JIKO LA USHAURI

Itambue Injili Ya Maji Na Roho. Ushiriki Ufalme wa Mungu, pata kitabu cha bure. Wasiliana nasi kwa sadikila65@gmail.com.

  • NYUMBANI
  • KUFURAHIA MAISHA
    • ushauri
    • KUHUSU SISI
    • MAISHA NDANI YA YESU
  • MAWASILIANO
    • NAMBA YA SIMU
      • Sub 0687000768
      • Sub Child Category 2
      • facebook
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • NJOZI
  • SAIDIA HUDUMA HII
    • Childcare
    • Doctors
  • NYUMBANI
  • KUFURAHIA MAISHA
    • Stock
  • TAFAKARI YA ROHO
    • HEKIMA ZA WAZEE
    • Games
    • AFYA
      • Office
  • MAHUSIANO
    • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI
      • Sub Child Category 1
      • Sub Child Category 2
      • Sub Child Category 3
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • USHAURI
  • TAFAKARI NENO YA SIKU
    • Childcare
    • Doctors
  • PATA BLOGU

Thursday, November 15, 2018

Mshukuru Mungu Kwa Kila Kitu.

 Sadick Kilasi     November 15, 2018     KUFURAHIA MAISHA     No comments   



Habari Ndugu yangu? Katika wiki ya shukrani, tunaendelea kuyapa thamani kubwa maisha yetu.

Leo hii tunaiendea siku yetu kwa kumshukuru Mungu kwa kila kitu. Unaposhukuru kwa kila kitu, unashukuru kwa sababu unaelewa ni kitu gani unashukuru.

Mpendwa Ndugu yangu, tunasema mapito ni zawadi yetu, kilichopo ni jibu ya changamoto yetu, naam, tumaini ni nguvu yetu. Ukweli ni kwamba hatuna cha kupoteza katika maisha yetu.


Sisi ambao tumechagua kuishi Nuru, neno ningeli halitutawali. Kama tulifanya makosa hapo mwanzo iliikuwa ni sababu ya kufanya maamuzi bora hivi sasa.

Tunapo mshukuru Mungu kwa kila kitu, hii inafanya tuthamini kile ambacho Mungu amekupa. Nenda leo kwa shukrani, mshukuru Mungu kwa chochote ambacho inakiona mbele yako, mshukuru Mungu kwa historia unazopata lakini pia tumaini letu linapenya patakatifu pa mbinguni, tumetia nanga huko ili tumaini letu liwe lenye nguvu.

Mshukuru Mungu kwa neno lake ambalo umekuwa unalisoma, mshukuru Mungu kwa watu waliokufa kwenye historia zao kwa kuingia katika hatari kubwa ili wewe upate kuishi maisha mema. Wapo wengi waliokufa katika biblia, ili wewe uwasome na uishi maisha yenye maana sasa.

Mshukuru Mungu kwa watu watumishi ambao wanakufundisha na unasoma vitabu vyao, usije ukafikiri huwa unasoma kwa nguvu zako.

Mshukuru Mungu kwa hali ya hewa hivi sasa ili ikichafuka usije ukajutia. Japokuwa itaonekana mjinga ama utajiona wewe mwenyewe mjinga ukimshukuru Mungu kwa ndege, wadudu na wanyama unaowaona, lakini nikwambie ukweli kila kitu cha asili ni zawadi kwa wenye mwili.

Angalia ndege, sauti zao zinakufariji, angalia wanyama pambo la ulimwengu, angalia miti huleta harufu nzuri na kusababisha mvua kunyesha, angalia watu wako wa karibu, ni zawadi yako hao. Usijali kama sasa wapo bize lakini ukweli ni kwamba ukisukwa na jambo zito hapo ndio wa kwanza kukuinua. Mshukuru Mungu kwa kila kitu, usiache chochote.

Unapomshukuru Mungu kwa kila kitu, ni sawa na kupokea kila kitu ambacho Mungu amekupa. Na zaidi ya yote, Mungu ataendelea kukupa zaidi kwa sababu akikupa unapokea.

Je! Ushawahi kumshukuru Mungu kwa ardhi uliyoikanyaga, thamani ya maisha yetu ni pale tulipo. Angalia kwa macho yako jinsi ulivyo hai, gusa mkono wako kwenye moyo uone moyo wako unavodunda, cheki macho yako yanavoona mengi, sikiliza ndugu yangu, akili yako ipo vizuri na ndiomaana unasoma hapa, masikio yako yapo sawa na ndiomaana unasikia, kinywa chako kipo sawa na ndiomaana unasema. Wapo wengi wenye mapungufu ya hivyo vitu, ijapokuwa ni kimoja tu kati ya hivyo, lakini vinawanyima furaha kwa sababu hawana.

