JIKO LA USHAURI

Itambue Injili Ya Maji Na Roho. Ushiriki Ufalme wa Mungu, pata kitabu cha bure. Wasiliana nasi kwa sadikila65@gmail.com.

  • NYUMBANI
  • KUFURAHIA MAISHA
    • ushauri
    • KUHUSU SISI
    • MAISHA NDANI YA YESU
  • MAWASILIANO
    • NAMBA YA SIMU
      • Sub 0687000768
      • Sub Child Category 2
      • facebook
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • NJOZI
  • SAIDIA HUDUMA HII
    • Childcare
    • Doctors
  • NYUMBANI
  • KUFURAHIA MAISHA
    • Stock
  • TAFAKARI YA ROHO
    • HEKIMA ZA WAZEE
    • Games
    • AFYA
      • Office
  • MAHUSIANO
    • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI
      • Sub Child Category 1
      • Sub Child Category 2
      • Sub Child Category 3
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • USHAURI
  • TAFAKARI NENO YA SIKU
    • Childcare
    • Doctors
  • PATA BLOGU

Monday, October 22, 2018

Ubatizo Ni Nini?

 Sadick Kilasi     October 22, 2018     KUFURAHIA MAISHA     No comments   

1.Ubatizo ni nini?
2.Asili yake ni nini?
3.Kwanini tubatizwe?
4.Hutusaidia nini?
5.Je! Ni ubatizo upi unaofaa?
6.Maji Na Roho vinahusianaje katika ubatizo?
Amani.

Habari za wakati huu Ndugu yangu? Natumai unaendelea vizuri kabisa. Hayo hapo juu ni maswali ambayo yameulizwa na Ndugu yetu Amani, kwahiyo nikwenda kuyajibu kwa kadili Mungu atakavyo nijalia.

Kwanza kabisa nakushukuru Amani kwa kuuliza maswali haya maana kwa kuuliza kwako wengi wanapata kuelewa. Na ni jambo zuri kwa mtu kuuliza jambo ambalo anaona hailewi nini maana ya kile ambacho kinaelezwa kila wakati. Ni maswali mzuri sana na ni ya muhimu kujua.

1.Ubatizo ni nini?
Ubatizo maana yake, kuzamisha. Kidini ni tendo la kumtia mtu maji baada ya kumwamini Yesu Kristo. Lakini maana halisi na ya kawaida ni kuzama katika jambo fulani. Unapokuwa umejivisha kwenye jambo fulani, hapo tunasema umebatizwa au umejibatiza. Unaweza kusama, kwa sasa mimi sitaitwa Sadick bali nitaitwa Antoni, hapo unakuwa umejibatiza jina jipya. Umeacha jina la kwanza na kuzamia jina la pili. Sasa kupatiza, hakupo katika jina pekee yaweza ikawa matendo fulani, yaani unaacha matendo fulani na kuingia matendo mengine. Kama umechukua hatua mwenyewe, tutasema umejibatiza na kama ni mtu kakushawishi, tunasema umebatizwa. Hii ndio maana ya ubatizo, kwa ujumla ni kutoka sehemu fulani na kuingia sehemu ngingine na kuzama kabisa. Tutazidi kuelewa kwa kadili ambavyo ninajibu maswali huko mbele.
Mathayo 3:11, Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwaajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.

2. Asili yake ni nini?
Dunia imekuwa inabadilika tangu kuumbwa.  Na mabadiliko ambayo yanatokea ni kutokana na mwanadamu aliyeumbwa kwa mfano wa Mungu kufanya mambo kinyume na Mungu. Mungu alianza kuiumba nchi kutoka katika maji, lakini dunia haikuwa sawa, ilikuwa utupu na ukiwa. Mungu akaifanya dunia kuwa sawa. Akamweka mwanadamu aitawale nchi na vyote vilivyomo ndani yake. Lakini badae Mungu baadae Mungu alimwona mwanadamu amepotoka akaangamiza dunia kwa maji hayo hayo ambayo ni mwanzo wa dunia kuummbwa, wakati wa Nuhu. Alipokuwa anaingamiza dunia hakuwa na lengo la kuifuta kabisa dunia bali lengo ni kufuta kizazi kiovu na kuingiza kizazi kipya ambacho si kiovu. Habari hizi ni kutoka kitabu cha Mwanzo 6 na kuendelea.

