JIKO LA USHAURI

Itambue Injili Ya Maji Na Roho. Ushiriki Ufalme wa Mungu, pata kitabu cha bure. Wasiliana nasi kwa sadikila65@gmail.com.

  • NYUMBANI
  • KUFURAHIA MAISHA
    • ushauri
    • KUHUSU SISI
    • MAISHA NDANI YA YESU
  • MAWASILIANO
    • NAMBA YA SIMU
      • Sub 0687000768
      • Sub Child Category 2
      • facebook
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • NJOZI
  • SAIDIA HUDUMA HII
    • Childcare
    • Doctors
  • NYUMBANI
  • KUFURAHIA MAISHA
    • Stock
  • TAFAKARI YA ROHO
    • HEKIMA ZA WAZEE
    • Games
    • AFYA
      • Office
  • MAHUSIANO
    • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI
      • Sub Child Category 1
      • Sub Child Category 2
      • Sub Child Category 3
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • USHAURI
  • TAFAKARI NENO YA SIKU
    • Childcare
    • Doctors
  • PATA BLOGU

Saturday, November 10, 2018

Kuwa Na Jicho La Tai, Ishi Matumaini.

 Sadick Kilasi     November 10, 2018     KUFURAHIA MAISHA     No comments   

Kuwa Kama Tai.

Tai ni ndege wa kipekee sana. Huishi kwa imani kubwa anapofanya mawindo.  Ukimwangali tai anapofanya mawindo unaweza kujifunza kitu kikubwa sana.

Tai anapotaka kufanya mawindo yake huenda juu sana (juu ya anga), ikisha hujitengeneza katika upande fulani wa pembe na kuangalia chini akiwa mbali kutoka juu. Huitazama dunia kwa lengo la kutaka kupata kitu huku akiwa amejitayarisha kupata anachotaka.

Hupata kile anachotaka kupata akiwa mbali sana juu ya anga, huangalia chini wakati mwingine humwona panya, nyoka na wanyama wengine wanaofaa kuliwa na yeye. Jicho lake hutazama akiwa mbali sana, huchagua anachotaka na kukiendea kile anachotaka kwa kasi ya ajabu. Bila kufanya kosa katika mkao ule ule ambao amekaa, hujiachilia na kukifuatia kile ambacho anakitumainia kukipata. Jambo la kushangaza ni kwamba hata chini kukiwa na wanyama wengi hufuata yule ambaye alikuwa amemtagenti katika pembe aliyokuwa amempimia. Jicho lake huona kutoka mbali sana, hata kama samaki akiwa amejificha chini ya maji jicho lake humwona na kumkamata kwa kujifanyia mawindo yake. Na huwa na maeneo maalumu ambayo atamshika,(shingoni) na kwa jinsi alivyokuwa amejiwekea shabaha yake hushika maeneo yale yale.

Mpendwa msomaji, ikiwa tunaweza kujifunza kutoka kwa tai basi tunaweza kuishi maisha ya maana sana.

Kitu kikubwa ambacho kinafanya maisha yetu yanakosa maana ni kukosa shukrani. Kama jicho letu lingekuwa kama la tai mambo yote yangekuwa na maana sana.

Watu wengi tumekosa matumaini kwa sababu hatuna shukrani. Hatutaki kuamini kile ambacho tayari tunacho, hatutaki kufanya chaguo la muhimu, hatutaki kupokea kile ambacho tayari tunacho. Siku zote tumekuwa tunaishi maisha ya kutamainia vile ambavyo tayari hatunavyo. Lakini licha ya kuwa tunatamania vile ambavyo hatuna bado vile ambavyo tunavyo hatuvikubali. Katika mfumo wa kutembea, huwezi kukandamiza ardhi inayofuata kwa unyayo wako kabla ya kukandamiza ardhi uliyokanyaga kwanza. Kandamiza ulipokanyaga ikisha uendelee mbele. Siku hizi watu wamepotoka kabisa, eti umaskini ni laana, laana maanake nini? Chukua hatua anza kukua ili kwenda unakoelekea.

Maisha yanacheza katika nyanja tatu; imani, utayari na matumaini. Imani huja kwa kusikia, kama huwezi kuamini kile ambacho umekiona, utaaminije kile ambacho hujakiona? Utayari ni kuishi kile ambacho tayari unacho. Matumaini ni maono ya mbali zaidi. Sasa huwezi kuwa na imani ya mbali kama hakuna kidogo cha jilani ambacho tayari unacho. Unapokubari kile ambacho ni kidogo inamaana tayari unaweza kukubali kwamba kuna vikubwa vinakuja.

