JIKO LA USHAURI

Itambue Injili Ya Maji Na Roho. Ushiriki Ufalme wa Mungu, pata kitabu cha bure. Wasiliana nasi kwa sadikila65@gmail.com.

  • NYUMBANI
  • KUFURAHIA MAISHA
    • ushauri
    • KUHUSU SISI
    • MAISHA NDANI YA YESU
  • MAWASILIANO
    • NAMBA YA SIMU
      • Sub 0687000768
      • Sub Child Category 2
      • facebook
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • NJOZI
  • SAIDIA HUDUMA HII
    • Childcare
    • Doctors
  • NYUMBANI
  • KUFURAHIA MAISHA
    • Stock
  • TAFAKARI YA ROHO
    • HEKIMA ZA WAZEE
    • Games
    • AFYA
      • Office
  • MAHUSIANO
    • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI
      • Sub Child Category 1
      • Sub Child Category 2
      • Sub Child Category 3
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • USHAURI
  • TAFAKARI NENO YA SIKU
    • Childcare
    • Doctors
  • PATA BLOGU

Sunday, September 30, 2018

Toa Ulichonacho, Anzia Hapo Ulipo.

 Sadick Kilasi     September 30, 2018     TAFAKARI YA ROHO     No comments   


KANUNI YA KUTOA KAFARA.

Kafara ama kwa lugha nyingine sadaka ni kitu ambacho unatumia ili kuhusianisha kati yako wewe na kitu ambacho unataka kukipata. Ikiwa mtu hajatoa kafara katika jambo analotaka kulifanya basi ni ngumu kulifanya hilo jambo. Mara nyingi huwa baada ya kupokea jambo fulani jipya ambalo tumelipenda na tungehitaji kulipata huwa tunakwepa gharama ya maumivu ya mwanzo. Ukweli ni kwamba kilajambo ambalo ni sahihi na ni kweli huwa linahitaji kulipa gharama fulani mwanzo mwa hilo jambo. Na mara nyingi gharama ile ndiyo inakuwa ukuta mkubwa sana wa kufikia jambo hilo ambalo mtu anapaswa kulichukulia hatua. Japo kuwa licha ya kuwepo gharama ya kulipa mwanzo sio kwamba lile jambo huwa haliwezekani bali mhusika huwa anakwepa kijanja kulifanya jambo lile. Zipo sababu ambazo mara nyingi humzuia mtu kutokufanya jambo ambalo anataka kulifanya. Mazoea huwa yanafanya mtu asichukue hatua fulani. Ikiwa mtu una uraibu wa kufanya jambo fulani, kuachana na jambo hilo na kuanza kufanya jambo jipya inakuwa ni ngumu sana. Ni pale sasa ambapo unahitaji kujitoa mzima mzima, kujitoa wewe mwenyewe kama kafara.

Sababu nyingine ni vijisababu visivyoeleweka huweza kusababisha kutofanya jambo jipya. Unaweza ukawa unatamani kufanya jambo fulani lakini unaweka sababu ambazo hazilingani kabisa na kusudi lako, lakini wakati mwingine sababu hizo zikawa zinaleta maana kabisa kwako wewe binafsi na kwa wengine pia wanaokusikiliza.

Biblia huonyesha namna ya kujitoa katika hali fulani ya mazoea ambayo mtu amezoea kufanya.
Mahubiri ya Yohana. Mathayo 3:1-10.
Siku zilealiondokea Yohana Mbatizaji akihubiri katika nyika ya Uyahudi, na kusema, Tubuni; kwa maana Ufalme wa Mbinguni umekaribi. Kwa sababu huyo ndiye aliye nenwa na nabii Isaya, akisema, Sauti ya mtu aliaye nyikani, itengenezeni njia ya Bwana, yangyosheni mapito yake. Naye Yohana mwenyewe alikuwa na vazi la singa za ngamia, na mshipi wa ngozi kiunoni mwake; chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu. Ndipo walipomwendea Yerusalemu, na Uyahudi, wote, na nchi zote za kandokando ya Yordani; naye akawabatiza katika mto Yordani, huku wakiziungama dhambi zao.Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya nyinyi kukimbia hasira itakayokuja? Basi zaeni matunda yapasayo toba; wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawambia ya kwamba Mungu anaweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto. Na shoka limeshawekwa kwenye mashina ya miti; basi kila mti usioweza kuzaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.

Ubatizo maana yake kuzamia katika jambo fulani,zamisha kwenye maji. Ikiwa mtu amekiri toba, kuna madhehebu mengine huwabatiza watu kwa kuwazamisha kwenye maji kama ishara ya kusafisha dhambi. Lakini lengo kubwa kuwazamisha katika maji bali lengo kubwa ni kufanya yanayofaa kufanywa. Ikiwa kweli umetubu basi utaonyesha kwa matendo na ndio maana Yohana aliwaka hasira kwa Mafarisayo na Masadukayo, sio kuamini tu bali wanapaswa kuonyesha kwa matendo kulingana na imani yao.

Luka 3:10-14,Makutano wakamwuliza, tufanye nini basi? Akawajibu akawambia, mwenye kanzu mbili na ampe asiye na kanzu; mwenye vyakula na afanye vivyo hivyo. Watoza ushurunao wakaja kubatizwa, wakamwuliza Mwalimu, tufanye nini sisi? Akawambia, msitoze kitu zaidi kuliko ulivoamriwa. Askarri nao wakamwuliza sisi tufanye nini? akawambia, msidhulumu mtu, wala msishitaki kwa uongo; tena mtoshewe na mshahara wenu.

Ikiwa mtu unasumbuliwa na jambo fulani ambalo limekuwa uraibu kwako na linakufanya ukose furaha na unashindwa namna ya kujitoa kilicho muhimu ni kutubu, kwa kukiri kwamba sasa nipo hapa na natubu kwa kuacha kufanya jambo jingine jipya. Kuna uraibu wa mambo mbalimbali, kubishana, kulala sana, mawazo mengi,kuangalia tivi sana, kujikuta unapenda kwenda mahali fulani bila sababu na tabia nyingine ambazo umezoeza na baadae ikawa usumbufu kwako. Kumbuka rafiki yangu, ninachofanya hapa ni kuhubiri injili kwahiyo, umakini wako ndio utakufanya uponywe kutoka na hali mbalimbali. Wakati Yohana alipokuwa akihubiri injili, akitokea jangwani, injili ya wito wa toba, watu walikuwa wamejizoeza kuabudu sanamu, wamejawa na dhambi na mambo mengine machafu. Lakini Yohana alikuja kugeuza mioyo yao, kwa kuwambia tubuni, yaani geuka, na kuonyesha matunda baada ya kugeuka kwamba umeamini kile unachokigeukia unafanya kwa matendo. Yohana alikuwa anageza mioyo ya watu ambao walikuwa wanaenda kuangamia kwa kkufanya mambo yasiyo faa, wito wake ni kugeuza mioyo yao na kuwambia wachukue  hatua za  matunda ya imani mpya.

Unaweza kijikuta upo katika hali ya maumivu wakati mwingine, kutokana na tabia ambayo umeiendekeza kwani mwili hukulazimisha ufanye jambo ambalo wewe mwenyewe hutaki; Warumi 7:19, Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo. Katika hali kama hii unaweza kujikuta katika wakati mgumu sana, kwa sababu kuna vita inakuwa inaendlea ndani yako.  Katika hali hii unahitaji kutimiza mapenzi yako kwa kile ambacho unadhamilia kufanya, kwa uwezo ulionao mwenyewe. Usiishie kusema nataka kufanya jambo fulani, hapana. inakupasa imani yako uunganishe na matendo yako. Usione kama huwezi kuchukua hatua yoyote, kwani kiashilia cha maumivu hayo, kinaonyesha kwamba unapaswa kufanya jambo ambalo ni sahihi.
2Wakorintho 8:11, Lakini sasa timizeni kule kutenda nako, ili kama vile mlivyokuwa tayari kutaka, vivyo hivyo mkawe tayari na kutimiza kwa kadiri mlivyo navyo. Kutokana na utayari wako unahitaji kutimiza mapenzi ya Mungu kutokana na utayari wa Moyo wako. Unaanzia pale ulipo kujitoa wewe mwenyewe, kwani hatupo sawa. Unaweza kuangalia pembeni wakati unajitoa ufanya jambo fulani, au unaweza kuangali mtu mwingine wakati unafanya jambo fulani, waweza kujikuta lile jambo hulifanyi kwa sababu unaweza kujiona kana kwamba huna pa kuanzia ama hujakamirika. Ukweli ni kwamba , tunahitaji kukamirisha kile ambacho tunacho na si kile ambacho wengine wanacho.

Ni lazima sisi wenyewe tujitoe katika kufanya jambo lililo sahihi, ikiwa unahisi kwamba hujakamirika basi ukijitoa mzima mzima kwenye jambo hilo basi utakuwa umekamirika. 2Wakorintho 8:1-3, Tena ndugu zetu, twaarifu habari ya neema ya Mungu, waliyopewa makanisa ya Makedonia; maana walipokuwa wakijaribiwa kwa dhiki nyingi, wingi wa furaha yao na umaskini wao uliokuwa mwingi uliwaongzea utajri wa ukalimu wao. Maana wanashuhudia kwamba, kwa uwezo wao, na zaidi ya uwezo wao, kwa hiyari yao wenyewe walitoa vitu vyao. Pale ambapo unahisi kana kwamba huwezi kutoa kitu, hapo ndipo unajionyesha unaweza kutoa kitu, maana mtu hawezi kuzungumzia kitu ambacho hakipo. Anzia pale ulipo na ujitoe kafara katika hilo unalotaka kufanya.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.

Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Saturday, September 29, 2018

Panda Mti Leo.

 Sadick Kilasi     September 29, 2018     NJOZI     No comments   

Mtu fulani amekaa kivuluni leo kwa sababu mtu fulani alipanda mti miaka ya nyuma.
Warren.

Upo kwa jinsi ulivyo kwa sababu Umngu alikuandaa uwe kwa jinsi ulivyo. Mshukuru Mungu kwa kukupa upekee ambao haufanani na mtu yeyote.

Tupo hapa duniani kwa sababu Mungu aliandaa dunia iwe sehemu yetu sisi kupitia kama maisha baada ya kupewa miili yetu. Mshukuru Mungu kwa hilo kwa sababu ukiwa na mwili umekuwa mkamirifu.

Una sura hiyo uliyonayo kwa sababu ya wazazi wako waliunganika kwa upendo na wakakufanya uwe wewe. Waheshimu wazazi wako na uwape shukrani.

Mtu fulani amekaa kivulini leo kwa sababu mtu fulani alipanda mti miaka ya nyuma.

Mpendwa msomaji, panda mti, panda mti ambao watu watakuja kukaa na kupata kivuli ambacho watajivunia kwa sababu ya wewe.

Fanya kitu ambacho dunia itaendelea kukumbuka hata kama haupo licha ya kwamba hutakumbukwa milele lakini angalau uishi miaka zaidi ya miaka uliyoishi.

Wewe ni barua iliyotumwa na Mungu, ni lazima upande mti ambao Mungu alikutaka uupande ili uje ulete kivuli ulimwenguni. Hakuma mtu aliyezaliwa bahati mbaya, kila mtu alizaliwa kwa kusudi lake, kama Mitume walizaliwa kuhubiri injili basi Mtume Paulo alizaliwa kusambaza injili kwa mataifa. Kila mtu amepewa kitengo cha kuendeleza pale ambapo mwenzie kafikia.

Kama upo kwenye mti uliopandwa na mtu fulani wa mwanzo basi na wewe ongeza mti mmoja zaidi ili kuonyesha kwa umekubali kilichoanzishwa na wa kale.

Panda mti leo uje ukusaidie baadae wewe mwenyewe na kizazi kijacho.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

[TAFAKARI NENO YA LEO..13] Hatupokei Haki Ya Mungu Kwa Kuomba Toba Bali Kwa Kutubu.

 Sadick Kilasi     September 29, 2018     KUFURAHIA MAISHA     No comments   

Habari rafiki yangu? Natumai umekuwa na siku njema, karibu katika tafakari neno ya leo.

Hatupokei haki ya Mungu kwa kuomba toba bali kwa kuamini na kutubu. Maneno haya yasikuchangaye rafiki yangu, ninachomaanisha ni hiki, huwezi kupokea haki ya Mungu kwa kutubu mwenyewe baada ya kuona umetenda dhambi, hapo unakuwa unajihesabia haki mwenyewe bali hujajitia chini ya Mungu.

 Watu wengi wamejikuta wanafanya toba, kila siku kwa sababu hawajaamini neno la Mungu na hujisikia kuomba toba kila siku kwa sababu wana dhambi ndani yao. Ikiwa ndivyo hivyo basi hawana Roho Mtakatifu ndani yao. Nimeamua leo nilizungumzie hili kwa sababu watu wengi ndivyo wanaishi kwa kuomba toba kila siku. Ukweli ni kwamba kama unajihisi kwamba una dhambi ndani yako na unahitaji kuomba toba, inakupasa uzaliwe upya katika injili ya maji na Roho.

Tunamwamini Mungu na kutubu, yaani, hapa tunamwamini Mungu na ikisha kubali matendo yetu na hii ndio toba ya kweli. Tunapokea ujumbe wa Mungu, ikisha tunajiweka chini ya haki ya Mungu. Hii ndio toba ya kweli.

Hatuwezi kabisa kuonyesha matendo yetu, mbele za Mungu wala huwezi kuhesabu dhambi ulizotenda mbele za Mungu. Bali tunapoamini injili ya maji na Roho, ambayo ndiyo iliyosafisha dhambi zetu pale Yesu alipobatizwa na Yohana Mbatizaji, basi ubatizo wake ndio uliotuosha dhambi zetu. Yohana Mbatizaji ndiye alimtwisha dhambi Yesu. Yohana Mbatizaji kama kuhani wa mwisha wa sheria ndiye aliyemtwisha dhambi Yesu, Yesu aliyefanyika kama mwana-kondoo wa Mungu. Yohana alifanya tendo la kikuhani kwa kumwekea dhambi Yesu kichwani mwake, Yohana alikuwa kuhani wa wanadamu.