Lakini ile asili ya uovu bado ilikuwemo ndani ya mwanadamu, licha ya kizazi kimpya. Mungu hakuazimia kuharibu dunia kwa maji tena. Mpango mpya wa Mungu ni kuiharibu dunia kwa moto na mfano wake tayari umeshakuwepo ni Sodoma na Gomora. Lakini lazima uelewe kwamba, kila kitu ambacho kinatokea Mungu tayari alisha maliza kazi yake siku ya sita, kila kitu kipo tayari. Katika Agano la Kale watu waliishi wakiwa bado wana dhambi licha ya kwamba Mungu alifanya kizazi kipya cha Nuhu. Mungu akaazimia kwamba, kwa sababu hii, itaiharibu dunia kwa moto na mfano wake tayari umeonekana wa Sodoma na Gomora. Sisi wenyewe tunatazamia uharibifu utakao kuja kwa moto. Lakini pia Mungu ametumia maji kujenga dunia lakini pia ametumia moto huo huo kujenga dunia. Wale wote ambao wametazamia kufanya mambo mazuri wakiwa chini ya ubatizo wa maji, licha ya kwamba si wakamirifu lakini wanatazamia kufanya mambo mema, Mungu amefanya agano lililo bora zaidi ambalo ni ubatizo wa moto. Hii ndio Asili ya ubatizo.
1Petro 3:21, Mfano wa mambo hayo ni ubatizo, unaowaokoa ninyi pia siku hizi, [siyo kuweka mbali uchafu wa mwili, bali jibu la dhamiri safi mbele za Mungu], kwa kufufuka kwake Yesu Kristo.

3. Kwanini tubatizwe?
Mwanadamu alizaliwa katika uzao wa kizazi cha dhambi baada ya Adamu na Hawa kutenda dhambi, sasa ile asili bado inatembea nasi. Hakuna ambaye anaweza kukataa kwamba hana dhambi, asili ya ndani. Mungu alimruhu shetani amgonge kisigino mzawa wa Hawa na yeyote mwenye mwili amezaliwa katika uzao wa hawa. Ni mtu mmoja pekee ambaye hakuzaliwa na mwanadamu, Adamu, lakini pia Hawa alitoka katika mifupa ya Adamu. Kwa sababu kila mwenye mwili amezaliwa na Hawa ni lazima awe na asili ya Hawa. Hawa alipotii maneno ya shetani ilibidi awe chini ya utawala wa shetani. Lakini Mungu aliandaa mpango wa kumkomboa mwanadamu, akamwambia shetani, uzao wa mwanamke huyu atakuponda kichwa, na Huyu ndiye Yesu Kristo. Sasa ubatizo ambao  tunabatizwa ni ubatizo ambao unatutoa kutoka utawala mwingine kwenda utawala mwingine. Kama hujabatizwa inamaana utabaki katika utawala ule ule wa mwanzo. Hata kama hutendi dhambi, bado unaasili ile ya dhambi ambayo ipo ndani yako. Moyo wa mtu umejaa uovu, hakuna hata mmoja ambaye hajatenda dhambi. Ndani ya moyo hutoka, wivu, kiburi, kuabudu sanamu, uaji, kuzini, hakuna mtu ambaye hajatenda dhambi. Kuna aina kumi na mbili ambazo zipo ndani ya moyo wa mtu na ndio maana waweza kujikuta unafanya jambo ambalo hata wewe mwenyewe hukutazamia kufanya, hiyo ni asili, hutakuwa na uwezo wa kujimiriki mwenyewe, asili ndiyo itakayo kumiriki, Paulo alilalamika kwamba lile ninalo azimia ndani yangu kulifanya silifanyi, nafanya lile nisilo lipenda. Na ndiomaana unaweza kujikuta una hasira na jambo fulani harafu baadae unakuja kujutia. Kikubwa ambacho shetani anataka kutoka kwako ni wewe ukose furaha.
Mwanzo 3:15, nami naweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa na wewe utamponda kisigino.

Unapobatizwa inaondolewa ile asili ya kwanza na kuwekwa asili mpya.