Shukrani ni uwezo wa kukubali kidogo ambacho tayari unacho ili kupata kikubwa zaidi ambacho hicho sasa tunaita matumaini yako, ama maono yako.

Sasa rafiki yangu, kuwa na jicho la tai, kaa katika makao wa jicho la kuona chema kinachoweza kukupa nguvu ya kuishi tena. Ichunguze harufu ya maisha yako na kitumainie chakula hicho.

Kubali vile ambavyo Mungu kakupa tayari na uache kulalamika na songa mbele. Wakati nabii Elisha alipoletewa lalamiko na mke wa mwanafunzi wake ambaye tayari alikuwa amekufa, na mwanamke huyo alimletea mararamiko kwamba anadaiwa, nabii Elisha alimwuliza kwanza nikusaidie nini? Una nini nyumbani kwako? Akamwambia nina chupa ya mafuta, akamwambia akusanye vyombo vingi ili apate kumimina mafuta, alimimina mafuta vyombo vyote vikajaa mpaka akaenda kuazima vyombo kwa majilani, pale aliposema vyombo vimeisha na ndipo mafuta yaliisha ndani ya chupa. Akaenda kuuza mafuta na kupata fedha na kulipa madeni yake.

Ndugu yangu, popote pale tulipo kipo ambacho tunaweza kufanya, popote pale tulipo kipo ambacho kinaweza kuwa harufu nzuri ya maisha yetu, chukua hatua ili uishi utamu wa harufu. Ingia kwa shukrani wakati unapikea vitu vitakatifu. Acha kulalamika.

Makuhani katika Agano la kale walikuwa wanaingia patakatifu huku wamefumba macho. Ikiwa inamaanisha shukrani kwa kile ambacho tayari umepewa.

Acha kuwa mchoyo, uchoyo ni pale ambapo unasema huna kitu kumbe umeficha mengi ndani yako. Hakuna mtu ambaye hana kitu, mtu yeyote ana kitu cha kumpa mwingine. Neno linasema katika Zaburi, nyingi ni miungu lakini msipowasaidia wengine mtakufa maskini. Ikiwa tutakuwa wachoyo wa vile ambavyo tayari tunavyo  itakuwa kama watu waliokufa. Bwawa lenye maji ambapo haliingizi wala kutoa maji ni lazima maji yake yanuke tu. Hivyo hivyo uliyo unaweza kuirutibisha ardhi yaani watu. Wakati Mungu anatuumba hakutuumba tuwategemee wengine na kama unasoma hapa basi tayari wewe unapaswa kutegemewa na wengine.

Umefungia uwezo wako ndani yako, harafu unasema huna kitu, Mungu katuita sisi Miungu sasa unaposema huna kitu ni kufuru. Hatupati kile tuomba kwa sababu hatukubali kile ambacho tunapewa.

Sasa nataka tuanze kuishi kwa shukrani, nataka mimi na wewe rafiki yangu unayesoma hapa tuishi maisha badala ya kuigiza kuishi maisha.

Nimeanda mfumo wa kuishi maisha yenye maana kwa mwezi mzima; wiki ya kwanza itakuwa wiki ya shukrani, wiki ya pili itakuwa wiki ya kutawala, wiki ya tatu itakuwa wiki ya hamasa na wiki  ya nne ni wiki ya kukua.

Hivi ndivyo ambavyo tutaishi ndani ya mwezi mzima. Na vitu vipo ndani ya mwanadamu, ukisoma katika kitabu cha ufunuo utaona.
Ni lazima tuishi maisha yenye maana ili dunia iwe sehemu sahihi ya kuishi.

Katika maeneo yote manne tutakuwa tunaiendea siku kwa mfumo maalamu. Kama ni wiki ya shukrani basi jambo la kwanza kulitanguliza litakuwa ni shukrani na huku mengine yanafuata kwa nyuma, kama ni wiki ya hamasa basi mwogozo wetu kwa wiki hiyo ni hamasa, mengine yatafuata kwa nyuma.