Basi, kwa tendo hilo, dhambi yote ya ulimwengu ilichukuliwa, nasi tumebaki hatuna dhambi tena. Baada ya kuamini kwamba hatuna dhambi, sasa tunatimiza mapenzi ya Mungu kwa ujasiri, huku tukiishi kwa shukrani. Yeyote anayeamini hivi anapokea haki ya Mungu, unapaswa kuamini kama bado hujaamini, katika maji, damu na Roho. Maji ni ubatizo wake, damu ni mateso yake msalabani na Roho ni uungu wake uliomfanya afufuke baada ya kufa pale msalabani.

Ishi maisha mapya baada ya kuiamini injili hii, utapokea haki ya Mungu. Dhambi ya ulimwengu ilisha chukuliwa tangu miaka 2000 iliyopita, anayeamini tu, hupokea haki ya Mungu na kuishi mapenzi ya Mungu.

Kajifunze; 
1YOHANA 5:1-12.
1PETRO 3:21
YOHANA 19:31-37.

Asante.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Friday, September 28, 2018

Saidia Huduma Hii Kuwafikia Wengi Zaidi.

 Sadick Kilasi     September 28, 2018     SAIDIA HUDUMA HII     No comments   

Habari Ndugu, Mpendwa msomaji wa blogu hii ya JIKO LA USHAURI? Natumai huduma hii ya machapisho haya imekuwa inakusaidia. Itaendelea kukusaidia ikiwa utakuwa tayari kuchukua hatua kwa kila unalojifunza. Lengo la Mungu kunipa kipawa hichi ni kuhakikisha wengine wanapona wanapojifunza haya ninayoandika.

Kama umekuwa ni mtu wa kujifunza na kuchukua hatua natumai hivi sasa unaona mwanga katika maisha yako. Ombi langu kubwa kwako ni wewe kuendelea kujifunza lakini pia ombi langu ni wewe unisaidie kusambaza kazi hizi kuwafikia wengi zaidi. Unaweza kushare tu makala kwa marafiki zako, unaweza kuwaeleza pia marafiki juu ya blogu hii lakini pia unaweza kuitangaza blogu hii kwa mfumo wa kulipia, hii yote utakuwa umefanya kazi ya Mungu kwa nafasi yako.

Lakini pia unweza kudonate huduma hii kwa kuchangia kwa kiasi chochote kile ulichonacho. Namba zetu ni 0687000768 AIRTEL, 0659639168 TIGO NA 0755783228 VODACOM. Majina lazima yaje Sadick Lazaro Kilasi. Pia unaweza kuwasiliana nami kwa email yangu ya sadikila65gmail.com.

Nipo kwaajiri yako wewe rafiki yangu. Mungu akubariki. Asante.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Usijikinai Ndugu, Utaoza.

 Sadick Kilasi     September 28, 2018     KUFURAHIA MAISHA, NJOZI     No comments   

Kuna watu wamejikinai na maisha yao kwa sababu wamekataliwa na wale waliowapenda na  sasa wanaamini wamekosa tumaini tena, mpendwa utaoza, tena utatoa harufu mbaya, utakuwa hufai kitu. Simama maisha ni ya kwako.

Kuna watu ambao wamejikinai kwa sababu ya hofa ya mapito yao  mpendwa amka, la sivyo utaoza, utatoa harufu mbaya, utakuwa hufai kitu. Simama maisha ni ya kwako, njia bado ipo.

Kuna watu wamekinai safari yao ya mafanikio, wamejikinai kabisa, mpemdwa, utaoza, amka, dunia inakuhitaji sana wewe katika kufika mahali fulani pa kujenga watu.

Kuna watu wamejikinai mahusiano yao, mpendwa, utanuka, vaaa viatu vya utayari, la sivyo dunia itakufanya unuke. Kumbuka ulipodindoka ukajenge hapo.

Mpendwa wapo watu ambao ni mfano kwetu ambao waliishi matumaini licha ya kwamba waliteseka kwa miaka mingi mingi. Mwana mke aliyetokwa na damu miaka kumi na mbili, akatengwa na jamii lakini bado alikuwa na tumaini. Ameenda kwa waganga wengi wakashindwa lakini bado alikuwa anatumaini, hakujikinai, aliona bado fursa, alipomwona Yesu licha ya kwamba watu wengi walikuwa wamemsonga Yesu, alijiambia nafsini mwake bado hapa pana njia, nikigusa tu pindo la vazi lake kwa kidole changu nitapona, alichukua hatua, akapona.

 Mpendwa msomaji, Batimayo kipofu, licha kuishi miaka mingi kama ombaomba na kipofu lakini bado alikuwa na matumaini, hakujikinai bado alikuwa hai kwa matumaini yake, alichukua hatua alipoona fursa, aliita kwa nguvu akapata haki yake.

Watu wanaweza kukupinga, watu wanaweza kukuzalau, watu wanaweza kukuchukulia kawaida lakini kama wewe unamatumaini ishi matumaini yako. Watu wengi mnapatana kwa sababu mnaendana mnachofanya lakini siku ambayo utanuia kufanya mageuzi ya maisha yako, rafiki yako wa kwanza, hatakuwa rafiki yako wa kwanza, wengine watakupinga kabisa, wengine watasema unajidai, wengine watasema wanachotaka kusema.

Lakini nikwambie kitu kimoja lazima uwe chumvi ya ulimwengu, inayofaa kuungwa na kutumika, usifanye mambo kwa mazoea utanuka. Kuna wakati unaweza kufika upo peke yako kwa sababu ya maamuzi uliyochukua, wacha dunia ikutenge tu kwa muda, wacha wajitokeze watu ambao Mungu kakuandalia watu wa dizaini yako, wewe endelea kufanya linalofaa la sinyo utanuka utatoa harufu.

Ikiwa unaangalia watu na kusema watu watanionaje basi unahatari ya kupolopoka zaidi yao kwani wewe waonyesha upo chini yao, chukua maumivu kwa kitambo lakni ushindi upo mbele yako. La sivyo utanuka, utatoa harufu.

Usikubali kupoteza kwa sababu unahisi huna mwelekeo, njia ipo, fanya unalofanya, usikubali hisia zikuongoze, hisia zinahtaji kukufuata wewe baada ya kuchukua maamuzi, usikubali kufa moyo kwa sababu huna pa kuanzia, ndugu, kumbuka ulikuja dunia bila nguo na hata mwili ulikuwa huna, aliyekuvisha mwili atakusaidia, alikuvisha nguo hawezi kukuacha. Paza sauti yako.

Usikubali kunuka katika kila eneo la maisha, kama umeanza kufanya kitu endelea kupiga juhudi, kama hujaanza amka sasa wewe uliyekufa, nuru ikuangazie sasa, kama unahisi watu wanakutenga chukua jukumu lako dunia ndivyo ili hata Yesu mwisho wa kuelekea katika maamuzi magumu hakuna hata mwanafunzi wake aliyeogozana naye lakini mwisho alijipatia watu wengi zaidi na hata wale waliomtenga walikuwa wanamtukza. Wapo watu kwa siri wanakupenda, wapo watu kwa siri wanatamani kuwa na hicho ulichonacho, wapo watu ambao wanatamani kuwa mashabiki zako, una kila aina ya watu, chukua jukumu la maisha yako.

Kuwa na matumaini, ishi matumaini, amini matumaini yako. Wacha dunia iongee inachotaka kuongea lakini usikubali kunuka, usikubali kuwa chumvi ambayo haifai kitu, usikubali kuwa nguo kuukuu, usikubali kutoa harufu mbaya, dunia itatengeneza njia ya wewe kupita. Asante.

Kama bado hujapata kitabu cha UKRISTO NA MAISHA, ili uanze maisha mapya yenye matumaini mapya. Uwe na nguvu ya safari yako ya mafanikio. Kwa kusoma kitabu hichi na kukiamini, utapokea kipawa cha Roho Mtakatifu, ambavyo ni; uvumilivu, upendo, amani, furaha, kiasi na vingine ambavyo ni siraha katika safari ya mafanikio. Usijikinai Ngugu, utanuka, bado kunatumaini. Nisaidie kusambaza makala hii, asante.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

[TAFAKARI NENO YA LEO..12] Injili Ya Maji Na ROHO. Ubatizo Wa Yesu.

 Sadick Kilasi     September 28, 2018     KUFURAHIA MAISHA     No comments   

Kuponywa Kiroho.

Maisha ya sasa kila mtu anatamani kufika sehemu fulani. Kila mtu anapenda kufurahia maisha, lakini inakuwa ngumu kwa mtu kufurahia maisha kutoka na jinsi ndani mwake mtu alivo, kujimiliki mwenyewe inakuwa ni kazi ngumu sana. Kwa sababu mtu anashindwa kujiendeshamwenyewe bali anaendeshwa na hisia zake. Analolitaka kulifanya halifanyi bali anajikuta anafanya jambo jingine kabisa tofauti na malengo yake. Inawezekana hata wewe huwa unajikuta katika hali hii, unaweka mipango lakini hutimizi mipango yako, unajikuta tu hufanyi licha ya kwamba hicho kitu ambacho unakifanya hukipendi lakini bado wakifanya.

Wapo wengi ambao hupitia katika hali hii, nasema hili kwa sababu hata mimi nimepitia hali hii, si kwamba kwa sababu nimepitia hali hii na ndio maana nalisemea , hapana, bali ni asili ambayo hufanya kazi kwa mtu yeyote ambaye hajampokea Roho Mtakatifu. Wengi hujikuta wanatabia yakugombana na mtu licha ya kwamba yeye mwenyewe hapendi tabia hiyo lakini asili ya ndani humsukuma mtu huyo, ubinafsi wa ndani hufanya kazi kwa kiwango kikubwa sana. Ni maisha ambayo yanaumiza kwa sababu mtu anaendeshwa na hisia zake, na hana uwezo wa kukotroo hisia.


 Ukijikuta upo katika hali hii, sio kitu cha kushangaza bali ni asili ya mwanadamu ambaye hajazaliwa upya. Kwanini? Kwa sababu hata dunia ilianza katika mtumo huo huo wa ukiwa na utupu yaani hali ya kutokueleweka. MWANZO:1-2. Kwa hiyo ikiwa umejikuta katika hali hii na unaishi hali hii, Mungu tayari aliandaa mpango kuhakikisha kwamba, Roho Mtakatifu anaishi ndani yako na kuweza kukukotroo kutokana na hisia zako, wakati hujaokoka unakuwa unaendeshwa na hisia badala ya wewe kuendesha hisia zako. Kwani unapaswa kufanya maamuzi na hisia zako zifuate baadae.

Roho Mtakatifu ni Roho wa Mungu kwahiyo hawezi kukaa sehemu yenye dhambi kwani Mungu ni Nuru. Sehemu yeyote yenye mwaga giza huwa halipo, kwahiyo kama kuna giza la dhambi Roho wa Mungu hawezi kuweka makao mahali hapo. Kwa sababu mpango wa Mungu ni kuhakikisha mwanadamu anaishi maisha yenye maana ilibidi aandae mpango wa kumwokoa mwanadamu baada ya mwanadamu kufanya makosa au dhambi katika bustani ya Edeni. Dhambi ilingia kwa mtu mmoja, Adamu na watu wote wakawa katika uzao wa dhambi.

Kwa kuwa Mungu hakutaka mwanadamu aishi hivyo wakati wote, aliandaa mpango;
Mwanzo:3-15, nami naweka uadui kati yako nahuyomwanamke, nakati ya uzao wako, na uzao wake; huo atakuponda kichwa , nawe utamponda kisigino. Baada miaka mingi, toka Adamu mpaka Yohana Mbatizaji, wanadamu wote walikuwa chini ya utawala wa shetani lakini ujio wa Yesu ndio ulileta tumaini jipya kwa wanadamu. Yesu alibeba dhambi zote za ulimwengu bila kuacha dhambi yoyote. Yohana :1-29, Siku yapili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu! Huu ulikuwa ni mpango wa Mungu Yesu kuchukua dhambi ya ulimwengu ili Roho wake aishi ndani ya mioyo ya watu.

Mambo yalianzia katika ubatizo wa Yesu, alipokuwa anabatizwa na Yohana ndipo alichukua dhambi yote ya ulimwengu, akakaa na dhambi hizo kwa muda wa miaka mitatu, ili afundishe namna mpya ya kuishi baada ya ufalme wa Mungu yaani kupokea Roho wa Mungu.Baada ya hapo akateswa msalabani kwa sababu ya dhambi alizochukua wakati wa ubatizo wake, alitwishwa dhambi hizo na Yohana, mfano wake tendo la kikuhani lililokuwa linafanyika katika Agano la kale walipokuwa wanawekea mikono juu ya mbuzi, au mwana kondoo ama fahali. Mambo ya Walawi 16:23-34.[Usome]. Haya yalikuwa matendo ya kikuhani lakini yalikuwa hayaleti ukamirifu wa kuondoa dhambi kwani ilikuwa inawalazimu wana wa Israeli kurudia kufanya hivyo mara kwa mara lakni tendo alilolifanya Yesu kuchukua dhambi ya ulimwengu alifanya tendo la kikamirifu na liliondoa dhambi zote za ulimwengu.

Waebrania 10:1-12,Basi torati, kwa kuwa ni kivuli cha mema yatakayokuwa, wala si sura yenyewe ya mambo hayo, kwa dhabihu zilezile walizozitoa kila mwaka daima, haiwezi wakati wowote kuwakamirisha wakaribiao.Kama ndivyo, je! dhabihu hazingekoma kuotolewa; kwa maana waabuduo, wakisha kusafishwa mara moja, wasingejiona tena kuwa na dhambi? Lakini katika dhabihu hizo liko kumbukumbu la dhambinkila mwaka. Maana haiwezekani damu ya mafahali na na mbuzi kuondoa dhambi. Kwahiyo ajapo ulimwenguni, asema, dhabihu na toleo hukutaka, lakini mwili uliniwekea tayari; Sadaka za kuteketezwa na sadaka za dhambihukupendezwa nazo; Ndipo uliposema, tazama, nimekuja [ katika gombo la chuo nimeandikwa]. Nifanya mapenzi yako Mungu. Hapo juu asemapo, dhabihu na matoleo na sadaka za kuteketezwa na hizo dhambi hukuzitaka, wala hukupendezwa nazo [zitolewazo kama ilivyoamuru torati], ndipo aliposema tazama nimekuja, nifanye mapenzi yako. Andoa la kwanza ilikusudi asimamishe la pili. Katika mapenzi hayo mmepata utakaso, kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu. Na kila kuhani husimama kila siku akifanya ibada, na kutoa dhabihu zile zile mara nyingi; ambazo haziwezi kabisa kuondoa dhambi. Lakini huyu, alipokwisha kutoa kwajili ya dhambi moja idumuyo hata milele, aliketi mkono wa kuume wa Mungu,

Yesu aliondoa dhambi zote za matendo na za asili, alipobatizwa. Ubatizo aliokuwa unaufanya sio kuondoa matendo ya nje ya mwili, hapana, ila katika dhamiri ya mtu. Alifanya hivyo ili kuweka ufunuo katika neno lake. Kwani bila kufunuliwa na Mungu ama kama hujampokea Roho Mtakatifu huwezi kusoma neno la Mungu. 1Petro 3:21, Mfano wa mambo hayo ni ubatizo, unawaokoa ninyi pia siku hizi; [siyo kuwekea mbali uchafu wa mwili, bali jibu la dhamiri safi mbele za Mungu], kwa kufufuka kwake Yesu Kristo.  Mungu alisafisha dhamiri ya mtu kwani bila hilo tusingeweza kusoma neno la Mungu. Mioyo ya watu ni mizito kuelewa isipofunuliwa na Mungu lakni Yesu alifanya hivyo na akamweka mtu aendelee kufunuliwa zaidi na zaidi pale anaposoma neno la Mungu, na Roho Mtakatifu hufunulia zaidi siri za Mungu mtu huyo kwani Roho Mtakatifu na Neno la Mungu ni sawa, hupatana.

