Kama ilivyo katika maisha ya kila siku, maisha ni utayari wa kuishi matuini sasa kwa Imani. Kilicho cha thamani zaidi ni utayari wa kuchukua hatua sasa maana hicho ndicho kitakupeleka katika matumaini yako.
Wakati wa kutembea, mguu mmoja ukiusindilia chini mwingine unakupa uafadhali kwa kuwa unakupa unafuu katika tembea, unakupa hamasa ya kuendelea mbele. Kwa hiyo, hatua moja moja ambazo tunapiga ni kama, kufa na kufufuka, unakanyaga hatua ya kwanza unaipa thamani, unendelea mbele, ya pili nayo unaipa thamani, unaendelea mbele.
Kila hatua utakayopiga inathamani kubwa sana katika maisha yako. Mshukuru Mungu kwa hatua ndogo ndogo unazopiga kwani hizi ndizi zinakupeleka katika kusudi na shabaha yako.
Mungu alipikuwa anaumba, alikuwa anathamini kila alichokuwa anakifanya, nasi lazima tumwige Mungu.
Ukawe na hatua nzuri, kila hatua kwako ni ya thamani sana, thamani kila hatua.
Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.
Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
0 comments:
Post a Comment