Ni nani atashiriki? Tutatengeneza group ambalo kila siku asubuhi tutakuwa tunapata kianzio cha mwongozo wetu. WhatsApp group inatosha. Hii haina gharama yoyote. Kama upo tayari nitumie ujumbe  0687000768. Ni mengi ambayo tutajifunza na kufanya maisha yetu yawe na ladha na kwa wengine pia.

Watu wanao hitajika kuanzia kumi na tano, kushuka, ama kumi, ama watano ama pake yangu. Wowote wale ambao wapo tayari kufanya hivyo basi ndio hao.

Lengo ni kuanza na sisi wenyewe harafu baadae kutoka nje zaidi na kuwafanya wengine kuwa na matumaini zaidi kwa kutumia vipawa vya uwezo wetu.

Karibu sana, tuna ujumbe 0687000768 au sadikila65@gmail.com. Kwa pamoja zaidi tunakwenda mbali zaidi. Dunia imekosa kitu kinachoitwa umoja, badala yake kila mtu anaishi na kuhitaji kufalijiwa. ASANTE.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.


  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg
Email ThisBlogThis!Share to XShare to Facebook
Newer Post Older Post Home

0 comments:

Post a Comment

Search This Blog

Translate

Total Pageviews

About Me

Sadick Kilasi
View my complete profile

Followers

Kurasa

  • Nyumbani
  • Saidia Huduma Hii Kuwafikia Wengi Zaidi.

Search This Blog

Blog Archive

  • ►  2020 (5)
    • ►  January (5)
  • ►  2019 (46)
    • ►  December (4)
    • ►  October (1)
    • ►  July (8)
    • ►  June (1)
    • ►  May (2)
    • ►  March (14)
    • ►  February (11)
    • ►  January (5)
  • ▼  2018 (275)
    • ►  December (17)
    • ▼  November (25)
      • Katika Wiki Ya Kukua, Wewe Umeachwa.
      • Katika Wiki Ya Kukua, Kama Hatua Unazopiga Unapoel...
      • Katika Wiki Ya Kukua, Washa Njiti Yako.
      • Katika Wiki Ya Kukua.
      • Je! Ndege Hutegemea Tawi Alilotua?
      • Katika Wiki Ya Kutawala, Mungu Ndiye Mfalme Wa Kil...
      • Katika Wiki Ya Kutawala, Jiweke Nafasi Ya Wengine.
      • Katika Wiki Ya Kutawala, Moyo Huwa Unakubali.
      • Katika Wiki Ya Kutawala, Inahitaji Utambuzi Na Aki...
      • Katika Wiki Ya Kutawala, Toka Nje Ya Hema Yako.
      • Ndani Ya Wiki Ya Kujitawala, Jitambue Wewe Mwenyewe.
      • Katika Wiki Ya Shukrani, Itazame Wiki Yako Imekwen...
      • Katika Wiki Ya Shukrani, Ni Nani Aliyempanzi Wa Tu...
      • Mshukuru Mungu Kwa Kila Kitu.
      • Katika Wiki Ya Shukrani, Tambua Kitu Kikuongoze Ka...
      • Katika Wiki Ya Shukrani; Anza Na Chochote.
      • Ndani Ya Wiki Ya Shukrani, Mtazamo Wa Kudumisha Il...
      • Wiki Ya Shukrani.
      • Tabia Nne Za Kuishi.
      • Kuwa Na Jicho La Tai, Ishi Matumaini.
      • Elewa Kinachofuata.
      • Asiye Na Maarifa Hali Vya Babaye.
      • Mchakato Upo Kinywani Na Ladha Ipo Kinywani.
      • Adhibu Matendo Yako.
      • Kama Ndege Arukaye Angani.
    • ►  October (29)
    • ►  September (43)
    • ►  August (7)
    • ►  July (12)
    • ►  June (17)
    • ►  May (19)
    • ►  April (31)
    • ►  March (33)
    • ►  February (25)
    • ►  January (17)
  • ►  2017 (58)
    • ►  December (16)
    • ►  November (22)
    • ►  October (2)
    • ►  September (11)
    • ►  August (4)
    • ►  July (3)
Sadick Kilasi. Powered by Blogger.

Jisajili kwa kujiunga nasi hapa

Posts
Atom
Posts
Comments
Atom
Comments
Maisha yenye maana ni yale maisha ambayo mhusika atambua nini kusudi lake la kuwepo hapa duniani. Hapandipo muhusika anapo kaa katika nafasi yake na kuwasha nuru katika sehemu aliopo kutokana uhusika wake. Jiunge na mtandao huu kupata maarifa zaidi na kwa ushirikiano mwingine kwa ujumla.