Kwahiyo unapoamini katika injili hii, ndipo unafanyika kuwa huna dhambi baada ya dhambi zako kusafishwa na hii haitegemei sara za toba bali imani yako kwani tendo hili tayari lilisha kamirika. Roho Mtakatifu ataweka makazi ndani yako na ataanza kukotroo hali yako sasa kile ambacho utamua ndicho utakifanya. Yapo matunda ya Roho Mtakatifu; upendo, uvumilivu, amani, imani, fadhili na moyo wa kiasi. Moyo wa kiasi unakusaidia kujithibiti mwenyewe. Injili ya Maji na Roho ndiyo injili ya kweli. Mtu hawezi kuzaliwa mara yapili bila hii, kwani katika Agano la kale ilikuwa inasafisha dhambi za wana wa Israeli japo haikuwapa ukamirifu kilikuwa ni kivuli cha injili hii ya sasa. Maji, Damu na Roho. NDIYO INAYOTUOKOA HIVI SASA.

Ikiwa utaiamini injili hii, utaomba lolote na Mungu atakupa kwani tayari ndani yako kuna tunda la imani. Ni kuamini tu, basi ndipo utapokea haki ya MUNGU. Karibu kwa swali lolote, nitumie ujumbe kama una swali, lakini ili kuijua zaidi injili hii hakikisha unajipatia kitabu cha UKRISTO NA MAISHA.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Thursday, September 27, 2018

Utukufu Ni Wa Mungu.

 Sadick Kilasi     September 27, 2018     TAFAKARI YA ROHO     No comments   

Mungu ndiye mwanzo wa kila kitu, Mungu ndiye aliyeumba kila kitu, utukufu ni wake.
Mungu ndiye aliyeumba mbingu na nchi, utukufu ni wake.
Mungu ndiye aliyeifanya nchi na kuiweka misingi yake juu ya anga na isitikisike, utukufu ni wake Mungu.

Mwenyezi Mungu ndiye aliyefanya bahari, bahari ambayo maji ya mito huingia humo kila siku lakini haijai, utukufu ni wake Mungu.
Mwenyezi Mungu aliweka misingi ya nchi na kila kitu kwa asili yake na majira, jua huchomoza kila siku na kuzama katika mhimili uleule, amefanya usiku na mchana katika mwonekano uleule, hizo ni hekima za Mwenyezi Mungu, utukufu ni wake Mungu.

Tunamshukuru Mwenyezi Mungu ambaye hubadilisha watu kwa wakati wake na majira yake, maana Mwemyezi Mungu humpa mtu mwingine welevu na hekima yake kwa wakati wake, hizo nazo ni hekima za Mungu, utukufu ni wake. Mwambie Mungu asante kwa sababu umenifanya nijisifie kwamba mimi nina hichi na hichi, kwani unahesabu kwa sababu mwingine hana, mpende adui yako kwa sababu anakufanya ujisifie, hizo zote ni hekima Mwenyezi Mungu, utukufu ni wake.

Mwenyezi Mungu ni waajabu, hakuna anaye mzidi utukufu wake, kaficha hekima zake, lakini huwafumbulia watu hekima zake pole pole ili waweze kufurahia maisha wakati wanachunguza hekima za Mungu, utukufu ni wake Mungu.

Liangalie giza la usiku, lichunguze kwa umakini sana, utagundua ndani yake kuna nuru kidogo, utagundua kwamba kuna giza totoro na kuna giza lisilo totoro. Giza nalo hutumainia kuwa kama nyota, nyota nazo hutumainia kuwa kama mwezi, na mwezi nao hutumainia kuwa kama jua na jua nalo hutumaini kama kuwa utukufu wa Mwenyezi Mungu; hizo na siri na hekima zake Mwenyezi Mungu, utukufu ni wake.

Chunguza chunguza kwa umakini, mwanasayansi huchunguza hekima za Mungu, hufurahia akipata majibu mazuri lakini majibu yake huwa hayafikii utukufu wa Mungu, Mungu aliumba umeme wa jua huwa haukatiki hata siku moja, humulika dunia nzima lakini umeme wa Tanesco kila siku kilio. Misingi ya Mwenyezi Mungu haitikisiki wala haingiliki, hizo nazo ni hekima za Mungu, utukufu ni wake.

Mwangalie sisimizi mdogo sana, waweza kujiuliza uhai wake wakaa wapi? chakula chake hukaa wapi? emeubwajeubwaje? Hujitafutia chakula, huchimba mashimo ya kuishi na kufanya mambo ya ajabu utazani mwanadamu, huyo ni sisimizi mdudu mdogo sana. Hizo nazo ni hekima za Mungu, utukufu ni wake.

Jichunguze jinsi ulivo, jiangalie angalie, kitu gani kinakufanya unakaa? kitu gani kinakufanya unatembea? kitu gani kimekufanya gozi yako iwe kama ilivyo? Hebu, rudisha macho yako kwenye macho yako, jiule kwanini macho yako? Angalia mdomo jinsi ulivo, unaongea. Mwanasayansi atachunguza na kuleta maoni yake, kwani Mwenyezi Mungu ni mwanzo wa yote  na hekima ni zake na utukufu ni wake.

Ndugu yangu, rafiki yangu, mwambie Mungu asante, rudia tena na tena, Mungu amekupa utashi, akili ya kuelewa mazingira ili utawale visivyo eleweka, hekima zote ni za Mungu, yeye ndiye mwanzo, sasa na mwisho. Utukufu ni wake, hekima ni zake. Ukubali kwamba Mungu kakupa kila kitu, kakupa utawale kwa nafasi yako. Mtukuze Mwenyezi Mungu, mwambie Mungu asante kwa hekima zako. Ninafurahia ulichonipa.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

[TAFAKARI NENO YA LEO..11] Je! Ufanye Nini Wakati Unapitia Wakati Mgumu?

 Sadick Kilasi     September 27, 2018     TAFAKARI YA ROHO     No comments   

Sio kwamba ukiokoka huta pitia wakati mgumu. Ili mradi tu upo duniani lazima upitie hali tofautitofauti. Lazima utambue kwamba kila kinachokutokea kinasababu. Hatua ulizopiga hapo nyuma ndizo zilizokupelekea kuwa hapo ulipo kwenye uchungu. Tunajengeka kupitia magumu ambayo tunapiti na ndio maana inapaswa ukubali kwamba ni lazima upitie katika hali tofauti.

Je! utafanya nini wakati ambao mambo hayaendi kama vile yanavyopaswa kwenda? Utafanya nini pale ambapo unapaswa kuvuka kiunzi kilichowekwa mbele yako ili kikupime ulivyo na ubunifu?

Kutoka 15:23-26, Walipofika mahali palipoitwa Mara hawakupata kuyanywa maji yale ya Mara; kwa kuwa yalikuwa machungu; kwa ajili ya hiyo jina lake likaitwa Mara. Ndipo watu wakamnung'unikia Musa, wakisema, tunywe nini?Naye akamlilia Bwana; Bwana akamwonyesha mti, naye akautia katika hayo maji, maji yakawa matamu. Basi akawawekea amri na hukumu huko, akawaonja huko; akawambia, kwamba utaisikiza kwa bidii sauti ya Bwana, Mungu wako, na kuyafanya yaliyoelekea mbele zake, na kutega masikio usikie maagizo yake, na kushika amri zake, mimi sitatia juu yako maradhi yoyote niliyowatia Wamisri; kwa kuwa mimi ndimi Bwana nikuponyaye.

Kitu ambacho unapaswa kuelewa wakati unapitia magumu ni kwamba , wakati huo ni wakati wa kujengwa, wakati wa kujifunza. Lakini lazima uelewe kwamba, Mungu ameweka kanuni ambayo unapaswa kuifuata ili kusikia sauti hii wakati huu mgumu.

Kwanza kabisa Mungu amesema, unahitajika kuwa mtulivu sana, na utasikiliza kwa bidii sana sauti ya Roho Mtakatifu, na kufanya lile jambo ambalo Mungu amekuelekeza ufanye. Sasa hapa lazima utambue kwamba, unahitaji utulivu mkubwa sana na ile sauti ya kwanza ambayo Mungu kakuonyesha uifanye ndiyo hiyo hiyo. Unatulia kimya harafu kitakacho kuja ambacho umesikia kutoka ndani kabisa ya Roho yako hicho ndicho ufanye.

Lakini lazima utambue kitu kimoja, kwamba lazima uwe mtu ambaye unazitii sheria za Mungu na maagizo yake. Ni lazima kwanza uwe unamwamini Mungu na ndipo utapata kile ambacho unahitaji.

Kwa hiyo magumu katika maisha yapo lakini kwa watu ambao wanautayari wa kuishi na kukubali mazingira wanayopiti hawahesabu, wakati huu kama wakati wa kujijenga. Tunajijenga kupitia magumu, sasa kama unafikiri kufurahi wakati wa mema pekee, basi, hapa unahitaji kuelewa hili kwamba, wakati wote ni sahihi kwa mwenye shukrani na kuona wema kwenye kila jambo.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Wednesday, September 26, 2018

Watu Hawatakosa La Kusema, Endelea Kufanya Unachopwa Kufanya.

 Sadick Kilasi     September 26, 2018     NJOZI     No comments   

Sio kila mtu atakuwa sawa na wewe kwa lile unalofanya. Wengine watakujaji kama wanavotaka wao, wengine watakuunga mkono, wengine watakwambia kitu, wengine hawatasema kitu ila wana kitu ama maoni ndani yao. Sio wote watakuwa sawa.

Kama unachofanya hakikuumizi mwenyewe wala hakimuumizi mwingine, fanya, hata kama utapokea maoni ambayo yapo kinyume na wewe na kwa asilimia themanini maoni yatakupinga.

Ndugu yangu, kuna mtu alipingwa kama Yesu? Alipigwa bila makosa yoyote. Dunia inataka kufanya kile ambacho kimezoeleka na wao lakini ukija na jambo jipya watu watakupinga na kukuona hufai kabisa.

Mathayo 11:16-19, Basi, nitakifananisha kizazi hiki na kitu gani?Ni kama vijana waliokuwa wamekaa uwanjani, wakawa wakiambiana kikundi kimoja na kingine: Tumewapigieni ngoma lakini hamkucheza! Tumeimba nyimbo za huzuni lakini hamkuomboleza! Kwa maana Yohane alikuja, akafunga na wala hakunywa divai, nao wakasema: amepagawa na pepo. Mwana wa mtu akaja, anakula na kunywa, nao wakasema, rafikiao watoza ushuru na wenye dhambi!Hata hivyo, hekima ya Mungu itadhibitisha kuwa njema, kutokana na matendo yake.

Kama hao walipingwa na ndio hao leo hii wamefanya sisi kutokuwa na dhambi, je! wewe kwanini usipingwe? Endelea kufanya kwa sababu unapaswa kufanya, endelea kufanya kwa sababu unajenga watu, endelea kufanya kwa sababu malengo yako ni kujenga na wala sio kupomoa. Siku moja unachokifanya kitathibitisha kwamba kusudi lako lilikuwa ni nini?

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

[TAFAKARI NENO YA LEO...10] Hamna Namna, Mshangaze Jirani Yako.

 Sadick Kilasi     September 26, 2018     MAHUSIANO     No comments   

Fikiri kama unaishi katika kijiji fulani, kijiji ambacho kila mtu anaishi upekee wa pekee yake, yaani kila mtu  anajari tu ya kwake. Kuna msemo mmoja ambao watu wengi wamekuwa wanautumia ktika maisha yao, natafuta hela ya kula tu. Kiukweli ni msemo ambao umekaa kibinafsi sana, lakini haishangazi kwani hiyo ndio asili ya dunia. Dunia hukazana kukusanya vitu lakini kwa bahati mbaya vitu hivyo huishia kufa na kunuka na baadae kurudi vilikotoka.

Lakini kwa sababu wewe si wa dunia hii, wewe unakazana kuacha alama na kutoa thamani kwa wengine, hauna namna, ishangaze dunia, mshangaze jirani yako ambaye hukumbatia alichonacho bila kuwapa wengine. Dunia inaamini kwamba unatakiwa kukusanya vitu, inakosa utambuzi kwamba, unatakiwa kubarikiwa na kutawanya.

Huna namna rafiki yangu, mshangaze jirani yako, muonyeshe kipaji ulichonacho kwamba kinaweza kumfariji hata yeye. Huna namna rafiki yangu muonyeshe jirani yako kwamba unaweza kumshangaza kwa kumsaidia chochote kile ambacho anahitaji kufanyiwa.

Hata kama upo katika hali gani una cha kuanzia. Kuna msemo unaosema, Anzia popote ulipo, ikiwezekana, kimbia lakini kama huwezi kukimbiatroti. lakini pia kama huwezi kutroti, tembea, lakini pia kama huwezi kutembea tambaa, lakini pia kama huwezi kutambaa, tikisa hata mguu. Kama unaishi kwenye kijiji ambacho kila mtu anaishi kivyake waoneshe watu kwamba mnaweza kunya lolote ili kufanya mageuzi ya upendo.

