JIKO LA USHAURI

Itambue Injili Ya Maji Na Roho. Ushiriki Ufalme wa Mungu, pata kitabu cha bure. Wasiliana nasi kwa sadikila65@gmail.com.

  • NYUMBANI
  • KUFURAHIA MAISHA
    • ushauri
    • KUHUSU SISI
    • MAISHA NDANI YA YESU
  • MAWASILIANO
    • NAMBA YA SIMU
      • Sub 0687000768
      • Sub Child Category 2
      • facebook
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • NJOZI
  • SAIDIA HUDUMA HII
    • Childcare
    • Doctors
  • NYUMBANI
  • KUFURAHIA MAISHA
    • Stock
  • TAFAKARI YA ROHO
    • HEKIMA ZA WAZEE
    • Games
    • AFYA
      • Office
  • MAHUSIANO
    • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI
      • Sub Child Category 1
      • Sub Child Category 2
      • Sub Child Category 3
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • USHAURI
  • TAFAKARI NENO YA SIKU
    • Childcare
    • Doctors
  • PATA BLOGU

Thursday, October 18, 2018

Jifunze Kwa Bidii Ili Uwe Huru.

 Sadick Kilasi     October 18, 2018     No comments   



Ukiona unagombana na mtu ujue bado hujaanza kuishi uhalisia wa maisha ila upo tu katika kuishi. Kama bado unashangazwa na matukio jua bado una safari ndefu sana ya kufikia uhuru wa maisha.

Katika maisha yapo mambo mengi ambayo hutukia na ili kuyashinda ni muhimu zaidi kujifunza kwa kila tukio ambalo unapitia. Kama kwa sasa wewe ni kijana mtu mzima wa miaka ishirini na kuendelea ni wazi kwamba yapo mengi ambayo yametukia huko nyuma na inaweza ikawa zawadi yako kubwa sana ya kuishi maisha yenye maana kama utajifunza kwa yele ambayo umepitia.

Tuna mambo mengi sana ya kujifunza katika maisha, mahusiano, shughuli zetu, na mambo mengine ambayo tunapaswa kufahamu. Ili ufikie angalau kiwango cha kuweza kutatua matatizo kiurahisi, basi, utambuzi wa kutofautisha lazima uwe nao na lazima uwe na utambuzi wa kuielewa lugha.

Wengi huwa tunapuuzia katika swala la kujinza lakini swala la kujifunza ni sehenu muhimu sana kuliko jambo jingine.
Methali 4:7, Bora hekima, basi jipatie hekima; naam, kwa mapato yako yote jipatie ufahamu.

Dunia sio sehemu ambayo inauhalisia wa mambo, wakati wote kila jambo tunalolifanya ni lazima liende na mapungufu, ikiwa huna ufahamu hutaelewa hili. Ni muhimu zaidi kujifunza ni muhimu sana.

Kama wewe ni mmoja wa watu wazima sasa, unatambua kabisa, wakati mwingine unaweza ukawa unataka kuwasilisha jambo lakini watu wakawa wamelichukulia tofauti kabisa na namna ambavyo wewe ulikuwa unamaanisha. Unajikuta umeingia kwenye migogoro ambayo hukutarajia, lakini chanzo kikuu ni ukosefu wa ufahamu. Ufahamu unakupa utambuzi, utambuzi wa kutambua mazingira na lugha.

Mapito yako ni moja ya zawadi ambayo inaweza kukufanya kwa sasa ukafanya vizuri, na Mungu hutufanya tupitie katika wakati fulani na hawezi kuacha tuondoke hapo bila kuhakikisha tumeacha kovu ambalo ni ukumbusho kwetu. Wakati wana wa Israeli walipokuwa wanavuka katika joint ya mto Yordani, Mungu aliwataka wachukue mawe ya ukumbusho ili wawasimulie wanaye jambo lililo tukia hapo. Hii ndio zawadi ya mapito, mapito yanakufunza lakini usipofunzwa na mapito yako basi ni wazi mapito yako yatakuwa mapigo kwako.

Huwa ninakumbuka sana mapito ya nyuma, kwa kweli hapa ndipo ambapo siwezi kuacha kutafakari kwenye kila kitu. Nilisha wahi kuwakosea watu wengi sana kwa namna moja ama nyingine lakini leo mapito yangu ni zawadi kwangu. Naweza kufanya maamuzi sahihi kutokana na mapito yangu na makosa niliyofanya huko nyuma.