Kurasa

  • Nyumbani
  • TAFAKARI ROHO
  • Saidia Huduma Hii Kuwafikia Wengi Zaidi.

JIUNGE NASI SASA KWA KUJAZA FOMU HAPO CHINI


ANZA KUFURAHIA MAISHA NDANI YA YESU, MPOKEE ROHO MTAKATIFU KWA INJILI YA MAJI NA DAMU 0687000768

Zilizosomwa sana

  • Chukua hizi hapa nukuu za Malcolm x mtu ambaye anawavutia wengi sana.
    Ni siku nyingine tena ambayo ni mpya kabisa, karibu tena katika blogu hii ya JIKO LA USHAURI ambapo mimi mpendwa wako nimekuwa naingia jikon...
  • Ubatizo Wa Maji Mengi Na Ubatizo Wa Maji Machache, Upi Ni Sahihi?
    Ubatizo wa Maji Mengi Na Maji Machache. Kumekuwa na migongano kwa muda mrefu sana juu ya ubatizo, kati ya ubatizo wa maji mengi na ule uba...
  • Falsafa Za Maisha, Yaani Neno La Maarifa.
    Falsafa Za Maisha, Yaani Neno La Maarifa. Habari mpendwa? Natumai wewe unayesoma hapa umzima.   Karibu tena katika Falsafa Za Maisha. Ku...

Blog Archive

  • July 2017 (3)
  • August 2017 (4)
  • September 2017 (11)
  • October 2017 (2)
  • November 2017 (22)
  • December 2017 (16)
  • January 2018 (17)
  • February 2018 (25)
  • March 2018 (33)
  • April 2018 (31)
  • May 2018 (19)
  • June 2018 (17)
  • July 2018 (12)
  • August 2018 (7)
  • September 2018 (43)
  • October 2018 (29)
  • November 2018 (25)
  • December 2018 (17)
  • January 2019 (5)
  • February 2019 (11)
  • March 2019 (14)
  • May 2019 (2)
  • June 2019 (1)
  • July 2019 (8)
  • October 2019 (1)
  • December 2019 (4)
  • January 2020 (5)

JIKO LA USHAURI

Itambue Injili Ya Maji Na Roho. Ushiriki Ufalme wa Mungu, pata kitabu cha bure. Wasiliana nasi kwa sadikila65@gmail.com.

Tags

  • BIASHARA
  • HEKIMA ZA WAZEE
  • KUFURAHIA MAISHA
  • KUPATA BLOGU
  • MAHUSIANO
  • MAWASILIANO
  • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI
  • NJOZI
  • PATA BLOGU
  • SAIDIA HUDUMA HII
  • TAFAKARI NENO YA SIKU
  • TAFAKARI YA ROHO
  • UJASIRIAMALI
  • USHAURI
  • USWAZI TRICK

Kurasa

Labels

  • HEKIMA ZA WAZEE (24)
  • KUFURAHIA MAISHA (76)
  • KUPATA BLOGU (2)
  • MAHUSIANO (81)
  • MAWASILIANO (1)
  • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI (8)
  • NJOZI (94)
  • PATA BLOGU (3)
  • TAFAKARI YA ROHO (57)
  • UJASIRIAMALI (31)
  • USHAURI (78)
  • USWAZI TRICK (9)

Loading...

Fomu ya Anwani

Name

Email *

Message *

  • Napenda kusoma Biblia

About Me

Sadick Kilasi
View my complete profile
INJILI YA MAJI NA DAMU.

Search This Blog

Chapisho Lililoangaziwa

Alipambania Tumaini Lake Na Ndoto Yake Ikawa Kweli.

Kila mtu katika maisha ana tumaini lake. Msingi mkuu wa maisha ni tumaini. Nguvu kubwa ya maisha ni imani na mapito makuu ya maisha ni u...

Posts
Atom
Posts
Comments
Atom
Comments
INJILI YA KWELI NI INJILI YA MAJI NA ROHO. (MAJI, DAMU NA ROHO).
HII NDIYO KWELI YENYEWE.
YOHANA 19:34-35.

Copyright © JIKO LA USHAURI | Powered by Blogger
Design by Hardeep Asrani | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com | Distributed By Gooyaabi Templates