Jitaidi kuanza kufikiria ni namna gani ambavyo unaweza kuishangaza jamii, jitaidi kufikiri mawazo ya upendo, ni namna gani unaweza kuifanya jamii ikapata ulichonacho. Kila mtu anacho cha kuanzia, tulianza tukiwa na mwili pekee bila hata mavazi, hata kujikuna kwenyewe tulikuwa hatuwezi, lakini baadae tukaanza kuvaa nguo. baadae kutambaa, mpaka sasa tupotukiwa sawa na bado tunaendelea kusonga mbele.

Huwa inanishangaza kuona kwamba, japokuwa tulipokuwa wadogo, tulionekana hatuna lolote lakini tulionyesha tulichonacho. Tulitoa tulichonacho ndani, tulianza kutambaa, tukaanza kutembea lakini baadae dunia ikatufundisha kinyume cha hayo, badala yake dunia ikaanza kutuonyesha kwamba tunahitaji kupokea tu, ikatufanya kuwa wadhaifu, tunaohitaji kusaidiwa wakati wote. Mpendwa msomaji, tuurudi utoto wetu, tuwe kama hatuwezi kitu ili tutoe kile kilicho ndani yetu kwa bidii kubwa. Maana neno linasema, mtu asipoongoka kuwa kama mtoto hawezi kuuona ufalme wa Mungu.

Anza kufikiri tofauti, anza kufikiri namna gani unaweza kujifunza kwa kasi ya utoto na kutoa ulichonacho kwa kasi ya utoto. Haijarishi, fikiri mawazo ya kiupendo.
Unaweza kuanza kuwapongeza watu labda kila siku watu wawili, kwa maeneo ambayo yabo bora lakini mabaya usiyaongelee.
Unaweza kuanza kutoa msaada wa mia tano kwa yule ambaye unasukumwa kufanya hivyo.
Unaweza kuanza kumpisha mtu siti ndani ya daladala.

Dunia hii, ina njaa ya upendo, dunia hii, inautele wa kibinafsi, dunia hii, inautele wa mtazamo hasi. Usifikiri namna ya dunia. Angalia namna ambavyo unaweza kufanya lolote.

Siyo mbaya ukimwambia adi yako nakupenda. Unayo madhabahu ambayo huzi kujihudumia mwenyewe, uahitaji asiye nacho ili ukamirishe usawa na kujali utofauti ulionao.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Tuesday, September 25, 2018

Endelea Kufanya Yanayofaa.

 Sadick Kilasi     September 25, 2018     NJOZI     No comments   

Habari Ndugu?
Siku nyingine tena, Mungu ametuamsha, nguvu ni zake na kila kitu ni chake. Yeye anatambua kila kitu kuhusu sisi kwahiyo ni vema tukaomba mwongozo wake katika hatua zetu za maisha yetu.

Mpendwa rafiki, siku hii ya leo, endelea kufanya dunia kuwa sehemu ya amani, endelea kutia juhudi katika kazi zako, endelea kusoma neno la Mungu, endelea kitia juhudi katika kazi zako, endelea kusoma wema katika kila jambo, endelea kufanya maombi kila wakati, endelea kuishi kwa shukrani katika kila jambo, endelea kujifunza yaliyo mema, endelea kuwatia hamasa wale wanaokusaidia, endelea kujijenga katika tabia nzuri, endelea kusamehe kabla ya kukosewa, endelea, endelea, endelea.

Asante.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

[TAFAKARI NENO YA LEO...9] Ukimpokea Yesu Onyesha Kwa Matendo Kwamba Umeamini.

 Sadick Kilasi     September 25, 2018     KUFURAHIA MAISHA     No comments   

Karibu katika tafakari neno ya leo. Kama ulivyo utaratibu wa kila siku, mtu hataishi kwa mkate bali na kwa neno la Mungu.

Tafakari yetu ni ukimpokea Yesu onyesha kwa matendo kwamba umeamini.

Ubatizo wa Yohana ni ubatizo wa toba. Na huu ni ubatizo ambao unakuhitaji uchukue hatua fulani kwamba kweli umeamini, unaonyesha kwa matendo kwamba kweli umeamini kwamba Yesu ni Kristo. Ubatizo wa huu unasafisha dhamiri ya mtu, ndio huu ubatizo wa maji, utaanza kufanya matendo ya kufanya sala, shukrani na hapo ndipo Yesu humchunguza mtu, ikisha humbatiza kwa Roho Mtakatifu.

Kwa hiyo ikiwa kweli umeiamini injili ya Maji na Roho, unapaswa kuonyesha kwa matendo kwamba, kweli nimeamini.

Marko 11:7-17, Wakamletea Yesu yule Mwana -punda, wakatandika mavazi yao juu yake; akaketi juu yake. Watu wengi wakatandaza mavazi yao njiani, na wengine matawi waliyoyakata shambani. Nao watu waliotangulia na wale waliofuata wakapaza sauti, Hosana; ndiye mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana; umebarikiwa na ufalme ujao, wa baba yetu Daudi. Hosana juu mbinguni. Naye akaingia Yerusalemu hata ndani ya hekalu; na alipokwisha kutazama yote  pande zote, kwa kuwa ni wakati wajioni, akatoka, akaenda Bethania pamoja na wale Thenashara. Hata asubuhi yake alipotoka Bethania aliona njaa. Akaona kwa mbali mtini wenye majani, akaenda labda ili aone kitu juu yake; na alipoufikilia hakuona kitu ila majani; maana si wakati wa tini. Akajibu, akauambia, tangu leo hata milele mtu asile matunda kwako. Wanafunzi wake wakasikia. Wakafika Yerusalemu, naye akaingia ndani ya hekalu, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza na kununua ndani ya hekalu, akazipindua neza za wabadili fedha, na viti vyao wauzao njiwa; wala hakuacha mtu achukue chombo kati ya hekalu. Akafundisha, akasema, Je! Haikuandikwa, numba yangu itakuwa nyumba ya sala kwa mataifa yote? Bali nyinyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi.

Tumeona hatua tatu, kumpokea Yesu, mtini kulaniwa na Yesu kufukuza wafanya biashara hekaluni. Kama hutoonyesha kwa matendo huwezi kubatizwa  Roho Mtakatifu, utalaaniwa kama mtini lakini kama ukiamini Yesu atakusafisha  kwa damu yake zile dhambi za rohoni kabisa na hii ndio maana ya kufukuza wafanyabiashara hekaluni.

Lazima utambue kwamba, Mungu aliuandaa mji wa Yerusalemu ili watakatifu waabudu humo lakini pia ndani ya mji huo lilijengwa hekalu la Mungu, watu waliokuwa wanaishi katika mji wa Yerusalemu walikuwa wanaabudu katika hekalu hilo, ukiwaona utatambua kwamba hawa ni watu wanaoabudu katika hekelu takatifu la Yerusalemu.

Kwa sasa tunaubatizo wa maji na damu, mji wa Yerusalemu na hekalu la Yerusalemu, patakatifu na patakatifu sana. Ninachomaanisha ni hiki, ikiwa unamwamini Yesu ni lazima ufanye yale ambayo yanaonyesha kwamba umeamini, na baadae Yesu atakusaidia kwa sababu umeonyesha ushirikiano kwa kukuonyesha yale ambayo wewe huyawezi.

Ikiwa unamwamini Yesu ni lazima uchukue hatua zinazoonyesha kwamba umeamini. Thamiri yako ilisafishwa matendo na dhamiri yako yalioshwa katika mto Yordani pale Yohana alipomwekea mikono juu ya kichwa chake. Lakini zile dhambi za rohoni kabisa ambazo wewe huwezi hata kuzikotroo kwa damu yake Yesu aliosha. Onesha kwamba umeamini, timiza mapenzi ya Mungu, soma neno, neno la Mungu litasafisha zaidi na zaidi na zaidi dhamiri yako lakini Roho Mtakatifu nae atakuletea siri za Mungu. Samehe watu nawe utasamehewa. Onyesha ushirikiano na Mungu. ASANTE.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Hii ndio Njaa Kubwa Ya Dunia Ya Sasa.

 Sadick Kilasi     September 25, 2018     MAHUSIANO     No comments   

Njaa kubwa ya dunia ya leo ni kukamirisha utupu uliopo ndani ya mtu. Wakati Mungu alipomwumba Adamu alimfanya utupu kwa kuondoa sehemu ya ubavu wake.

Changamoto kubwa tulionayo kwa sasa ni kwamba kila mtu anataka tu yeye, watu wote wapo upande mmoja. Hayupo mtu ambaye yupo tayari kuchukua madhaifu ya mwingine. Kila mtu atakwambia nampenda anayenipennda. Rafiki yangu, hii inaleta maana, kila mtu anataka kupendwa tu, sasa nani atampenda mwenzie? Leo hii hata mwanzo wa ndoa, watu wanajaribiana kwanza tabia, je hii inaleta maana? Je, chanya kwa chanya zinaweza kujifiti kwa pamoja. Mwanaume alitolewa ubavu wake ili autafute ubavu wake, mwanamke anapaswa kufitisha lile pengo na mwisho wawe mwili mmoja. Mpendwa msomaji, upendo wa kweli ni kupenda kisicho pendeka.

Mwanzo 2:21-24, Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito,naye akalala, kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake, na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akamfanya mwanamke, akamleta kwa Adamu. Adamu akasema sasa huyu ni mifipa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi, ataitwa mwanamke kwa sababu ametwaliwa katika mwanamme. Kwa hiyo mwanamme na mwanamke atamwacha baba na mama yake, naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja. 
Rafiki, sizungumzii upendo wa mke na mme tu, nazungumzia upendo wote kwa ujumla. Kamilisha upendo penda pale palipokosa upendo.

Mpendwa msomaji, njaa kubwa ya watu hivi sasa, kufarijiana. Watu wanahitaji kufarijiwa lakini ni nani atakaye wafariji, ni nani atakaye amsha mioyo iliyovunjika? Kila mtu anahitaji kufarijiwa, usimwangalie mtu kwa nje tu, watu wamekosa hamasa katika maisha yao. Wanahitaji neno kutoka kwako wewe rafiki yangu, neno la matumaini. Haihitaji gharama kusema neno, haihitaji gharama kumsifiamtuambaye amekufanyia mambo mazuri, hata kama ni kidogo kiasi gani. Kiimani mambo madogo ndio makubwa sana. Anza kujari mambo madogomadogo ambayo watu wanakufanyia, utabadilika wewe binafsi hata wengine pia itakuwa njema kwao.

Tumia maneno kama asante, hongera, kazi yako ni nzuri, umependeza na mengine mengi kutokana na mazingira ambayo upo. Tena zidisha zaidi kwa adui zako. Weka mpango hivi sasa, wafariji watu angalau wawili kila siku, kwa maneno tu. Chagua wale watu ambao hamuendani ili ukamirishe faraja.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Monday, September 24, 2018

Tumia Makombo Ya Wakati Wako Kujisomea Neno La Mungu.

 Sadick Kilasi     September 24, 2018     No comments   

Tumia Makombo Ya Wakati Kusoma Neno La Mungu.

Biblia kama kitabu kitakatifu kinaukweli wa uhalisia ambao hauwezi kubadilika kamwe. Biblia ni kitabu ambacho kimejaa uhalisia wa mambo yasiyobadilika. Kwa mujibu wa utafiti wa watu, Biblia ndio kitabu cha kale au zaidi duniani. Miaka yote kimekuwa kinazungumza ukweli wa uhalisi, mambo mengi yalitabiriwa na yamekuja kuwa halisi katika dunia. Kitabu cha biblia, kimejaa maneno matakatifu ambayo ni halisi. Kwa yeyote ambaye anasoma atapata uhalisia wa mambo.

Pamoja na kuwa Biblia ni kitabu cha kale zaidi duuniani lakini bado mambo yake, yalioyomo kwenye neno yamekuwa yakifanya kazi mpaka sasa, kweli neno la Mungu ni upanga usioisha makali. Biblia ndicho kitabu ambacho kina nakala ningi zaidi duniani, ni kitabu ambacho ni rahisi zaidi kupatikana kila mahala na kila nyumba. Leo hii kila nyumba ya Kikristo, walio wengi wanabiblia.

Maneno ya kwenye Biblia yamejaa uzima wa kiroho, kiakili na kimwili pia. Lakini pamoja na kuwa Biblia ndio kitabu ambacho kinapatikana zaidi kwenye nyumba za watu lakini pia ni kitabu ambacho hakichukuliwi kwa umanane na kusomwa. Watu wengi hawasomi Biblia, wamenunua biblia kutokana tu na tabia za kidini. Siku zote watu huishia kutazama tu, na kutambua tu kwamba hii ni Biblia lakini kilicho ndani kwao ni giza tu.

Biblia ni kitabu ambacho kinaweza kukupa matumaini mapya, biblia ni kitabu ambacho kinaweza kukuonyesha kusudi la maisha yako, Biblia ni kitabu ambacho kinaweza kukuelezea uhalisia wako wewe ni nani hasa, biblia ni kitabu ambacho kinaweza uone mazingira unayoishi na sio kuishia kutazama tu, biblia ni kitabu ambacho kinaweza kuwa na wewe wakati wa changamoto, biblia ni kitabu ambacho kinaweza kuboresha mahusiano yako, biblia ni kitabu ambacho kimejaa kanuni za kibiashara, kwahiyo kwa kutumia kanuni za kiblia ukafanikiwa kwenye biashara yako, biblia ni kitabu ambacho kitakufa uwe na njozi ya maisha yako ya baadae baada ya kifo, bilia ni kitabu ambacho kitakueleza kifo ni nini, biblia ni kitabu ambacho kitasafisha akilia yako kabisa, biblia ni kitabu ambacho kitakufanya uumiliki ukweli badala ya kuambiwa tu na kufundishwa, biblia ni kioo cha wewe, biblia ni kioo cha kuwaona wengine na mengina mengi yamo kwenye biblia.

Kutokana na faida nyingi ambazo zipo wazi na ndiomaana nakuletea kanuni hii ya [tumia makombo ya muda wako kujisomea neno la Mungu.] Kanuni hii ni kanuni ambayo ipo kwenye biblia na ndio maana nimekwambia, kila hatua ya maisha yako biblia inaweza kukuelekeza cha kufanya na kubadili kabisa maisha yako.