Ushawahi kujiuliza kwanini Mungu katumia gharama kubwa sana katika kutimiza neno la Mungu? Inawezekana hujawahi, lakini rafiki yangu, Mungu ametupa zawadi kubwa na yakipekee, wapo watu ambao walikufa kwenye biblia ili wewe ujifunze na uishi maisha ya maana, wapo watu ambao walipitia maisha magumu kwenye biblia ili wewe uishi maisha ya maana, wapo watu walifanya mambo mabaya kwenye biblia mambo yamerekodiwa ili wewe uishi maisha ya maana, wapo watu wamepigania kitabu kitakatifu ili wewe uishi maisha ya maana, wapo watawale ambao walikuwa na hekima ili wewe uishi maisha ya maana. Isitoshe, bado umepewa zawadi ya mapito yako. Roho Mtakatifu hukufundisha kila siku, mazingira ya asili ambayo unaishi nayo ni kwaajili yako, watu wanaokuzunguka waliofanikiwa na ambao hawajafanikiwa yote kwa sababu yako. Mungu amekupa kila kitu na mwisho bado anakwambia yeye ndio ngao yako na tuzo lako.

Ndugu yangu, tujifunze, tuvae utayari wa kujifunza kutoka kwake, haijarishi wewe ni mtu wa namna gani? Hata kama umeishia darasa la saba, wewe unafikiri watu wa zamani walikuwa wasomi? Akina Paulo watu ambao walikuwa na hekima ya kutosha na akina Sulemani, mtu mwenye hekima zaidi. Inawezekana ukanambia kwamba wao walitumiwa na Mungu, lakini kumbuka kwamba, Mungu alimaliza kazi yake siku ya saba na lazima utambue maandalio ya moyo ni ya mwanadamu, ukiuandaa moyo kwa kusudi la kupokea haki ya Mungu utapokea haki yake.

Leo hii changamoto nyingi hasa za migogoro ni kwa sababu ya kutokujifunza. Utambuzi na ufahamu ni kwaajili ya kushi maisha yenye maana. Tusitembee kama vipofu, tutajikuta tunafanya mambo yasiyofaa kwa sababu hatuna utayari wa kujifunza.

Mathayo 11:25-30,Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Namshukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako. Asema, nimekabidhiwa vyote na Baba yangu; wala hakuna amjuaye Baba, ila Mwana, na yeyote ambaye Mwana apenda kumfunulia. Njoni kwangu, nyinyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu mkajifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.

Ikiwa Yesu anamshukuru Mungu kwa sababu yeye amekabidhiwa kila kitu, basi nasi pia tunamshukuru Mungu kwani nasi ni ndugu wa Yesu kwa imani na pia amesema tujifunze kwake, tuvae nira yake tuwe kama yeye, ndipo tutapumzishwa. Na kuvaa nira yake inakupasa kujifunza, unajifunza kupitia neno lake  na kila kitu. Lakini yeye anasema yeye ni mpole na mnyenyekevu, kwa hiyo tunapaswa kuwa wanyenyekevu na wapole wakati tunajifunza.

Je! unataka kuishi maisha ya kustuka kila siku, mtu aliye  kama kipofu? Maana jibu la wakati ujao limefichwa ndani ya wakati. Lazima utambue kwamba Mungu anakupenda, kaa chini tafakari fikiri, acha kulaumu kila jambo. Ili watu wa dunia hii tufikie uhuru ni pale kila mmoja wetu atafikia kiwango cha kujitambua kipekee na ndipo hata kuwepo mtu wa kumlaumu mwingine. Watoto wanao zaliwa ni rahisi kuwasamehe kwa sababu hawatambui kitu lakini kwa mtu mzima akikuuzi ni lazima mgongano uwepo kwa sababu tunatambua kwa watu wazima wanajitambua. Lakini kwa sababu hata watu wazima hawana utayari wa kujinza changamoto inabaki pale pale. Lakini kama umejifunza ni rahisi kusamehe wengine.