Mpendwa Ndugu yangu, inawezekana maisha yako ni magumu, ni magumu kwa sababu hutimizi ndoto zako na huna furaha kwa hilo. Lakini nataka nikwambie kitu kimoja, kuna watu wanapigania maisha ya familia zao, hawajawahi kufikiria juu ya familia zao. Watoto wao kila siku wanahitaji ada na chakula. Kuna wengine wamekosa furaha kwa sababu hata mtoto wa kumlipia ada hana.

Ninachotaka ni nini Ndugu yangu, ni wewe kuangalia ulichonacho na ukione kwa macho yako ikisha mshukuru Mungu. Mungu ametupa kila kitu, lakini hatutaki kukubali kile Mungu ametupa,  Mungu hatupi kile ambacho tunataka bali anatupa kile ambacho tunahitaji.

Siku hii ya leo, ipe thamani kubwa sana, ukiipa leo thamani kubwa itafanya vizuri sana kwenye kile unachofanya, zaidi kesho itakuwa siku ya thamani zaidi ya leo. Ipe leo thamani kubwa tumia kila kitu ambacho umepewa na Mungu  ulichonacho kuhakikisha, maisha yako na ya wengine pia yanakuwa bora zaidi ya ulivyofikiri.

Usiangalie udogo wa jambo, bali tumia vizuri kama zawadi yako. Ndugu yangu, miili yetu ni mikubwa, na ipo kwa sababu ya cell za mwili ambazo ni ndogo ndogo sana kiasi kwamba hata kwa macho huzioni. Usiangalie ni kitu gani huna, bali angalia ni namna gani unavyoweza kubooresha maisha yako zaidi kwa vile vidogo ulivyonavyo ili vifanye kikubwa kiwe hai.

Siku ya leo na vyote unavyoviona ni zawadi yako. Asante.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg
Email ThisBlogThis!Share to XShare to Facebook
Newer Post Older Post Home

0 comments:

Post a Comment

Search This Blog

Translate

Total Pageviews

About Me

Sadick Kilasi
View my complete profile

Followers

Kurasa

  • Nyumbani
  • Saidia Huduma Hii Kuwafikia Wengi Zaidi.

Search This Blog

Blog Archive

  • ►  2020 (5)
    • ►  January (5)
  • ►  2019 (46)
    • ►  December (4)
    • ►  October (1)
    • ►  July (8)
    • ►  June (1)
    • ►  May (2)
    • ►  March (14)
    • ►  February (11)
    • ►  January (5)
  • ▼  2018 (275)
    • ►  December (17)
    • ▼  November (25)
      • Katika Wiki Ya Kukua, Wewe Umeachwa.
      • Katika Wiki Ya Kukua, Kama Hatua Unazopiga Unapoel...
      • Katika Wiki Ya Kukua, Washa Njiti Yako.
      • Katika Wiki Ya Kukua.
      • Je! Ndege Hutegemea Tawi Alilotua?
      • Katika Wiki Ya Kutawala, Mungu Ndiye Mfalme Wa Kil...
      • Katika Wiki Ya Kutawala, Jiweke Nafasi Ya Wengine.
      • Katika Wiki Ya Kutawala, Moyo Huwa Unakubali.
      • Katika Wiki Ya Kutawala, Inahitaji Utambuzi Na Aki...
      • Katika Wiki Ya Kutawala, Toka Nje Ya Hema Yako.
      • Ndani Ya Wiki Ya Kujitawala, Jitambue Wewe Mwenyewe.
      • Katika Wiki Ya Shukrani, Itazame Wiki Yako Imekwen...
      • Katika Wiki Ya Shukrani, Ni Nani Aliyempanzi Wa Tu...
      • Mshukuru Mungu Kwa Kila Kitu.
      • Katika Wiki Ya Shukrani, Tambua Kitu Kikuongoze Ka...
      • Katika Wiki Ya Shukrani; Anza Na Chochote.
      • Ndani Ya Wiki Ya Shukrani, Mtazamo Wa Kudumisha Il...
      • Wiki Ya Shukrani.
      • Tabia Nne Za Kuishi.
      • Kuwa Na Jicho La Tai, Ishi Matumaini.
      • Elewa Kinachofuata.
      • Asiye Na Maarifa Hali Vya Babaye.
      • Mchakato Upo Kinywani Na Ladha Ipo Kinywani.
      • Adhibu Matendo Yako.
      • Kama Ndege Arukaye Angani.
    • ►  October (29)
    • ►  September (43)
    • ►  August (7)
    • ►  July (12)
    • ►  June (17)
    • ►  May (19)
    • ►  April (31)
    • ►  March (33)
    • ►  February (25)
    • ►  January (17)
  • ►  2017 (58)
    • ►  December (16)
    • ►  November (22)
    • ►  October (2)
    • ►  September (11)
    • ►  August (4)
    • ►  July (3)
Sadick Kilasi. Powered by Blogger.