Mathayo 15:21-28, Yesu aliondoka mahali hapo akaenda kukaa katika sehemu za Tiro na Sidoni. Basi, mama mmoja Mkaanani wa nchi hiyo alimjia, akapaza sauti, Bwana, Mwana wa Daudi,nionee huruma! binti yangu anasunbuliwa na pepo. Lakini Yesu hakumjibu neno. Basi, wanafunzi wake wakamwendea, wakamwambia, mwambia aende zake kwa maana anatufuatafuata kipiga kelele. Yesu akamjibu, sikutumwa ila kwa watu wa Israeli waliopotea kama kondoo. Hapo huyo mama akaja, akamsujudia, akasema, Bwana, nisaidie. Yesu akasema, si vizuri kuchukua chakula cha watoto na kuttupia mbwa. Huyo mama akajibu, ni kweli Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yanayoanguka kutoka meza ya bwana wao. Hapo Yesu akamjibu, Mama, imani yako ni kubwa, basi, ufanyiwe kama unavotaka. Yule binti yake akapona wakati huohuo.

Lengo lako ni kula chakula lakini mabaki yanayobaki mbwa hula naye hupata haki yake. Lengo lako ni kusafiri lakini unamakombo ya wakati wakati unasafiri, tumia muda huo kusoma neno la Mungu, lengo lako ni kuuza duka lakini unamakombo ya wakati unaposubiri wateja, tumia wakati huo kusoma neno la Mungu, lengo lako ni kwenda mahala fulani lakini safari ni ndefu tumia wakati huo kusoma neno la Mungu, tumia kila makombo ya wakati wako kusoma neno la Mungu. Uzuri wa siku hizi kunna biblia za kidikitali kwa hiyo ni rahisi kusoma neno popote pale ulipo kwenye simu hizi za kisasa. Wakati mwingine, tumia muda mtaktifu na sio makombo ya muda.  Kama bado hujadownload biblia basi hakikisha unafanya hivyo ilikutumia muda vizuri.

Karibu kwenye Group letu la SURA YA UKWELI, ambapo tutakuwa tunashirikiana kwa pamoja yale ambayo tumejifunza kwa siku hiyo kutoka kwenye Biblia. Na pia itakuwa ni rahisi kuelewesha mambo mbalimbali na kuulizana maswali juu ya neno la Mungu. Napenda niwe pamoja nawe katika kusoma Biblia. Moja ya malengo yangu ni kusoma biblia kuhubiri injili ambayo imeniponya mimi mwenyewe, injili ya maji na Roho, na kuwasaidia watu, kutokana na mazingira wanayoishi, biblia ni kitabu ambacho kinaweza kukupa matumaini mapya. Karibu rafiki yangu, karibu rafiki yangu tuwe pamoja katika group hili, karibu tuuchimbue madini yaliyofichika, karibu tuijue uhakisia wa mambo, karibu tujengane kwa pamoja. Ili kujiunga na Group nitumie ujumbe wa whatsap ili nikuunge moja kwa moja kwenye Group. 0687000768 au kama unaona vipi unaweza kunitumia ujumbe kwa sadikila65@gmail.com. Lengo kubwa ni kusoma biblia na kutafuta uhalisia wa mambo. Lakini pia nitaendesha darasa la kuitambua kwa undani Injili ya Maji na Roho. Karibu sana rafiki yangu tuwe pamoja.

Hakikisha pia kama hujapata kitabu cha UKRISTO NA MAISHA, KUWA NA MATUMAINI, NISAIDIE NAOGOPA, jipatie zawadi hizi za vitabu.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mwasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Naomba Uniambie Rafiki Yangu, Unaishije Na Watu Wakati Wewe Hawakuelewi?

 Sadick Kilasi     September 24, 2018     KUFURAHIA MAISHA, MAHUSIANO     No comments   

Ukiwa mpole sana watu watakuonea sana lakini pia ukiwa mkali sana watu wa watakuona kana kwamba wewe ni katili na hufai kuishi na wao. Swali langu kwako wewe rafiki yangu, unaishije na watu, wakati hawakuelewi?

Ukionewa sana utafadhaika sana inamaana utakosa amani na wewe na kwa wengine. Ukiwa mkali sana utakosa watu wa kuishi nao. Nambie rafiki yangu unaishije na watu, wakati hawakuelewi?

Watu hawakuelewi kabisa unachowaza kwa sababu wewe ni kivuli cha wewe. Wewe ni msiri sana kwa wengine kwa sababu hawaoni ndani mwako. Je, unaishi na watu kama wao wanavotaka? Au unapingana nao kabisa kwa ukari?


Nipe jibu rafiki yangu, kwa kunitumia ujumbe, ama kutoa maoni yako.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Sunday, September 23, 2018

Una Shina La Kukupeleka Katika Ushindi.

 Sadick Kilasi     September 23, 2018     MAHUSIANO     No comments   

Kila mmoja amezaliwa akiwa amewekewa kipawa cha kipekee ndani yake. Hicho ndicho kiyu ambacho Mungu ameweka ndani yake. Ni shina ambalo likikua baadae huzaa mtawi mengi sana. Kama ilivyo Mungu, Mungu ndiye shina wa kila kitu hapa duniani, vitu vyote vilivyopo duniani yeye ndiye mwanzo wa kila kitu.

Mungu alivotuumba hata sisi alituweka katika mfumo wa namna hiyo. Kila mmoja ana shina lake. Kipawa ambacho ni cha kuzaliwa. Wengine ni wahamasishaji, wengine ni walimu, wengine ni wachezaji, wengine ni waimbaji, wengine ni wataalamu wa mahusino, wengine wafariji na kadharika. Hivi vyote ni vipawa ambavyo mtu huwa anakuwa nacho.

Lakini pamoja na kuwa na vipawa hivi, bado tunahitaji matawi ili tuweze kukamirika. Na hapa ndipo tunahitaji kujifunza kutoka kwa wengine, na kwa ujumla sisi binadamu tunahitajiana katika maeneo mbalimbali. Warumi12:4-9, Mwili una viungo vingi kila kimoja kina kazi yake. Hali kadharika ingawa sisi ni wengi,  tu mwili mmoja kwa kuungana na Kristo, na kila mmoja ni kiungo cha mwenzake. Basi, tunavyo vipaji mbalimbali kadiri ya neema tuliyopewa. Mwenye kipaji cha unabii na akitumie kwa kadili ya imani yake. Mwenye kipaji cha utumishi na atumike. mwenye kipaji cha kufundisha na afundishe. Mwenye kipaji cha kuwafariji wengine na afanye hivyo. Mwenye kuwagawia wenzake alichonacho na afanye hivyo kwa ukarimu. Msimamizi na asimamie kwa bidii; naye mwenye kutenda jambo kwa huruma na afanye hivyo kwa furaha. Mapendano yenu na yawe bila unafiki wowote. Chukieni jambo lolote ovu, na zingatieni jema.

 Katika maisha tunayoishi tumepewa vipawa mbalimbali na kwa watu tofauti, kila mmoja na kipawa chake lakini bado tunahitajiana ktokana na mapungufu tuliyonayo. Duniani huwa tunakazania maisha ya usawa lakini hatuwezi kuufikia usawa, tutashindwa kuhudumiana. Lakini utofauti wetu uwe ni ubora wa kujariana kwa mapendo ya kweli.

 Kwa hiyo rafiki yangu angalia maeneo ambayo unahisi ni kipawa chako na anza kutumia kuwasaidia wengine kipawa chako. Binafsi nilijijua kwamba ninakipawa cha kutafakari maneno magumu [lugha]. Japo mimi sio msomi lakini nilijielewa hivyo ndivyo nilivyo. Lakini pia nilijielewa kwamba ninamapungufu katika kuhusiana na watu. Siwezi kujenga mahusiano na watu kwa muda mrefu. Na hili linanifanya niwe tayari kuweka mpango ili kuwa na watu ambao mpo kwa pamoja katika kuhudumiana.

Kwahiyo kila mmoja amepewa kianzio na hii yote ni kuhakikisha kwamba maisha ya kila mtu yanakuwa bora kutokana na utofauti. Tunahitajiana , aliyenacho anamhitaji asiye nacho na asiye nacho anamhitaji aliye nacho.

Karibu katika group la SURA YA UKWELI, ili tuhudumiane tujifunze mengi. Pia hakikisha unapata kitabu cha UKRISTO NA MAISHA kama bado hujapata nakala yako. Asante.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Je! Mungu Atakuwepo Au Hatakuwepo?

 Sadick Kilasi     September 23, 2018     TAFAKARI YA ROHO     No comments   

Siku zote watu hawanauhakika na siku watakapokufa, baada ya kifo, itatokea nini? Je Mungu yupo huko Mbinguni? Watu wote hakuna aliyewahi kumwona Mungu . Mungu hajawahi kudhihirisha sura yake waziwazi.

Kama unawasiwasi kwamba Mungu yupo au hayupo, nitende mema au nisitende mema, kwa ushauri wewe tenda mema. Hata kama huna uhakika wa kumkuta Mungu wewe tenda la kufaa. Ukitenda la kukujenga ni faida kwako na ukitenda la kukubomoa ni hasara kwako, si bora utende lililo jema, usimkute Mungu lakini usiwe na cha kupoteza. Lakini kama ukitenda uvu, harafu ukamkuta Mungu basi ni wazi utakuwa umepoteza hapa duniani na peponi pia.

Mungu kaweka kanuni ambazo zinawafanya wale ambao wanamtumainia wawe na uhakika na uwepo wake. Asili ya mbegu mwitu na matunda yake huwa mwitu na asili ya mbegu njema na matunda yake huwa matunda mema. Hii ni kanuni ya Mungu ambayo kaiweka hapa duniani na watu ndzo kanuni tunazoziishi.

Mungu asili yake ni nuru, yaani mwanga. Nyota tumaini lake kuwa kama mwezi, na mwezi tumaini lake kuwa kama jua na jua tumaini lake kwa Mungu. Hii ni kanuni ya nuru ambayo Mungu kaweka duniani.

Wajinga wenye matumaini tumaini lao kuwa wenye haima na wenye hekima tumaini lao ni Mungu. Mungu ndiye mwisho wa kila jambo. Ndiye tumaini la mbingu na nchi, maana yeye ndiye aliyefanya upacha huu.

Mungu alifanya nuru na giza.
Mungu alifanya usiku na mchana.
Mungu alifanya maji ya chini na juu.
Mungu alifanya mbingu na nchi.
Mungu alifanya mvua na ukame.
Mungu alifanya mwamme na mwanamke.
Mungu alifanya wanyama mwituni na wanyama wa kufugwa.
Mungu alifanya samaki na wanyama.
Mungu alifanya bahari na nchi kavu.
Mungu alifanya leo na kesho.
Mungu alifanya jua na mwezi.
Mungu alifanya  nyota na giza.
 Mungu alifanya hofu na furaha.
Mungu alifanya Adamu na Yesu.
Mungu amefanya watu na yeye.

Mungu yupo rafiki yangu, kazana kutenda linalofaa kutendwa na wewe utapokea tuzo lake. Mfanye yeye kuwa imani yako, ngao yako na tuzo lako. Mungu anatupenda sana.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

[TAFAKARI NENO YA LEO..8] Mambo Mawili Ambayo Huondoa Hofu Na Misukosuko Katika Maisha Yako.

 Sadick Kilasi     September 23, 2018     KUFURAHIA MAISHA     No comments   

Hofu na misukosuko katika maisha, ni mambo ambayo hayawezi kuacha kutembea na wewe katika maisha yako katika dunia hii. Hii ni dunia ambayo inaendeshwa kwa upacha usiofanana, kwa hiyo ilimradi tu upo duniani basi tambua kwamba una hali za giza na nuru.

Dunia ipo chini ya utawala wa nguvu hasi, nguvu hiyo ndiyo nguvu ambayo ndani yake kuna hofu, kiburi, ubinafsi na hali mbalimbali za mfadhaiko. Wakati dunia inaumbwa giza tayari lilikuwa linatawala, sasa nuru ilipoletwa giza iliifia nuru. Si kwamba giza liliondoka moja kwa moja, hapana, nuru ilipata nguvu kwenye giza.

Mwanzo 1:2-4, Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tene utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa virindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji. Mungu akasema, iwe nuru, ikawa nuru. Mungu akaiona nuru ya kuwa ni njema; Mungu akaitenga nuru na giza.

Giza lilikuwepo lakini Mungu alipambanua alipoirusu nuru, akabainisha kwamba, nuru ni njema. Baada ya hapo Mungu aliendelea na kazi yake huku, huku nuru ikawa ndiyo inayomwongoza. Nuru ilikuwepo kwa sababu giza lilikuwepo na sasa nuru ipo kwa sababu giza lipo.

Mpinzani mkubwa sana wa maisha ya furaha ni hofu. Na hofu asili yake ni giza na furaha asili yake ni nuru. Kuna mambo mawili ambayo ndiyo msingi wa maisha ya mtu ambayo hutupilia mbali hofu na mafadhaiko.

1.Kujifunza Neno la Mungu na tafakari mbalimbali.
Moja ya kitu ambacho nimejifunza kutoka kwa maisha ya Yesu ni hiki; Mafarisayo na Walimu wa sheria, walikuwa wapinzani wakubwa sana wa Yesu.Toka Yesu anaanza kazi yake walikuwa wanajaribu kumtega na kumkamata lakini ilikuwa inashindikana. Mafarisayo katika neno la Mungu, walitumika kama wapinzani, inamaana walikuwa ni watu wa giza. Walimjaribu Yesu ili awe adui yao lakini ilishindikana, Yesu alikuwa anawachukulia kwa jinsi walivyo na alikuwa anawatumia kuwafunza wengine. Ikiwa utafuata nuru na kuondoa mtazamo wa uadui si rahisi hofu kukuingi. Lakini pia, Yesu alipokuwa anawafundisha watu walikuwa wanashindwa kumnasa kwa sababu neno lake lilikuwa ni nuru na mitego yao ilikuwa inashindwa. Ikiwa utachukua neno la Mungu na kujifunza unakuwa unaingiza nuru ndani yako na giza lenyewe litahama.  WAEFESO 5:26, Ili makusudi alitakase na kusafisha kwa maji katika neno. Kwa kadili ambavyo unasoma neno la Mungu ndivyo dhamiri yako inatakasika. Na giza linaondoka ndani mwako.

