [TAFAKARI NENO YA LEO...9] Ukimpokea Yesu Onyesha...
      • Hii ndio Njaa Kubwa Ya Dunia Ya Sasa.
      • Tumia Makombo Ya Wakati Wako Kujisomea Neno La Mungu.
      • Naomba Uniambie Rafiki Yangu, Unaishije Na Watu Wa...
      • Una Shina La Kukupeleka Katika Ushindi.
      • Je! Mungu Atakuwepo Au Hatakuwepo?
      • [TAFAKARI NENO YA LEO..8] Mambo Mawili Ambayo Huon...
      • Ukiona Unaliamini Jambo Na Huishi Hilo Jambo Basi ...
      • Je! Unapanda, Au Unashuka Bondeni?
      • Huwezi Kuuona Umuhimu Wa Maji Mpaka Visima Vikauke.
      • Kuijua Imani Na Kuishi Maisha Ya Ushindi.
      • Ukiona Fursa Hazigongi Mlango Jenga Mlango.
      • Jenga Tabia Hii Nayo Tabia Itakujenga Katika Mahus...
      • Gharama Ya KupataVitu Vizuri Vinavyokupeleka Katik...
      • [TAFAKALI NENO YA LEO...7] Ondoleo La Hofu Na Mais...
      • [TAFAKARI HEKIMA ZA WAZEE], Kuwaelewa Wengine, Kuj...
      • Alituchagua Tangu Tukiwa Na Dhambi. [Kwa Imani Tun...
      • Kanuni Ya Kibiblia Ambayo Inaweza Kukusaidia Kupan...
      • Utabiri Wa Nabii Danieli Juu Ya Injili Ya Maji Na ...
      • [TAFAKARI NENO YA LEO...6] Tumeandaliwa Mazingira ...
      • Umezaliwa Wa Kipekee Sana Lakini Watu Ndio Kioo Ch...
      • (TAFAKARI NENO YA LEO...5) Kama Una Tumaini Basi T...
      • Hakuna Mtu ambaye Hana Kabisa Katika Maisha.
      • [TAFAKARI NENO YA LEO..4] Mtumainie Mungu Usikate ...
      • Hii Ni Bahati Yako Au Ni Wakati Sahihi Kwako?
      • [TAFAKARI NENO YA LEO 3] Usiende Kwa Mganga Siku Y...
      • Tunapokea Na Kutoa Kutokana Na Utayari Tulionao....2
      • [TAFAKARI NENO YA LEO...2] Je! Unataka Kuwa Na Fur...
      • Geuza Machungu Yako Kuwa Ushindi.
      • [TAFAKARI NENO YA LEO ...1] Jinsi Chuki Zinavyoene...
      • Tafakari Neno Ya Siku.
      • Tunapokea Na Kutoa Kwa Utayari Tulionao.
    • ►  August (7)
    • ►  July (12)
    • ►  June (17)
    • ►  May (19)
    • ►  April (31)
    • ►  March (33)
    • ►  February (25)
    • ►  January (17)
  • ►  2017 (58)
    • ►  December (16)
    • ►  November (22)
    • ►  October (2)
    • ►  September (11)
    • ►  August (4)
    • ►  July (3)
Sadick Kilasi. Powered by Blogger.

Jisajili kwa kujiunga nasi hapa

Posts
Atom
Posts
Comments
Atom
Comments
Maisha yenye maana ni yale maisha ambayo mhusika atambua nini kusudi lake la kuwepo hapa duniani. Hapandipo muhusika anapo kaa katika nafasi yake na kuwasha nuru katika sehemu aliopo kutokana uhusika wake. Jiunge na mtandao huu kupata maarifa zaidi na kwa ushirikiano mwingine kwa ujumla.

Kurasa

  • Nyumbani
  • TAFAKARI ROHO
  • Saidia Huduma Hii Kuwafikia Wengi Zaidi.