Jisajili kwa kujiunga nasi hapa

Posts
Atom
Posts
Comments
Atom
Comments
Maisha yenye maana ni yale maisha ambayo mhusika atambua nini kusudi lake la kuwepo hapa duniani. Hapandipo muhusika anapo kaa katika nafasi yake na kuwasha nuru katika sehemu aliopo kutokana uhusika wake. Jiunge na mtandao huu kupata maarifa zaidi na kwa ushirikiano mwingine kwa ujumla.

Kurasa

  • Nyumbani
  • TAFAKARI ROHO
  • Saidia Huduma Hii Kuwafikia Wengi Zaidi.

JIUNGE NASI SASA KWA KUJAZA FOMU HAPO CHINI


ANZA KUFURAHIA MAISHA NDANI YA YESU, MPOKEE ROHO MTAKATIFU KWA INJILI YA MAJI NA DAMU 0687000768

Zilizosomwa sana

  • Chukua hizi hapa nukuu za Malcolm x mtu ambaye anawavutia wengi sana.
    Ni siku nyingine tena ambayo ni mpya kabisa, karibu tena katika blogu hii ya JIKO LA USHAURI ambapo mimi mpendwa wako nimekuwa naingia jikon...
  • Ubatizo Wa Maji Mengi Na Ubatizo Wa Maji Machache, Upi Ni Sahihi?
    Ubatizo wa Maji Mengi Na Maji Machache. Kumekuwa na migongano kwa muda mrefu sana juu ya ubatizo, kati ya ubatizo wa maji mengi na ule uba...
  • Falsafa Za Maisha, Yaani Neno La Maarifa.
    Falsafa Za Maisha, Yaani Neno La Maarifa. Habari mpendwa? Natumai wewe unayesoma hapa umzima.   Karibu tena katika Falsafa Za Maisha. Ku...

Blog Archive

  • July 2017 (3)
  • August 2017 (4)
  • September 2017 (11)
  • October 2017 (2)
  • November 2017 (22)
  • December 2017 (16)
  • January 2018 (17)
  • February 2018 (25)
  • March 2018 (33)
  • April 2018 (31)
  • May 2018 (19)
  • June 2018 (17)
  • July 2018 (12)
  • August 2018 (7)
  • September 2018 (43)
  • October 2018 (29)
  • November 2018 (25)
  • December 2018 (17)
  • January 2019 (5)
  • February 2019 (11)
  • March 2019 (14)
  • May 2019 (2)
  • June 2019 (1)
  • July 2019 (8)
  • October 2019 (1)
  • December 2019 (4)
  • January 2020 (5)

JIKO LA USHAURI

Itambue Injili Ya Maji Na Roho. Ushiriki Ufalme wa Mungu, pata kitabu cha bure. Wasiliana nasi kwa sadikila65@gmail.com.

Tags

  • BIASHARA
  • HEKIMA ZA WAZEE
  • KUFURAHIA MAISHA
  • KUPATA BLOGU
  • MAHUSIANO
  • MAWASILIANO
  • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI
  • NJOZI
  • PATA BLOGU
  • SAIDIA HUDUMA HII
  • TAFAKARI NENO YA SIKU
  • TAFAKARI YA ROHO
  • UJASIRIAMALI
  • USHAURI
  • USWAZI TRICK

Kurasa

Labels

  • HEKIMA ZA WAZEE (24)
  • KUFURAHIA MAISHA (76)
  • KUPATA BLOGU (2)
  • MAHUSIANO (81)
  • MAWASILIANO (1)
  • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI (8)
  • NJOZI (94)
  • PATA BLOGU (3)
  • TAFAKARI YA ROHO (57)
  • UJASIRIAMALI (31)
  • USHAURI (78)
  • USWAZI TRICK (9)

Loading...

Fomu ya Anwani

Name

Email *

Message *

  • Napenda kusoma Biblia

About Me

Sadick Kilasi
View my complete profile
INJILI YA MAJI NA DAMU.

Search This Blog

Chapisho Lililoangaziwa

Alipambania Tumaini Lake Na Ndoto Yake Ikawa Kweli.

Kila mtu katika maisha ana tumaini lake. Msingi mkuu wa maisha ni tumaini. Nguvu kubwa ya maisha ni imani na mapito makuu ya maisha ni u...

Posts
Atom
Posts
Comments
Atom
Comments
INJILI YA KWELI NI INJILI YA MAJI NA ROHO. (MAJI, DAMU NA ROHO).
HII NDIYO KWELI YENYEWE.
YOHANA 19:34-35.

Copyright © JIKO LA USHAURI | Powered by Blogger
Design by Hardeep Asrani | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com | Distributed By Gooyaabi Templates