4.Husaidia nini?
Kwanza kabisa lazima utambue kila mmoja anamatumaini. Licha ya matumaini madogo madogo ambayo unatarajia kufanya lipo tumaini la mwisho kabisa ambalo hili unalitumania maada ya kifo chako. Tumaini kuu. Sasa ikiwa huna matarajio yoyote inamaana upo chini ya uzao wa nyoka yaani utawala wa shetani. Na tumaini hili ambalo lipo chini ya shetani ni kuchomwa moto. Ubatizo unakuondoa katika hali hiyo, la kutoka katika tumaini la kuelekea kifo na kuelekea uhai. Ubatizo unaondoa dhambi ndani yako, kama nilivosema hapo juu, unapobatizwa unaondolewa kutoka asili ya kwanza na kuingia asili mpya. Asili mpya ni pale unapotumainia kuvishwa mwili mpya baada ya kubatizwa kwa Roho Mtakatifu ambao ndio kwa moto.

Unapokuwa duniani ni lazima uishi ufalme wa mbinguni hapa dunia, kwa sababu ufalme wa Mungu upo ndani yako na kwa sababu unatumaini la kuingia katika ufalme wa mbinguni ni lazima ukae katika njia inayoelekea katika ufalme huu. Mbinguni kuna fuaraha na haki basi kwa sababu wewe tumaini lako ni huko ni lazima ufurahie maisha hapa duniani. Lakini pia kwa wale ambao wapo chini ya utawala wa ibilisi, watakosa furaha, furaha yao ni burudani, kutegemea vitu ili kupata furaha, bila kitu fulani hawezi kuwa na furaha, tuaimaini lao ni kilio kwa sababu analia kwanza hapa hapa duniani. Ikiwa mtu unataka kupokea jambo fulani ni lazima ukae katika mkao wa jambo hilo, ni ngumu kuingiza chakula mdomoni wakati umefunga mdomo.
1Timotheo 8:5, Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chepeo yetu ni tumaini la wokovu.

5.Je! ni ubatizo upi unaofaa?
Ubatizo unaofaa na usiofaa kwa kweli ubatizo ni mmoja tu, wa kumwamini Yesu. Hakuna ubatizo wa aina mbili. Kama nilivosema hapo mwanzo ubatizo ni kujizamisha katika jambo fulani. Sasa injli ya maji na Roho ndiyo ubatizo wenyewe yaani ni kama mlango wa kujizamisha kwenye tumaini jipya. Mara nyingi watu tumekuwa tunatazama kwa matendo ya nje lakini hivyo, unaweza kwenda kubatizwa kwenye maji mengi lakini ukaendelea kufanya mambo yasiyo faa, lakini pia unaweza kwenda kubatizwa katika maji machache harafu ukaendelea kufanya mambo yasiyofaa. Unapokuwa unaamini injli ya kweli hilo ndilo jambo linalofaa. Unapaswa kuamini na kutenda kile kinachofaa kutendwa.

Hakuna ubatizo wa aina mbili ni aina moja tu, ni kuamini ubatizo ambao Yesu alibatizwa. Unapoamini ndipo aunapokea haki. Hii haitegemei wewe kubatizwa, inategemea imani yako, pale ambapo unaamini unashiriki kile ambacho Yesu alifanya. Kwa imani, na ili kuonyesha kwamba kweli umeamini basi yakupasa ufanye mapenzi ya Mungu. Lakini si kumwamini Yesu peke yake, hapana bali lazima utambue na umani namna Yesu alivokuja. Kwa hiyo hakuna namna ni kuamini injili ya kweli iliyo moja tu na kupokea haki ya Mungu.Sijasema kubatizwa bali kuamini.
1Yohana 5:9, Mwenye kuushinda ulimwengu ni nani, ipokuwa ni yeye aaminiye kwamba Yesu ni Mwana wa Munu? Huyu ndiye aliyekuja kwa maji na damu, Yesu Kristo; si katika maji tu, bali katika maji na katika damu. Naye Roho ndiye ashuhudiaye kwa sababu Roho ndiye kweli. Kwa mana wapo watatu washuhudiao [mbinguni,, Baba, na Neno, na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni umoja. Kisha wapo watatu washuhudiano duniani], Roho, na maji, na damu; na watatu hawa hupatana kwa habari moja. Tukipokea ushuhuda wa wanadamu, ushuhuda wa Mungu ni mkuu zadi; kwa maana ushuda wa Mungu ndio huu amemshuhudia Mwanaye.