2.Upendo.
Moja ya jambo kubwa kabisa ambalo hofu haiwezi kuingia kabisa basi ni upendo. Penye upendo wa kweli hata magonjwa hayawezi kuingia. Siku ambayo Yesu alitiwa mbavuni na maadui zake ni siku ambayo watu wote walimtenga. Wakati watu walipokuwa wanaunganika kwa pamoja kwa upendo Yesu hakukamatwa. Yesu aliwatibu watu magonjwa, watu waliokuwa wametengwa kama wenye ukoma lakini kwa sababu ya upendo alishinda hayo yote. Penye pendo hapana hofu.

Sababu hizi mbili ni msingi ya Neno la Mungu yaani amri kuu mbili; Mpende Bwaba Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote na kwa nguvu yako yote. Mpende jilani yako kama unavojipenda wewe mwenyewe.  Kwa hiyo ni vema tukajitahidi kukua katika kusoma neno la Mungu na kuishi kwa upendo na watu. Asante.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.


Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Saturday, September 22, 2018

Ukiona Unaliamini Jambo Na Huishi Hilo Jambo Basi Unakosa Uaminifu.

 Sadick Kilasi     September 22, 2018     NJOZI     No comments   

Imani bila matendo imekufa. Ukiona unaliamini jambo halafu huliishi hilo jambo basi unakosa uaminifu. Imani ni kuishi matumaini kwa imani.

Yakobo 2:14,26, Ndugu zangu yafaa nini, mtu akisema ya kwambaanayo imani, lakini hana matendo? Je! Ile imani yaweza kumwokoa? Maana kama vile mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo natendo imekufa.

Chochote kile ambacho unakiamini basi unapaswa kuishi wakati huu wa sasa. Tunaishi dunia yenye mambo mengi sana, matukio hutukia kila baada ya sekunde, kifo nacho kipo jilani sana kuliko uhai kwahiyo chochote unachokiamini ishi hicho unacho kiamini.

Usisubiri ukamirifu, ukamirifu haupo hapa duniani kwahiyo kazana kuishi kile ambacho unakiamini. Usingoje mpaka uwe na kitu fulani ama kianzio fulani, hapana, fanya kitu ambacho unakiamini huku ukizingatia msingi wa hapo ulipo. Kunali mazingira uliyopo kisha songa mbele.

Ukipiga hatua kutoka hapo ulipo, utasimlia watu kutoka hapo ulipo. Usijidanganye mwenyewe, chukua hatua. Kama unataka kusoma kitabu basi chukua hatua soma, kama unataka kumsamehe mtu basi chukua hatua samehe, chochote kile ambacho unataka kufanya fanya.

Hakuna imani bila matendo, kama unaliamini jambo harafu hulitendi wewe unalitambua tu, huliamini. Ishi unachokiamini.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Je! Unapanda, Au Unashuka Bondeni?

 Sadick Kilasi     September 22, 2018     KUFURAHIA MAISHA, TAFAKARI YA ROHO     No comments   

Je! Unapanda Au Unashuka Bondeni?


Katika maisha hakuna kubaki sehemu moja kama hupandi ama hushuki. Kwa sababu ya dunia jinsi ilivyo, dunia ambayo imetawaliwa na nguvu hasi kabisa. Kama huna unachokifanya ambacho kinakupeleka mbele basi tambua dunia inakushusha chini. Huwezi kubaki palepale.

Ikiwa utapanda mbegu mbovu basi mti na matunda yake yatakuwa matunda mwitu tu, kutokana na mbegu uliyopanda. Wapo watu ambao maisha yao haya furaha lakini wapo watu ambao maisha yao yana furaha. Wanaokosa furaha siku zote huendelea kukosa furaha kwani mbegu waliyochagua huendelea kuwapeleka bondeni. Wanao furahia maisha huendelea kufurahia maisha maana mbegu waliyoipanda hundelea kuzaa na kutoa mbegu njema.

Tujifunze kutoka kwenye neno la Mungu: Mwanzo 1:11-12, Mungu akasema, nchi na itoe majani, mche utoao mbegu, na mti wa matunda uzaao matunda kwa jinsi yake, ambao mbegu zake zimo ndani yake, juu ya nchi; ikawa hivyo. Nchi ikatoa majani, mche utoao mbegu kwa jinsi yake, na mti uzaao matunda, ambao mbegu zake zimo ndani yake, kwa jinsi yake. Mungu akaona ya kuwa ni vyema.


Mpendwa msomaji, nchi hii ukilima mazao, ukipanda mahindi ni lazima magugu yatamea yenyewe bila kupandwa. Unakazana kwenye nini? kitu gani unapalilia? kama unapalilia magugu basi magugu yatakua lakini kama unapalilia mahindi basi mahindi yatakua. Watu wengi huwa wanapoteza furaha kutokana na hatua zake za maisha na kile ambacho unakizingatia.

Unaweza ukapanda mbegu mbovu lakini kama umestuka unaweza kupanda mbegu njema na ukaizingatia mbegu njema. Wakati Mungu aliumba hi dunia aliumba wanyama wakufugwa na wasiofugwa, miti ya kufugwa na isiofungwa. Ukifuga mnyama asiye fungwa, jiandae kwa maumivu. Ukifuga mti usiofugwa, basi jiandae kwa matunda ya mwituni.


Lakini wapo watu ambao maisha yao wanatamani sana kujiondoa kwenye hali ya kuwa mwituni kwao limekuwa jambo ambalo haliwekani licha ya kuwa hawataki kusumbuliwa na hali hiyo. Nalizungumzia hilo kwa sababu nimekubwa na hali hiyo kwa muda mrefu, licha ya kwamba nilipanda mti mwema lakini bado ile hali iliendelea kunifuata kwa sababu ipo na mimi, kama maneno matakatifu yanavyosema;  Yeremia 3:1, Watu husema, mtu akimwacha mkewe, naye akienda zake, akawa mke wa mtu mwingine, je! mtu huyo atamrudia tena? Je! nchi hiyo haitatiwa unajisi? Lakini wewe umefanya ukahaba na wapenzi wengi; nawe, je!  utanirudia mimi? Asema Bwana.

Katika mazingira kama hayo wengi huteseka, wengi hujikuta wanafanya na wanaendelea kupalilia uovu hata kama hawataki. Mungu alipoiumba dunia aliikamirisha kila kitu lakini tatizo ni watu kuwana matumizi mabaya na vitu ambavyo Mungu amewaumbia na kuwapa wanadamu watawale. Mfano mdogo tu, ambao watu hutumia vibaya kile ambacho Mungu ameweka ndani yao, kama vile, dharau au kupuuzia. Dharau sio mbaya kwa mwenye matumizi mazuri lakini dharau ni mbaya sana pale ambapo unatumia kuwaumiza wengine. Lakini pia unaweza ukatumia dharau kuwasaidia wengine na kuepuka matatizo ambayo hayana maana. Luka 23:34, Yesu akasema, Baba, uwasamehe kwa maana hawalijui wanalolifanya. Huu ni mfano mzuri tu wa matumizi mazuri ambayo Mungu katuwekea vitu tutawale kwa bahati mbaya wengi humiliki.

Mpendwa msomaji; inawezekana mambo yako si mazuri katika maisha yako lakini kuna njia ya kutoaka. Haijarishi kuna kitu ambacho huwa kinakufinya na kukuumiza kiasi gani ndani mwako lakini yeyote yule ambaye yupo tayari kuchukua hatua Mungu ameweka uponyaji kwa kila mmoja. Watu wengi wanateseka kwa sababu wanataka wanavyotaka kwa sababu watu wanataka; lakini ngoja nikwambie hivi, chochote kile ambacho unakitaka utapata ikiwa tu utaanzia ndani yako na kukubali mazingra ya hapo ulipo kwamba nipo hapa sasa natubu kwa kufuata njia iliyo sahihi.

Kama umejikuta umeingia kwenye mtego basi kaa na utambue tu kwamba mtego sio mauaji bali ukinaswa kwenye mtego bado unamatumaini ya kuishi. Shukuru kwamba umepata makala ambayo itakusaidia na hali uliyonayo na kuanza kishi maisha ya matumini.

Mimi huhubiri injili ya maji na Roho lakini wakati nasoma kitabu cha ISHINDE TABIA YA KUGHAHIRISHA MAMBO, nilikutana na kanuni ya kupona kutoka kwenye hali hiyo na kanuni hiyo inaendana na ubatizo wa Yohana Mbatizaji, kanuni yenyewe ni;
Mfumo wa kutengeneza tabia yoyote mpya huwa unapitia hatua tatu, unatengeneza tabia yoyote ile ambayo unaitaka;
1.Kikumbushio.
2.Kitendo unachofanya.
Faida unayopata.
Huu ni utafiti wa kisayansi ambao unaweza kutumia kubadili tabia yoyote ile. Lakini nimekwambia kwamba utafiti huu unafanana kabisa na mahubiri ya Yohana Mbatizaji, formula ndiyo hiyo hiyo. Angalia, Mathayo 3:1-12, Siku zile Yohane Mbatizaji alitokea, akaanza kuhubiri katika jangwa la Yudea. Tubuni maana ufalme wa Mbinguni umekaribia. Huyu Yohane ndiye yule ambaye nabii Isaya alinena juu yake aliposema. Sauti ya mtu inaita jagwani: Mtayarisheni Bwana njia yake, nyosheni barabara zake ,Yohana alivaa vazi lililoshonwa manyoya ya ngamia, na ukanda wangozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni. Basi, watu kutoka Yerusalemu, kutoka pande zote za Yudea na sehemu zote za kandokando ya mto Yordani, walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani. Lakini alopoona Mafarisayo wengi na masadukayo wanamjia, ili aawabatize aliwaambia, Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea mikimbie ghadhabu inayokuja? Onesheni kwa vitendo kwamba mmetubu.Msifikiri na kujisemea Baba yetu ni Abrahanu  hakika, Mungu anaweza kuyafanya mawe haya kuwa wototo wa Abrahamu. Basi,shoka lipo tayari kwenye mizizi ya miti; hivyo kila mti usiozaamatunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni. Mimi nawabatizeni kwa maji kuonyesha mmetubu. Lakini anayekuja baada yangu ananguvu kuliko mimi, nami sistahili hata kubeba viatu vyake. Yeye atawabatizeni kwa Roho Mtakatifu na kwa moto. Yeye anashika mkononi mwake chombo cha kupuria nafaka, ili aipure nafaka yake; akusanye ngano yake ghalani, na makapi ayachome kwa moto usiozimika.


Yohana alikuja kuwageuza watu ambao walikuwa wamepotea, watu waliokuwa wanaabudu sanamu, watu wenye shida mbalimbali, watu wenye dhambi na hilo ndiyo kazi ya Yohana. Yohana alikuwa anawakumbusha kwamba uliko siko, tubu. Kutubu ni pale ambapo unakubali umekosea na unachukua hatua ya pili. Mpendwa msomaji, ili kuelewa hili kwa makini, kuna mambo matatu ambayo ni; imani, utayari na matumaini. Na siku zote hiyo ndiyo fomula ambayo kila mtu huwa anatumia kuishi. Rafiki yangu naomba uwe makini sana hapa; Labda nikufafanulie mstari wa kwanza na wa pili ili tuende kwa pamoja,...Siku zile Yohana Mbatizaji alitokea, akaanza kuhubiri katika jangwa la Yudea: Tubuni, maana Ufalme wa mbinguni umekaribia...[ hiki ni kikumbusho], kwa sababu watu walikuwa bize kufanya mambo yao ya hovyo, kufanya mambo yasiyofaa ambayo yapo nje ya uwepo wa Mungu sasa ilibidi Yohana awakumbushe hivyo. Sasa katika hiyo mbegu ndogo kabisa ya kikumbusho imebeba, mfumo wa imani, utayari na matumaini.

 Sasa kabla ya kuendelea mbele naomba nikuonyeshe mfumo wa Mbegu jinsi unavofanya kazi; MWANZO 1:11-12, Kisha Mungu akasema, nchi na ioteshe mimea. Mimea izaayo mbegu, na miti izaayo matunda yenye mbegu. Ikawa hivyo. Basi, nchi ikaotesha mimea izaayo mbegu kwa jinsi yake, na miti izaayo matunda yenye mbegu kwa jinsi yake. Mungu akaona ya kuwa ni vyema. Hizi ndizo hekima za Mungu, hakuna mtu anayetambua, mwanzo wa mambo yote ni yeye, asante, tuendelee.

Ukisoma mstari unaofuata utakuja kugundua kwamba, mbegu aliyokuwa anaihubiri Yohana, ilikuwa chanzo chake ni Mungu,  Mathayo 3:3, Huyu Yohane ndiye yule nabii Isaya alinena juu yake aliposema: Sauti ya mtu anaita jangwani: Mtayarisheni Bwana njia yake, nyosheni barabara zake. Kwa hiyo Mungu alitia neno ndani ya Yohana, mbegu aliyekuwa anaihubiri Yohana, mwanzo wake ni Mungu. Hareluya.

Sasa ukisoma kwa umakini kifungu kizima ambacho nimekuwekea hapo juu kinachohusu Yohana utakuja kugundua mfumo wake ndiyo huohuo. Sasa kwa kadili ambavyo anazidii kutoa ndivyo mambo yanazidi kuwa wazi wazi mpaka unakuwa msitu mnene.

Tutaendelea na makala na makala hii, kwa leo tuishie hapo. Lakini kitu kimoja ambacho rafiki yangu ningependa unisaidie kuwaalika watu ili tuwe pamoja katika makala hizi, alika kila mmoja kwa kumtumia makala hii. Hizi ni makala zenye uponyaji wa ndani kabisa kwahiyo hata wewe unapaswa kufuatilia mwendelezo huu ili uchimbe msingi kwa ndani zaidi. Makala hizi ni za uponyaji kiroho, kiakili na kimwili. Leo ndio tumeanza.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Friday, September 21, 2018

Huwezi Kuuona Umuhimu Wa Maji Mpaka Visima Vikauke.

 Sadick Kilasi     September 21, 2018     HEKIMA ZA WAZEE, NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI     No comments   

Mara nyingi huwa naamini kwamba, ukweli ambao anaoutoa mtu baada ya ushindi mara nyingi huwa sio ukweli halisi. Ukweli halisi ni ule ukweli ambao upo ndani ya ukweli. Huwezi kujitenga na ukweli harafu ukazungumzia ukweli.