JIUNGE NASI SASA KWA KUJAZA FOMU HAPO CHINI


ANZA KUFURAHIA MAISHA NDANI YA YESU, MPOKEE ROHO MTAKATIFU KWA INJILI YA MAJI NA DAMU 0687000768

Zilizosomwa sana

  • Chukua hizi hapa nukuu za Malcolm x mtu ambaye anawavutia wengi sana.
    Ni siku nyingine tena ambayo ni mpya kabisa, karibu tena katika blogu hii ya JIKO LA USHAURI ambapo mimi mpendwa wako nimekuwa naingia jikon...
  • Ubatizo Wa Maji Mengi Na Ubatizo Wa Maji Machache, Upi Ni Sahihi?
    Ubatizo wa Maji Mengi Na Maji Machache. Kumekuwa na migongano kwa muda mrefu sana juu ya ubatizo, kati ya ubatizo wa maji mengi na ule uba...
  • Falsafa Za Maisha, Yaani Neno La Maarifa.
    Falsafa Za Maisha, Yaani Neno La Maarifa. Habari mpendwa? Natumai wewe unayesoma hapa umzima.   Karibu tena katika Falsafa Za Maisha. Ku...

Blog Archive

  • July 2017 (3)
  • August 2017 (4)
  • September 2017 (11)
  • October 2017 (2)
  • November 2017 (22)
  • December 2017 (16)
  • January 2018 (17)
  • February 2018 (25)
  • March 2018 (33)
  • April 2018 (31)
  • May 2018 (19)
  • June 2018 (17)
  • July 2018 (12)
  • August 2018 (7)
  • September 2018 (43)
  • October 2018 (29)
  • November 2018 (25)
  • December 2018 (17)
  • January 2019 (5)
  • February 2019 (11)
  • March 2019 (14)
  • May 2019 (2)
  • June 2019 (1)
  • July 2019 (8)
  • October 2019 (1)
  • December 2019 (4)
  • January 2020 (5)

JIKO LA USHAURI

Itambue Injili Ya Maji Na Roho. Ushiriki Ufalme wa Mungu, pata kitabu cha bure. Wasiliana nasi kwa sadikila65@gmail.com.

Tags

  • BIASHARA
  • HEKIMA ZA WAZEE
  • KUFURAHIA MAISHA
  • KUPATA BLOGU
  • MAHUSIANO
  • MAWASILIANO
  • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI
  • NJOZI
  • PATA BLOGU
  • SAIDIA HUDUMA HII
  • TAFAKARI NENO YA SIKU
  • TAFAKARI YA ROHO
  • UJASIRIAMALI
  • USHAURI
  • USWAZI TRICK

Kurasa

Labels

  • HEKIMA ZA WAZEE (24)
  • KUFURAHIA MAISHA (76)
  • KUPATA BLOGU (2)
  • MAHUSIANO (81)
  • MAWASILIANO (1)
  • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI (8)
  • NJOZI (94)
  • PATA BLOGU (3)
  • TAFAKARI YA ROHO (57)
  • UJASIRIAMALI (31)
  • USHAURI (78)
  • USWAZI TRICK (9)

Loading...

Fomu ya Anwani

Name

Email *

Message *

  • Napenda kusoma Biblia

About Me

Sadick Kilasi
View my complete profile
INJILI YA MAJI NA DAMU.

Search This Blog

Chapisho Lililoangaziwa

Alipambania Tumaini Lake Na Ndoto Yake Ikawa Kweli.

Kila mtu katika maisha ana tumaini lake. Msingi mkuu wa maisha ni tumaini. Nguvu kubwa ya maisha ni imani na mapito makuu ya maisha ni u...

Posts
Atom
Posts
Comments
Atom
Comments
INJILI YA KWELI NI INJILI YA MAJI NA ROHO. (MAJI, DAMU NA ROHO).
HII NDIYO KWELI YENYEWE.
YOHANA 19:34-35.

Copyright © JIKO LA USHAURI | Powered by Blogger
Design by Hardeep Asrani | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com | Distributed By Gooyaabi Templates