6.Maji na Roho vinahusianaje katika ubatizo?
Ni swali zuri sana Ndugu hili, tena sana. injili ya maji na Roho ni injili ambayo Yesu mwenyewe aliihubiri. Alimwambia Nikodema kwamba, mtu hawezi kuzaliwa upya pasipo injili yamaji na Roho. Tunaweza kusema Yesu mwenyewe aliipa jina injili hii.

Uhusiono kati ya ubatizo na injili ya maji na Roho ni ubatizo wake Yesu aliobatizwa. Inamaana hakuna ubatizo pasipo injili ya maji na Roho, na neno ubatizo linasimama kwenye eneo la ubatizo ambao Yesu alibatizwa na ubatizo ambao Yesu anawabatiza watu kwa Roho Mtakatifu.

Mwanzo wa injili ni Yohana Mbatizaji, Yohana  alitokea jangwani akihubiri ili watu watubu. Yohana alikuwa anawandaa watu kukaa katika njia ya ubatizo ambao Yesu baadae alikungekuja kuwabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto. Unaweza kujiuliza kwanini Yohana alikuwa anawabatiza pale Yordani watu? Lengo kubwa ni kumjua Yesu, ili apate kumtwisha dhambi. Yohana alikuja kama kuhani wa wanadamu na Yesu alikuwa ni mwana-kondoo wa Mungu. Kwa sababu Yohana alikuwa hamjui Yesu ni nani ilibidi aanze kuwabatiza watu, na yeye aliyemtuma Yohana alimwambia yeye utakayemwona Roho anamshukia kama hua ndiye. Yohana ametokea katika uzao wa makuhani, uzao wa Haruni, kwahiyo tendo ambalo alikuwa analifanya ni tendo la kikuhani. Katika Agano la Kale ili dhambi za watu zipate kuondole ilikuwa ni lazima pawepo fahali ama kondoo wa ondoleo la dhambi lakini pia palikuwa na fahali ama mbuzi, ama mwana kondoo kwaajili ya upatanisho, hyu alikuwa anachinjwa na damu yake inakwenda kupatanishwa madhabahuni.

Tendo ambalo alikuwa analifanya Yohana alikuwa nafanya tendo la kikuhani, kama Babu zao walivyokuwa wanafanya. Sasa kwa hali hiyo ni kwamba, Yesu alikuja kama mwanakondoo ama mbuzi ambaye angechukua dhambi ya ulimwengu, Yohana mwenyewe alichuhudia kwamba , huyu ndiye mwana kondoo achukuaye dhambi ya ulimwengu. Tendo ambalo alifanya Yohana lilikuwa ni kumtwisha dhambi Yesu, sisi kubaki hatuna dhambi, kwa imani. Kama ilivyokuwa katika agano la kale, kuhani alisimama malangoni, na kuweka mikono yake juu ya fahali na kukiri dhambi, kwa imani dhambi za watu wote zilisafishwa. Watu wakuwa wabamwangalia kuhani wao alichokuwa anfanya. Hii ndio sababu ya Yesu kubatizwa katika mto Yordani lakini. Roho inamanishwa  kupokea Roho mtakatifu na kupatanishwa na Mungu. Tunapatanishwa na damu ya Yesu na kufanya agano takatifu.

Ili mtu azaliwe upya lazima aamini katika maji, ambayo ni ubatizo wa Yesu, damu, mateso yake msalabani ambayo yalitupatanisha na yeye kuwa kitu kimoja na Roho, ambao ni ufufuko wake Yesu baada ya kuteswa msalabani na sasa yupo hai anawabatiza watu kwa Roho Mtakatifu.

Ndugu, nimejibu kiufupi sana, jambo la muhimu ni hili, pata kitabu cha UKRISTO NA MAISHA, ili kujua zaidi na pia endeleo kusoma neno la Mungu baada ya kuamini. Tia juhudi katika kusoma. Yapo mengi ambayo atakuonyesha kipekee.