Lakini pia huwa naamini kwamba sio kila jambo ni kweli wakati wote kuna wakati jambo hilo linawezakuwa kweli na kunawakati mwingine sio kweli. Sio kweli kwamba lazima kila mtu awe tajiri mkubwa lakini pia sio kweli kwamba si lazima mtu awe maskini. Ukweli wenyewe halisia ni pale mtu unapoishi ndani ya wakati kwa wakati sahihi.

 Ukitaka uone umuhimu wa maji basi kosa maji. Sio usahihi wa ukweli kwamba anayeiba ni mwizi bali anayemtangazia mwenziye mwizi basi yeye ndiye mwizi namba moja.

Si kila neno  ambalo unamtolea mtu kutoka kwenye kinywa chako huwa anasikiliza bali wakati mwingine mwingine maneno mengine unaweza kuongea yakarudi kwako kupitia sikio lako yakaumiza moyo wako. Kwa hiyo jiangalie na maneno yako.


Sio kweli kwamba unapaswa kuwa na ndoto wakati wote bali unapaswa kuishi ndoto kwani ndoto huwezi kuifikia na ukiifikia umekufa. Ishi sasa.

Ukweli ni kwamba, anayekwambia kitu na kukwambia uweke siri, usite kumwambia kwamba mizigo yake huwezi kujitwisha. Siri ni mzigo mzito sana ambao wakati wote unatamani kuutua. Wezi hutamani siri ya wanachokiiba, wanamafanikio hutamani siri ya Mafanikio na ndio maana sehemu za siri hutafutwa kwa uchu sana na watu japo ni sehemu za aibu.


Usitumie muda wako kumdanganya mtu kwa hiyo itakuwa ni siri yako.

Huwezi kuona umuhimu mpaka visima vikauke kwani huwezi kujua kudondoka mpaka uteleze.

Usimhukumu anayeiba wewe siumeweka siri na siri siku zote hufumbuliwa.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Kuijua Imani Na Kuishi Maisha Ya Ushindi.

 Sadick Kilasi     September 21, 2018     TAFAKARI YA ROHO     No comments   

KANUNI YA  IMANI.

Cha kwanza kabisa kila kitu ambacho kipo duniani huendeshwa kwa imani tu. Vitu vyote vyenye sura ya kueleweka huwa havieleweki. Sasa kwa sababu havieleweki basi lazima lugha yenye mipaka lazima itumike. Vitu vyote vyenye mwili huendeshwa kwa imani tu na sio ukweli halisi. Majina yao ni majina ya kukalili au majina ya kuzoea, wasomi wanaita mantiki. Na ndiomaana ni rahisi mtu kubadili jina lake lakini uhalisia wa sura yake haupotei, naweza kubadili jina langu la Sadick labda kwenda jina la Antoni na baadae jina hilo likazoeleka na watu wakawa wanalitumia vizuri kama jina la mwanzo lakini mwanzo nilikuwa naitwa Sadick na watu walikuwa wamelizoea jina hilo. Ili ukweli wa majina uwe ukweli lazima nitumie imani. Imani huwa inabadilika lakini ukweli huwa haubadiliki. Kwa kadili ambavyo unajua kitu ndivyo ambavyo utazidi kubadili imani yako. Imani yako inawezekana ikawa inaongezeka au inapungua kutokana na ukamili wa taarifa na jinsi ambavyo unachukulia hilo jambo. Ni muhimu sana kuelewa juu ya imani kwani vitu vyote nyenye mwili huendeshwa kwa imani tu kwani kila kitu chenye mwili hakieleweki kilikotoka. Dunia hujaza sehemu ambayo inautupu na ikisha kujaza mwanadamu atakipa jina kile kitu; mfano, mti, nyasi, watu na kila kitu chenye mwili. Imani ni maoni ya mtu juu ya jambo fulani.

Imani ni kuwa na hakika na mambo yajayo, hii ni maana ya kibiblia. Waebrania 11:1, Kuwa na imani ni kuwa na hakika na mambo tunayotumainia; kusadiki kabisa mambo tusiyoyaona. Ikiwa tupo duniani na tunaona kila kitu, je, tutakuwaje na imani? Na kwa sababu imani ni kuwa na hakika na mambo usiyoyajua basi ni wazi kwamba kila kilichopo duniani hakina ukweli ulio sahihi. Na tunaamini kwamba hii ndio dunia ya kueleweka, mambo yote hapa yapo waziwazi tofauti na rohoni ambako kwa imani inasemekana kwamba huko hakuna vitu vyenye mwili.
Waebrania 11:3, Kwa imani sisi tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, vitu vinavyoonekana kutoka vitu visivyoonekana. Kwa sasa tupo katika dunia ya vitu vinavyoonekana na tumaini letu ni kuona uso wa Mungu ambapo ndipo mwanzo wa dunia kuumbwa kwani dunia iliubwa kwa neno la Mungu. Kwa sasa tupo kwenye vitu vinavyoonekana tunarudi sasa kwenye vitu visivyoonekana. Lakini kwa kuwa bado tupo safarini katika dunia hii tunaweza kuwa na hakika kutoka vitu visivyoonekana kwenda kwenye vitu vinavyoonekana, hiyo nayo ni imani. Waebrania 11:11, Kwa imani hata Sara aliamini kwamba Mungu hutimiza ahadi zake, kwa hiyo akajaliwa kuchukua mimba ingawaje alikuwa amepita umri. Imani ni kupata haki ya jambo ambalo halipo. Na hivyo ndivyo dunia inakwenda kwa imani. Watu wote tunaishi kwa imani, kutoka kwenye kitu kisichoonekana kwenda kwenywe kitu kinachoonekana na kutoka kitu kinachoonekana kwenda kwenye kitu kisichoonekana. Haya yote ni matumaini ambayo tunayo. Imani ni kufanya jambo kuwa haki amblo halina hakika kuwa kweli. Kila jambo limefichwa, ukiona unacho basi tambua wakati wote kile kitu ambacho unacho kinaweza kuchukuliwa na ukiona huna basi tambua kwamba ukiwa na imani tu na kupata haki ya kile ambacho huna utapokea kutoka kwa Mungu. Katika dunia tunaishi ndani ya wakati, vitu vyote vyenye mwili kwa kadili wkati unavokwenda hupoteza ubora wake na mwisho hupotea kabisa lakini hivyohivyo tena sehemu ambayo ipo wazi ni lazima ijazwe kutoka kwenye vitu visivyoonekana kwenda kwenda kwenye vitu vinavyoonekana na hii ndio imani. Lazima utambue kwamba vitu vya mwili na vya rohoni haviwezi kukaa kwa pamoja, ni jambo ambalo haliwezekani ni lazima mwili utumainie rohoni na rohoni kutumainie mwilini. Sasa  kutokana na kutokuwepo kwa ukamirifu huo basi imani lazima itumike, na hapo ndipo ambapo mtu anajenga picha kichwani mwake ya jambo ambalo halipo katika uwepo wa macho.
UMUHIMU WA IMANI KATIKA MAISHA.

Ikiwa umetambua tayari kwamba maisha ya hapa duniani hayana ukamirifu basi ni wazi kabisa tayari umeuona umuhimu wa imani. Kama chenye mwili huingia duniani na kuanza kupoteza kila wakati, kutoka kwenywe kwenye kuwepo kwenda kwenye kutokuwepo basi ni wazi kwamba ni muhimu sana kujali wakati au muda. Ni muhimu sana kujali wakati, kwa sababu kila sekunde kwako ni gharama ya maisha yako inapungua. Ikiwa kila sekunde unamegwa na kuondolewa sehemu fulani ya uzima wako basi mwisho uzima utakuishia na wewe utabaki huna cha kuishi katika ulimwengu, mwili wote umeisha. Sasa kama wakati sio kipaumbele chako basi tambua kwamba utaenda kama ulivokuja bila kuacha alama yoyote hapa duniani.

 Kitu kingine cha muhimu katika imani ni kutambua mazingira na kujitambua mwenyewe. Unajua, unavojielewa kwamba wewe ni mwili na unamatumaini ya kurudi rohoni ni wazi kwamba tayari utaishi kwa matumaini ya kwenda rohoni. Hivi sasa watu wengi wanaishi maisha ya kutumainia kwenda rohoni. Kwa kuwa unatambua abisa kwamba utakwenda rohoni basi bi wazi kwamba lazima ubaki kwenye njia ya kwenda rohoni, njia ambayo itakurudisha ulikotoka na sio kwenda jehanamu ambako hujatoka huko, hana, ni lazima ubaki katika njia kuu.

Kitu kingine cha muhimu kwenye imani, ikiwa tayari umeelewa imani ni nini? Tayari unaweza kutambua kwamba, hapa, hapa, duniani kama ulikuwa umekosa kitu fulani ni wazi kwamba unaweza kumwomba  Mungu na akakupatia kile kitu ambacho huna na ukakipata kwa sababu chochote kile ambacho huna ukimwomba Mungu anakupa. Mwanzo  15:1-6, Baada ya mambo hayo neno la Mwenyezi Mungu lilimjia Abramu katika maono, Abramu! usiogope! Mimi ni ngao yako. Tuzo alko litakuwa kubwa! Lakini Abramu akasema, Ee Mwenyezi Mungu, utanipa nini hali naendelea kuishi bila mtoto, na urithi wangu ni Eliezeri wa Damasko? Tazama! Hujanijalia mtoto; mtumwa aliyezaliwa nyumabani mwangu ndiye atakaye kuwa mrithi wangu! Ndipo Mwenyezi Mungu akamwambia, Huyu hatakua mrithi wako! Mwanao halisi nndiye atakayekuwa mrithi wako. Hapo Mwenyezi Mungu akamleta Abramu nje na kumwambia, Tazama mbinguni, zihesabu nyota, kama kweli utaweza  kuzihesabu! Hivyo ndivyo wazawa wako watakavokuwa wengi! Abramu akamwamini Mwenyezi Mungu, naye mwenyezi Mungu akamkubali Abramu kuwa mwadilifu.
Mungu alimkubali Abramu kwa imani na alimkubali Abramu kuwa mwadilifu kwa imani tu kabla ya matukio kutukia na Abramu alimwamini Mungu kwa imani tu kwani Abramu alikuwa bado hana uzao wa kumrithi na wala Mungu alikuwa hajamtimizia ahadi. Unapo amini, unapokea haki na ukisha kupokea ndipo matokeo nje huonekana. Leo hii hata sisi Abramu ni Baba yetu wa imani kwani yeye ndiye mwanzo waimani. Waisraeli pekee ndiyo waliokuwa taifa teule la Mungu lakini hata sisi tunashiriki kuwa watoto wa Mungu kwa imani. Maisha ya Abramu yalikuwa hayana tumaini lakini kwa imani akapata tumaini jipya ambalo Mungu alimuahidi.

Lakini faida nyingine ndiyo hii, ni njia nzuri zaidi ya kuondoa uchungu moyoni mwako ikiwa unamatatizo fulani. Ni rahisi kumsamehe mtu moyoni mwako kuliko kumkabili nje. Ikiwa utaanza kuwasamehe watu na kujisamehe mwenyewe basi tayari unakuwa unaukomavu wa ndani. Ni rahisi kuomba maombi mengi rohoni mwako, laakini pia ni rahisi kutimiza jambo ambolo linaanzia ndani na kutoka nje. Ikiwa unataka kutimiza mapenzi yako kwa matokeo ya nje basi ni wazi kwamba ndani mwako uwe unahamu zaidi ya mara mbili ya matokeo ya nje, ili utimize vizuri. Mathayo 5:20, Ndiomaana nawambieni, wema usipozidi ule wa walimu wa sheria na wa mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni. Ikiwa unataka kufanya jambo lolote basi inatakiwa uwe na hamu kubwa ndani yako harafu nje utatimiza kwa ubora zaidi kwa kadili ya imani yako. Mafarisayo na walimu wa sheria ni walikuwa watu ambao hutimiza mambo yao kwa kinafki kwa sababu walikuwa hawana imani ndani yao, sasa Yesu alimbia watu msipozidi kuwa na hamu kubwa zaidi ya walimu wa sheria na mafarisayo hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni. Ni lazima uwe na hamu kubwa ndani mwako ya kutaka kuwa bora, ni lazima ndani mwako uwe na hamu kubwa ya kutaka kuishi na watu vizuri na watu, ni lazima ndani mwako uwe na utayari wa kutaka kujijenga zaidi hata kama watu nje wanakuonyesha na kukukatisha tamaa.

Hii ni sheria, kwamba lazima uwe na imani ndani mwako na ndipo utimize mapenzi yako. Ikiwa unajengeka ndani mwako kwa imani kwa mtu ambaye hawezi kuona basi ni rahisi kujengeka kwa nje ambako watu huona. Kama ukiwa tayari kujielewa wewe mwenyewe basi ni rahisi kuwaelewa wengine. Kama ukiwa tayari kujihimili wewe mwenyewe basi ni rahisi kuwahili wengine. Ukitimiza haya basi huo ni utajiri. Lao Tsu.  Ni ukweli mtu, ukiweza kujijenga wewe mwenyewe binafsi basi rahisi kuwajenga wengine na ukiweza kujielewa wewe mwenyewe binafsi basi rahisi kuwaelewa wengine. Kama umejielewa kunamaeneo upo vizuri katika utendaji na kunamaeneo haupo vizuri katika utendaji basi katika maisha yako utaelewa kwamba kila mtu anaudhaifu maeneo fulani na kwenye maeneo fulani yupo bora. Wakati fulani huwa nafanya maamuzi haya bila kutegemea basi utaelewa kabisa hata mwenzangu hivo hivo, kwahiyo na imani hiyo inakuwa ni rahisi kutekeleza msamaha.