Je! unatumia muda gani kujiadhibu wewe kama wewe kwa kutowafanyia wengine jambo la kufaa? Je! unatumia muda gani kusoma vitabu vitakatifu? Biblia ni kitabu ambacho kipo katika lugha ya kiswahili na kwa sasa mambo ni rahisi zaidi maana mpaka kwenye simu zipo Biblia. Je! unatumia muda gani kusoma vitabu vya kawaida. Paulo alikuwa ni msomaji wa vitabu, alikuwa anamwagiza Timotheo, wakati anakuja amletee koti lake bamoja vitabu vyake hasa vile vya ngozi. Je! unatumia muda gani kujisoma kwa mapito yako? Neno la Mungu linavutabu vya historia ndani yake. Je! unatumia muda gani kutafakari? Roho Mtakatifu humfundisha mtu anayetafakari. Je! unatumia muda gani kujinenea maneno ya kutaka kujifunza na kuomba Mungu akufundishe hekima yake? Vitabu vya unabii ni kwaajili ya kujinenea mambo hayo. Je! unatumia muda gani kutafakari mazingira yanayokuzunguka? Vitabu vya hekima vinafunza juu ya mambo haya, jifunze mpaka kwa sisimizi.

Mwisho wa yote Mungu ndiye Mfalme wa kila kitu, pale ambapo sisi hatuwezi basi yeye hutuvusha. Walipofika Yordani Mungu aligandisha maji, walikuwa hawezi kuvuka lakini Mungu akahusika kuwavusha. Mtumainie Mungu, uwe na moyo, usikate tamaa. ASANTE.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg
Email ThisBlogThis!Share to XShare to Facebook
Newer Post Older Post Home

0 comments:

Post a Comment

Search This Blog

Translate

Total Pageviews

About Me

Sadick Kilasi
View my complete profile

Followers

Kurasa

  • Nyumbani
  • Saidia Huduma Hii Kuwafikia Wengi Zaidi.

Search This Blog

Blog Archive

  • ►  2020 (5)
    • ►  January (5)
  • ►  2019 (46)
    • ►  December (4)
    • ►  October (1)
    • ►  July (8)
    • ►  June (1)
    • ►  May (2)
    • ►  March (14)
    • ►  February (11)
    • ►  January (5)
  • ▼  2018 (275)
    • ►  December (17)
    • ►  November (25)
    • ▼  October (29)
      • Maisha Yenye Maana.
      • Wapi Ulipo?
      • Sala Ya Kuomba Amani.
      • Sicho Hicho Ndugu Yangu Unachohitaji.
      • Mwili Wako Ni Zawadi Kwa Wengine.
      • Utabiri Unaonesha Kwamba Wewe Utafurahia Maisha Ka...
      • Unachohitaji Katika Maisha Yako.
      • Kutambua Dalili Za Kujiliwa Kwa Jambo Jipya.
      • Ishi Kwa Kudhamiria Jambo Jema.
      • Ubatizo Ni Nini?
      • Upekee Unagharama Yake Ya Kulipa.
      • Ubatizo Wa Maji Mengi Na Ubatizo Wa Maji Machache,...
      • Uogope Woga unaokufanya Uwe Mwoga.
      • Jifunze Kwa Bidii Ili Uwe Huru.
      • Wakati Jama Wakati.
      • Madamu Unayo Leo Unaweza.
      • Viungo Vya Mwili Hufanya Kazi Kwa Ushilikiano.
      • Dunia Mama Haimtupi Mwenye Mwili.
      • Mwalimu Nyerere Zawadi Ya Afrika Na Dunia Kwa Ujumla.
      • Mambo Ya Kujua Na Kuepuka Ili Kudumisha Furaha Kat...
      • Unabadilisha Nguo Kila Siku, Kwanini Usibadilishe ...
      • Angalia Mbegu Unazokazana Kupanda.
      • Usikazane Kutafuta Raha Katika Maisha Bali Kazana ...
      • Ujumbe Uliobeba Ndani Yako.
      • Kila Mtu Yupo Bize Na Lugha Yake.
      • Mambo Ya Kuyatambua Katika Maisha Lakini Kuzingati...
      • Mwenyezi Mungu Ni Nani?
      • Hata Kama Umezaliwa Kwa Injili Ya Maji Na Roho Una...
      • Tujifunze Kutoka Kwa Panya Na Kuishi Maisha Yenye...
    • ►  September (43)
    • ►  August (7)
    • ►  July (12)
    • ►  June (17)
    • ►  May (19)
    • ►  April (31)
    • ►  March (33)
    • ►  February (25)
    • ►  January (17)
  • ►  2017 (58)
    • ►  December (16)
    • ►  November (22)
    • ►  October (2)
    • ►  September (11)
    • ►  August (4)
    • ►  July (3)
Sadick Kilasi. Powered by Blogger.