Ikiwa mtu anaaminiinjili hii atapokea haki ya Mungu, jambo la muhimu ni hili, kwenye kukiri, lazima utambue kwamba ulikuwa katika hatua fulani na unahitaji kwenda hatua nyingine. ASANTE.
Uliza lolote, upo huru.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65gmail.com.


  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg
Email ThisBlogThis!Share to XShare to Facebook
Newer Post Older Post Home

0 comments:

Post a Comment

Search This Blog

Translate

Total Pageviews

About Me

Sadick Kilasi
View my complete profile

Followers

Kurasa

  • Nyumbani
  • Saidia Huduma Hii Kuwafikia Wengi Zaidi.

Search This Blog

Blog Archive

  • ►  2020 (5)
    • ►  January (5)
  • ►  2019 (46)
    • ►  December (4)
    • ►  October (1)
    • ►  July (8)
    • ►  June (1)
    • ►  May (2)
    • ►  March (14)
    • ►  February (11)
    • ►  January (5)
  • ▼  2018 (275)
    • ►  December (17)
    • ►  November (25)
    • ▼  October (29)
      • Maisha Yenye Maana.
      • Wapi Ulipo?
      • Sala Ya Kuomba Amani.
      • Sicho Hicho Ndugu Yangu Unachohitaji.
      • Mwili Wako Ni Zawadi Kwa Wengine.
      • Utabiri Unaonesha Kwamba Wewe Utafurahia Maisha Ka...
      • Unachohitaji Katika Maisha Yako.
      • Kutambua Dalili Za Kujiliwa Kwa Jambo Jipya.
      • Ishi Kwa Kudhamiria Jambo Jema.
      • Ubatizo Ni Nini?
      • Upekee Unagharama Yake Ya Kulipa.
      • Ubatizo Wa Maji Mengi Na Ubatizo Wa Maji Machache,...
      • Uogope Woga unaokufanya Uwe Mwoga.
      • Jifunze Kwa Bidii Ili Uwe Huru.
      • Wakati Jama Wakati.
      • Madamu Unayo Leo Unaweza.
      • Viungo Vya Mwili Hufanya Kazi Kwa Ushilikiano.
      • Dunia Mama Haimtupi Mwenye Mwili.
      • Mwalimu Nyerere Zawadi Ya Afrika Na Dunia Kwa Ujumla.
      • Mambo Ya Kujua Na Kuepuka Ili Kudumisha Furaha Kat...
      • Unabadilisha Nguo Kila Siku, Kwanini Usibadilishe ...
      • Angalia Mbegu Unazokazana Kupanda.
      • Usikazane Kutafuta Raha Katika Maisha Bali Kazana ...
      • Ujumbe Uliobeba Ndani Yako.
      • Kila Mtu Yupo Bize Na Lugha Yake.
      • Mambo Ya Kuyatambua Katika Maisha Lakini Kuzingati...
      • Mwenyezi Mungu Ni Nani?
      • Hata Kama Umezaliwa Kwa Injili Ya Maji Na Roho Una...
      • Tujifunze Kutoka Kwa Panya Na Kuishi Maisha Yenye...
    • ►  September (43)
    • ►  August (7)
    • ►  July (12)
    • ►  June (17)
    • ►  May (19)
    • ►  April (31)
    • ►  March (33)
    • ►  February (25)
    • ►  January (17)
  • ►  2017 (58)
    • ►  December (16)
    • ►  November (22)
    • ►  October (2)
    • ►  September (11)
    • ►  August (4)
    • ►  July (3)
Sadick Kilasi. Powered by Blogger.

Jisajili kwa kujiunga nasi hapa

Posts
Atom
Posts
Comments
Atom
Comments
Maisha yenye maana ni yale maisha ambayo mhusika atambua nini kusudi lake la kuwepo hapa duniani. Hapandipo muhusika anapo kaa katika nafasi yake na kuwasha nuru katika sehemu aliopo kutokana uhusika wake. Jiunge na mtandao huu kupata maarifa zaidi na kwa ushirikiano mwingine kwa ujumla.