Ikiwa Ibramu alipata haki kwa imani basi Ibrahimu aliamini kwamba Mungu hawezi kushindwa kufanya lolote lile analolitaka. Imani inahitaji utambuzi ili kupata haki ya kutenda lile jambo unalotaka kutenda. Kama unataka kutimiza jambo ukiwa unafahamu mamlaka yako nni rahisi kutimiza jambo kwa imani. Kwa imani sisi tunavikubali vitu alivyoviumba Mungu, Kwa imani sisi tunakubali kwamba Mungu alimtoa mwanae Yesu Kristo ili achukue dhambi ya ulimwengu pale alipobatizwa na Yohana katika mto Yordani walifanya tendo la kikuhani na sisi kwa sasa hatuna dhambi. Kwa imani tunaamini Yesu aliteswa msalabani kwa sababu ya dhambi zetu na damu ya agano ikamwagika na sisi tukafanyika, kwa imani tunaamini kwambaYesu alikufa baada ya mateso na kufufuka kutoka kwa wafu na sasa yupo hai juu mbinguni. Kwa imani tunaamini kwamba ametubatiza kwa roho mtakatifu na sasa tunafurahia maisha. Imani hii inatupa haki sisi ya kufanyika wana wa Mungu. Kwa imani sasa  tunatekeleza upendo wa Mungu kwa sababu tayari hata sisi tumefanyika pendo kwa kuitwa wana wa Mungu na kujazwa Roho ya Mungu.
Imani inakupa wewe haki ya kutaka unachotaka ili mladi tu unijijenga mwenyewe au la unawajenga wengine. Imani hiyo inakufanya uchukue hatu ya kile ambacho unakiamini. Kwa hiyo rafiki yangu kazana kujijenga ndani mwako na kwa kadili ambavyo unajua zaidi ndivyo unapata haki ya kutaka kile kitu, utambuzi wa ndani ni muhimu zaidi.

Na cha mwisho ambacho ni muhimu  ni hiki, kila kitu mwanzo wake ni Mungu, na ndiomaana kila wazo huja kwako bila wewe kutambua na kinachofuata ni utayari wa kupokea kile ulichopokea kwa Mungu huku ukimtumainia yeye. Kwa hiyo imani ni kuishi tumaini wakati wa hivi sasa. Katika ndani ya maisha hayo kuna, imani, utayari na matumaini. Hivi vyote hufanya kazi kwa pamoja.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.

Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Thursday, September 20, 2018

Ukiona Fursa Hazigongi Mlango Jenga Mlango.

 Sadick Kilasi     September 20, 2018     NJOZI     No comments   

Ukiona fursa hazigongi mlangoni kwako, ujue pengine huna mlango, jenga mlango. Milton Berie.

Kuna kanuni moja ambayo siku zote huwa nasema kwamba, unaweza kuwa tayari, kuona mabaya, unaweza kuwa tayari kuona mema na mabaya lakini pia unaweza kuwa tayari kuona mema tu. Kulingana na Milton ni kwamba, unachochagua kuona ndicho utakacho kuona.

Kama wewe ni mmoja kati ya watu ambao whawaoni utaonaje? Usipokuwa tayari kuona huwezi kuona, lakini wakati ambao utakuwa tayari utaona na tena utaona mengi sana.

Wakati Yesu hajaja ulimwenguni alimtuma kwanza Yohana ili awafanye watu kugeuza macho yake ili waone na hii ndio inamaana ya sauti ya mtu atokaye nyikani inaiita, Mtayarisheni Bwana nji yake, nyosheni barabara zake. Yohana alikuwa anawaamusha watu watuwaliiolala ama alikuwa anajenga mlango ili Yesu aweze kugonga mlango. Hii tutaizungumzia siku nyingine ya Yohana kwa upana zaidi.

Sasa ukiona fursa hazigongi mlangoni kwako ujue haujakaa mlango wa fursa, kwanini? Kitendo cha kukataa kwamba fursa hazipatikani inamaana umeziba mlango wa fursa kwa kukataa kwako wewe mwenyewe. Chochote kile ambacho unakitaka utakipata endapo unataka. Ukisema fursa hazipatikani inamaana wewe ni mpinzani wa fursa, unaipinga fursa inayokuja.

Wakati mmoja Mungu alinifundisha hivi; Sadick, wewe unaomba maombi ya kuniomba mambo unayotaka lakini ninachokupa hupokei. Nikaelewa kwamba sina shukrani kwa mambo ambayo tayari Mungu amenipa. Unajua watu wengi hatupati tunachotaka kwa sababu hatukubali maeneo ambayo tupo, kwamba ule ndio mwanzo ambao tunapaswa kuanzia hapo. Kwa hiyo ukitaka kujenga mlango wa fursa kwanza anzia pale ulipo na kisha kubali mazingira ambayo upo ili uendeleze mazingira ambayo upo.

Ikiwa utaona jema kwenye kila jambo, basi, unaweza ukaendeleza kwenye chochote kile ambacho Mungu amekupa. Kila mtu hunza maisha ya umaskini hiyo ndio asili ya dunia. Hata kama utazaliwa katika nyumba tajiri kiasi gani bado wewe ni maskini tu. Utapambwa kwa nje na nguo nzuri lakini wewe ni maskini tu kwani ndani yako hicho kitu hakimo, hujajengeka kwa ndani. Yeyote yule huzaliwa bila nguo, awe amezaliwa na tajiri ama amezaliwa na maskini.

Watu wote tunazaliwa katika hali ya umaskini na kuuendea utajiri, japo hapa duniani huwa hatuufikii ukamirifu wa utajiri kwani dunia haina ukamirifu. Kwa hiyo ukiona fursa hazigongi kubali pale ulipo na endelea mbele. Usiuchukie umaskini kwani umaskini ni mwanzo wako wa kuuendea utajiri. Usiwe mtu wa kutaka fanya.

Ona wema kwenye kila jambo. Tumezaliwa kuendeleza.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 068700768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg
Newer Posts Older Posts Home

Search This Blog

Translate

Total Pageviews

About Me

Sadick Kilasi
View my complete profile

Followers

Kurasa

  • Nyumbani
  • Saidia Huduma Hii Kuwafikia Wengi Zaidi.

Search This Blog

Blog Archive

  • ►  2020 (5)
    • ►  January (5)
  • ►  2019 (46)
    • ►  December (4)
    • ►  October (1)
    • ►  July (8)
    • ►  June (1)
    • ►  May (2)
    • ►  March (14)
    • ►  February (11)
    • ►  January (5)
  • ▼  2018 (275)
    • ►  December (17)
    • ►  November (25)
    • ►  October (29)
    • ▼  September (43)
      • Toa Ulichonacho, Anzia Hapo Ulipo.
      • Panda Mti Leo.
      • [TAFAKARI NENO YA LEO..13] Hatupokei Haki Ya Mungu...
      • Saidia Huduma Hii Kuwafikia Wengi Zaidi.
      • Usijikinai Ndugu, Utaoza.
      • [TAFAKARI NENO YA LEO..12] Injili Ya Maji Na ROHO....
      • Utukufu Ni Wa Mungu.
      • [TAFAKARI NENO YA LEO..11] Je! Ufanye Nini Wakati ...
      • Watu Hawatakosa La Kusema, Endelea Kufanya Unachop...
      • [TAFAKARI NENO YA LEO...10] Hamna Namna, Mshangaze...
      • Endelea Kufanya Yanayofaa.
      • [TAFAKARI NENO YA LEO...9] Ukimpokea Yesu Onyesha...
      • Hii ndio Njaa Kubwa Ya Dunia Ya Sasa.
      • Tumia Makombo Ya Wakati Wako Kujisomea Neno La Mungu.
      • Naomba Uniambie Rafiki Yangu, Unaishije Na Watu Wa...
      • Una Shina La Kukupeleka Katika Ushindi.
      • Je! Mungu Atakuwepo Au Hatakuwepo?
      • [TAFAKARI NENO YA LEO..8] Mambo Mawili Ambayo Huon...
      • Ukiona Unaliamini Jambo Na Huishi Hilo Jambo Basi ...
      • Je! Unapanda, Au Unashuka Bondeni?
      • Huwezi Kuuona Umuhimu Wa Maji Mpaka Visima Vikauke.
      • Kuijua Imani Na Kuishi Maisha Ya Ushindi.
      • Ukiona Fursa Hazigongi Mlango Jenga Mlango.
      • Jenga Tabia Hii Nayo Tabia Itakujenga Katika Mahus...
      • Gharama Ya KupataVitu Vizuri Vinavyokupeleka Katik...
      • [TAFAKALI NENO YA LEO...7] Ondoleo La Hofu Na Mais...
      • [TAFAKARI HEKIMA ZA WAZEE], Kuwaelewa Wengine, Kuj...
      • Alituchagua Tangu Tukiwa Na Dhambi. [Kwa Imani Tun...
      • Kanuni Ya Kibiblia Ambayo Inaweza Kukusaidia Kupan...
      • Utabiri Wa Nabii Danieli Juu Ya Injili Ya Maji Na ...
      • [TAFAKARI NENO YA LEO...6] Tumeandaliwa Mazingira ...
      • Umezaliwa Wa Kipekee Sana Lakini Watu Ndio Kioo Ch...
      • (TAFAKARI NENO YA LEO...5) Kama Una Tumaini Basi T...
      • Hakuna Mtu ambaye Hana Kabisa Katika Maisha.
      • [TAFAKARI NENO YA LEO..4] Mtumainie Mungu Usikate ...
      • Hii Ni Bahati Yako Au Ni Wakati Sahihi Kwako?
      • [TAFAKARI NENO YA LEO 3] Usiende Kwa Mganga Siku Y...
      • Tunapokea Na Kutoa Kutokana Na Utayari Tulionao....2
      • [TAFAKARI NENO YA LEO...2] Je! Unataka Kuwa Na Fur...
      • Geuza Machungu Yako Kuwa Ushindi.
      • [TAFAKARI NENO YA LEO ...1] Jinsi Chuki Zinavyoene...
      • Tafakari Neno Ya Siku.
      • Tunapokea Na Kutoa Kwa Utayari Tulionao.
    • ►  August (7)
    • ►  July (12)
    • ►  June (17)
    • ►  May (19)
    • ►  April (31)
    • ►  March (33)
    • ►  February (25)
    • ►  January (17)
  • ►  2017 (58)
    • ►  December (16)
    • ►  November (22)
    • ►  October (2)
    • ►  September (11)
    • ►  August (4)
    • ►  July (3)
Sadick Kilasi. Powered by Blogger.

Jisajili kwa kujiunga nasi hapa

Posts
Atom
Posts
All Comments
Atom
All Comments
Maisha yenye maana ni yale maisha ambayo mhusika atambua nini kusudi lake la kuwepo hapa duniani. Hapandipo muhusika anapo kaa katika nafasi yake na kuwasha nuru katika sehemu aliopo kutokana uhusika wake. Jiunge na mtandao huu kupata maarifa zaidi na kwa ushirikiano mwingine kwa ujumla.

Kurasa

  • Nyumbani
  • TAFAKARI ROHO
  • Saidia Huduma Hii Kuwafikia Wengi Zaidi.

JIUNGE NASI SASA KWA KUJAZA FOMU HAPO CHINI


ANZA KUFURAHIA MAISHA NDANI YA YESU, MPOKEE ROHO MTAKATIFU KWA INJILI YA MAJI NA DAMU 0687000768

Zilizosomwa sana

  • Chukua hizi hapa nukuu za Malcolm x mtu ambaye anawavutia wengi sana.
    Ni siku nyingine tena ambayo ni mpya kabisa, karibu tena katika blogu hii ya JIKO LA USHAURI ambapo mimi mpendwa wako nimekuwa naingia jikon...
  • Ubatizo Wa Maji Mengi Na Ubatizo Wa Maji Machache, Upi Ni Sahihi?
    Ubatizo wa Maji Mengi Na Maji Machache. Kumekuwa na migongano kwa muda mrefu sana juu ya ubatizo, kati ya ubatizo wa maji mengi na ule uba...
  • Falsafa Za Maisha, Yaani Neno La Maarifa.
    Falsafa Za Maisha, Yaani Neno La Maarifa. Habari mpendwa? Natumai wewe unayesoma hapa umzima.   Karibu tena katika Falsafa Za Maisha. Ku...

Blog Archive

  • July 2017 (3)
  • August 2017 (4)
  • September 2017 (11)
  • October 2017 (2)
  • November 2017 (22)
  • December 2017 (16)
  • January 2018 (17)
  • February 2018 (25)
  • March 2018 (33)
  • April 2018 (31)
  • May 2018 (19)
  • June 2018 (17)
  • July 2018 (12)
  • August 2018 (7)
  • September 2018 (43)
  • October 2018 (29)
  • November 2018 (25)
  • December 2018 (17)
  • January 2019 (5)
  • February 2019 (11)
  • March 2019 (14)
  • May 2019 (2)
  • June 2019 (1)
  • July 2019 (8)
  • October 2019 (1)
  • December 2019 (4)
  • January 2020 (5)

JIKO LA USHAURI

Itambue Injili Ya Maji Na Roho. Ushiriki Ufalme wa Mungu, pata kitabu cha bure. Wasiliana nasi kwa sadikila65@gmail.com.

Tags

  • BIASHARA
  • HEKIMA ZA WAZEE
  • KUFURAHIA MAISHA
  • KUPATA BLOGU
  • MAHUSIANO
  • MAWASILIANO
  • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI
  • NJOZI
  • PATA BLOGU
  • SAIDIA HUDUMA HII
  • TAFAKARI NENO YA SIKU
  • TAFAKARI YA ROHO
  • UJASIRIAMALI
  • USHAURI
  • USWAZI TRICK

Kurasa

Labels

  • HEKIMA ZA WAZEE (24)
  • KUFURAHIA MAISHA (76)
  • KUPATA BLOGU (2)
  • MAHUSIANO (81)
  • MAWASILIANO (1)
  • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI (8)
  • NJOZI (94)
  • PATA BLOGU (3)
  • TAFAKARI YA ROHO (57)
  • UJASIRIAMALI (31)
  • USHAURI (78)
  • USWAZI TRICK (9)

Loading...

Fomu ya Anwani

Name

Email *

Message *

  • Napenda kusoma Biblia

About Me

Sadick Kilasi
View my complete profile
INJILI YA MAJI NA DAMU.

Search This Blog

Chapisho Lililoangaziwa

Alipambania Tumaini Lake Na Ndoto Yake Ikawa Kweli.

Kila mtu katika maisha ana tumaini lake. Msingi mkuu wa maisha ni tumaini. Nguvu kubwa ya maisha ni imani na mapito makuu ya maisha ni u...

Posts
Atom
Posts
All Comments
Atom
All Comments
INJILI YA KWELI NI INJILI YA MAJI NA ROHO. (MAJI, DAMU NA ROHO).
HII NDIYO KWELI YENYEWE.
YOHANA 19:34-35.

Copyright © JIKO LA USHAURI | Powered by Blogger
Design by Hardeep Asrani | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com | Distributed By Gooyaabi Templates