Jisajili kwa kujiunga nasi hapa

Posts
Atom
Posts
Comments
Atom
Comments
Maisha yenye maana ni yale maisha ambayo mhusika atambua nini kusudi lake la kuwepo hapa duniani. Hapandipo muhusika anapo kaa katika nafasi yake na kuwasha nuru katika sehemu aliopo kutokana uhusika wake. Jiunge na mtandao huu kupata maarifa zaidi na kwa ushirikiano mwingine kwa ujumla.

Kurasa

  • Nyumbani
  • TAFAKARI ROHO
  • Saidia Huduma Hii Kuwafikia Wengi Zaidi.

JIUNGE NASI SASA KWA KUJAZA FOMU HAPO CHINI


ANZA KUFURAHIA MAISHA NDANI YA YESU, MPOKEE ROHO MTAKATIFU KWA INJILI YA MAJI NA DAMU 0687000768

Zilizosomwa sana

  • Chukua hizi hapa nukuu za Malcolm x mtu ambaye anawavutia wengi sana.
    Ni siku nyingine tena ambayo ni mpya kabisa, karibu tena katika blogu hii ya JIKO LA USHAURI ambapo mimi mpendwa wako nimekuwa naingia jikon...
  • Ubatizo Wa Maji Mengi Na Ubatizo Wa Maji Machache, Upi Ni Sahihi?
    Ubatizo wa Maji Mengi Na Maji Machache. Kumekuwa na migongano kwa muda mrefu sana juu ya ubatizo, kati ya ubatizo wa maji mengi na ule uba...
  • Falsafa Za Maisha, Yaani Neno La Maarifa.
    Falsafa Za Maisha, Yaani Neno La Maarifa. Habari mpendwa? Natumai wewe unayesoma hapa umzima.   Karibu tena katika Falsafa Za Maisha. Ku...

Blog Archive

  • July 2017 (3)
  • August 2017 (4)
  • September 2017 (11)
  • October 2017 (2)
  • November 2017 (22)
  • December 2017 (16)
  • January 2018 (17)
  • February 2018 (25)
  • March 2018 (33)
  • April 2018 (31)
  • May 2018 (19)
  • June 2018 (17)
  • July 2018 (12)
  • August 2018 (7)
  • September 2018 (43)
  • October 2018 (29)
  • November 2018 (25)
  • December 2018 (17)
  • January 2019 (5)
  • February 2019 (11)
  • March 2019 (14)
  • May 2019 (2)
  • June 2019 (1)
  • July 2019 (8)
  • October 2019 (1)
  • December 2019 (4)
  • January 2020 (5)

JIKO LA USHAURI

Itambue Injili Ya Maji Na Roho. Ushiriki Ufalme wa Mungu, pata kitabu cha bure. Wasiliana nasi kwa sadikila65@gmail.com.

Tags

  • BIASHARA
  • HEKIMA ZA WAZEE
  • KUFURAHIA MAISHA
  • KUPATA BLOGU
  • MAHUSIANO
  • MAWASILIANO
  • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI
  • NJOZI
  • PATA BLOGU
  • SAIDIA HUDUMA HII
  • TAFAKARI NENO YA SIKU
  • TAFAKARI YA ROHO
  • UJASIRIAMALI
  • USHAURI
  • USWAZI TRICK

Kurasa

Labels

  • HEKIMA ZA WAZEE (24)
  • KUFURAHIA MAISHA (76)
  • KUPATA BLOGU (2)
  • MAHUSIANO (81)
  • MAWASILIANO (1)
  • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI (8)
  • NJOZI (94)
  • PATA BLOGU (3)
  • TAFAKARI YA ROHO (57)
  • UJASIRIAMALI (31)
  • USHAURI (78)
  • USWAZI TRICK (9)

Loading...

Fomu ya Anwani

Name

Email *

Message *

  • Napenda kusoma Biblia

About Me

Sadick Kilasi
View my complete profile
INJILI YA MAJI NA DAMU.

Search This Blog

Chapisho Lililoangaziwa

Alipambania Tumaini Lake Na Ndoto Yake Ikawa Kweli.

Kila mtu katika maisha ana tumaini lake. Msingi mkuu wa maisha ni tumaini. Nguvu kubwa ya maisha ni imani na mapito makuu ya maisha ni u...

Posts
Atom
Posts
Comments
Atom
Comments
INJILI YA KWELI NI INJILI YA MAJI NA ROHO. (MAJI, DAMU NA ROHO).
HII NDIYO KWELI YENYEWE.
YOHANA 19:34-35.

Copyright © JIKO LA USHAURI | Powered by Blogger
Design by Hardeep Asrani | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com | Distributed By Gooyaabi Templates