Kurasa

  • Nyumbani
  • TAFAKARI ROHO
  • Saidia Huduma Hii Kuwafikia Wengi Zaidi.

JIUNGE NASI SASA KWA KUJAZA FOMU HAPO CHINI


ANZA KUFURAHIA MAISHA NDANI YA YESU, MPOKEE ROHO MTAKATIFU KWA INJILI YA MAJI NA DAMU 0687000768

Zilizosomwa sana

  • Chukua hizi hapa nukuu za Malcolm x mtu ambaye anawavutia wengi sana.
    Ni siku nyingine tena ambayo ni mpya kabisa, karibu tena katika blogu hii ya JIKO LA USHAURI ambapo mimi mpendwa wako nimekuwa naingia jikon...
  • Ubatizo Wa Maji Mengi Na Ubatizo Wa Maji Machache, Upi Ni Sahihi?
    Ubatizo wa Maji Mengi Na Maji Machache. Kumekuwa na migongano kwa muda mrefu sana juu ya ubatizo, kati ya ubatizo wa maji mengi na ule uba...
  • Falsafa Za Maisha, Yaani Neno La Maarifa.
    Falsafa Za Maisha, Yaani Neno La Maarifa. Habari mpendwa? Natumai wewe unayesoma hapa umzima.   Karibu tena katika Falsafa Za Maisha. Ku...

Blog Archive

  • July 2017 (3)
  • August 2017 (4)
  • September 2017 (11)
  • October 2017 (2)
  • November 2017 (22)
  • December 2017 (16)
  • January 2018 (17)
  • February 2018 (25)
  • March 2018 (33)
  • April 2018 (31)
  • May 2018 (19)
  • June 2018 (17)
  • July 2018 (12)
  • August 2018 (7)
  • September 2018 (43)
  • October 2018 (29)
  • November 2018 (25)
  • December 2018 (17)
  • January 2019 (5)
  • February 2019 (11)
  • March 2019 (14)
  • May 2019 (2)
  • June 2019 (1)
  • July 2019 (8)
  • October 2019 (1)
  • December 2019 (4)
  • January 2020 (5)

JIKO LA USHAURI

Itambue Injili Ya Maji Na Roho. Ushiriki Ufalme wa Mungu, pata kitabu cha bure. Wasiliana nasi kwa sadikila65@gmail.com.

Tags

  • BIASHARA
  • HEKIMA ZA WAZEE
  • KUFURAHIA MAISHA
  • KUPATA BLOGU
  • MAHUSIANO
  • MAWASILIANO
  • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI
  • NJOZI
  • PATA BLOGU
  • SAIDIA HUDUMA HII
  • TAFAKARI NENO YA SIKU
  • TAFAKARI YA ROHO
  • UJASIRIAMALI
  • USHAURI
  • USWAZI TRICK

Kurasa

Labels

  • HEKIMA ZA WAZEE (24)
  • KUFURAHIA MAISHA (76)
  • KUPATA BLOGU (2)
  • MAHUSIANO (81)
  • MAWASILIANO (1)
  • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI (8)
  • NJOZI (94)
  • PATA BLOGU (3)
  • TAFAKARI YA ROHO (57)
  • UJASIRIAMALI (31)
  • USHAURI (78)
  • USWAZI TRICK (9)

Loading...

Fomu ya Anwani

Name

Email *

Message *

  • Napenda kusoma Biblia

About Me

Sadick Kilasi
View my complete profile
INJILI YA MAJI NA DAMU.

Search This Blog

Chapisho Lililoangaziwa

Alipambania Tumaini Lake Na Ndoto Yake Ikawa Kweli.

Kila mtu katika maisha ana tumaini lake. Msingi mkuu wa maisha ni tumaini. Nguvu kubwa ya maisha ni imani na mapito makuu ya maisha ni u...

Posts
Atom
Posts
Comments
Atom
Comments
INJILI YA KWELI NI INJILI YA MAJI NA ROHO. (MAJI, DAMU NA ROHO).
HII NDIYO KWELI YENYEWE.
YOHANA 19:34-35.

Copyright © JIKO LA USHAURI | Powered by Blogger
Design by Hardeep Asrani | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com | Distributed By Gooyaabi Templates