JIKO LA USHAURI

Itambue Injili Ya Maji Na Roho. Ushiriki Ufalme wa Mungu, pata kitabu cha bure. Wasiliana nasi kwa sadikila65@gmail.com.

  • NYUMBANI
  • KUFURAHIA MAISHA
    • ushauri
    • KUHUSU SISI
    • MAISHA NDANI YA YESU
  • MAWASILIANO
    • NAMBA YA SIMU
      • Sub 0687000768
      • Sub Child Category 2
      • facebook
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • NJOZI
  • SAIDIA HUDUMA HII
    • Childcare
    • Doctors
  • NYUMBANI
  • KUFURAHIA MAISHA
    • Stock
  • TAFAKARI YA ROHO
    • HEKIMA ZA WAZEE
    • Games
    • AFYA
      • Office
  • MAHUSIANO
    • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI
      • Sub Child Category 1
      • Sub Child Category 2
      • Sub Child Category 3
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • USHAURI
  • TAFAKARI NENO YA SIKU
    • Childcare
    • Doctors
  • PATA BLOGU

Monday, December 31, 2018

Jani Lilojiachilia.

 Sadick Kilasi     December 31, 2018     No comments   

Jani Lililojiashilia.

Mti hauwezi kulirudisha jani ambalo tayari limesha jiashilia na kudondoka kutoka kutika pale lilipokuwa.

Jani huusapoti mti kukua kwenda juu na kukua zaidi kwa kadili ambavyo lilikuwa tayari kuusapoti.

Ukweli ni kwamba, hatunauwezo wa kuwalipa watu ambao tayari wametufikisha hapa tulipofika. Hata tuwe na vipato gani hatuwezi kufanya chochote kwa wale ambao tayari wamefanya tufike hapa tulipofika.

Kila mtu kuna mtu amemsaidia kufikisha popote pale alipofika. Hatukufika tukiwa sisi wenyewe pekee yetu.  Na kwa sababu walisha tutendea hatuwezi kilipa gharama ambayo tayari tumefanyiwa. Nimefika hapa nilipofika ni kwa sababu watu wengine walikuja kama majani na kunisapoti licha ya jani kuwa ni sehemu ndoto ya mti lakini hao ndio walionipa chakula. Sijajua kama wasingekuwa wao leo ningekuwa wapi?

Haijarishi walikuja kwa picha gani ya ubaya ama uzuri lakini walinichonga hivi leo ninafurahia maisha.  Aliyekuja kwa ubaya ulibidi aje ili tuone na tuambatanishe na uzuri ili tupate nguvu. Aliyekuja kwa uzuri alikuja ili tuambatanishe na ubaya ili nguvu ipatikane. Basi, viungo haviwezi kufanya kazi bila joint ambayo sawa sawa na udhaifu.

Leo ninafurahia maisha kwa sababu walikuja kwangu kama zawadi yangu.  Naam, nimejiona kupitia wao.

Ninawashukuru nyinyi nyote ambao mlikuja kwangu na sasa hampo, kutokuwepo kwenu bado kunaniruhusu mimi nijione. Mungu awabariki. Majani yaliyodondoka nyinyi.

Basi, Adamu akasema, wewe ni mfupa wangu.

Nyinyi nyote ni zawadi yangu.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Friday, December 28, 2018

Je, Unaweza Kula Chakula Harafu Na Kufuta Mdomo Na Kusema Sijala Kabisa?

 Sadick Kilasi     December 28, 2018     No comments   

Je,  Waweza Kula Chakula Na Kufuta Mdomo Na Kusema Hujala?


Hivi ndivyo ambavyo tumezoea kuishi, kula chakula na kufuta mdomo na kusema kwamba mimi sijala kabisa.

Unafanya nini pale mtu anapokukosea? Wewe humsamehe? Kama unasubiri mtu akukosee harafu umsamehe ni sawa na kula chakula na kusema kwamba mimi sijala kabisa.

Kumsamehe mtu wakati ambao amekukosea ni sawa na kuweka jointi kwenye ubaya harafu ukasema sina ubaya ndani mwangu.

 Ufanye nini sasa wakati umekosewa?

Kuwa kama jua linalochomoza likipita giza linakimbia lenyewe. Samehe kabla ya kukosewa na hapo ndipo giza litakimbia lenyewe.

Kingiza giza na kulitoa ni jambo ambalo halileti maana. Vaa siraha za kiroho, uvae utayari miguuni mwako. Usitengeneze jointi.

Kila mwanadamu anamapungufu yake kwahiyo ukimtegemea binadamu ni sawa na kujiangamiza mwenyewe.

 Unaye Roho wa Mungu ambaye atakutia nguvu katika hili. Zaliwa upya katika hili uanze kuishi maisha tofauti.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Wednesday, December 26, 2018

Je! Andazi Laweza Kupita Mikononi Mwako Harafu Lisikuachie Kitu?

 Sadick Kilasi     December 26, 2018     No comments   

Je! Andazi Laweza Kupita Mikononi Mwako Harafu Lisikuachie Kitu?

Ni andazi hili hili ambalo kila mmoja analijua. Ukilishika tu na kuliachia litakuachia mafutamafuta na harufu kwenye mikono yako.

Kama andazi laweza kukuachia kitu kama hichi basi chochote kila ambacho unakuona kwa macho kwa kutaka ama kutokutaka lazima ubakiwe na chochote ndani mwako.

Na lazima uelewe kuwa chochote kile ambacho umekifanya ipo siku kitakuja kuoza na kutoa harufu. Kinapokuja kubadilika nguvu ili kifanye kazi nyingine. Vitabu unacyosoma ipo siku vitatoa harufu, mazoezi unayofanya ipo siku utaona kazi yake. Ulevi wa pombe ipo siku utaona kazi. Hakuna kitu ambacho hufanyika na kisibadilike na kinapobadilika inamaana kinakubadilisha.

Kila mbegu ambayo inapandwa kwako zingatia ni mbegu ipi ambayo unapaswa kuimwagilia ili baadae uvune mavuno ya kufaa. Ukweli ni kwamba, hatuwezi kukwepa mambo ambayo hatuyataki lakini tuna nafasi ya kuvipa vipaumbele vile tunavyohitaji vikue ili vitupe mabadiliko. Mwagilia mbegu njema, acha kumwagilia yasiyofaa.

Ardhi ni kubwa lakini sisi tupo sehemu ndogo tu. Basi, zingatia kidogo kinachokujenga kuliko kuzingatia ubaya mwingi unakuharibu na kukubomoa baadae. Tai hutazama kitu anachohitaji akiwa juu, huona ardhi kwa ukubwa lakini huzingatia kile anachohitaji.

Pata muda kutafakari ili mambo yatakapobadilika kwako yasiwe muujiza.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Monday, December 24, 2018

Je! Itapona?

 Sadick Kilasi     December 24, 2018     No comments   

Je! Itapona?

Ni miti ambayo ipo chini ya mti mkubwa wakati wa kuangamizwa mti mkubwa, je! hii inayojiburudisha chini yake itapona?

Wakati maalumu, wakati wa kutoweka mti mkubwa, hii ya chini itakuwaje?

Nakuuliza wewe ndugu Yangu, ni wapi ambapo unatumainia? Wewe wamtumania mwanadamu, wakati ukifika wa kuondoka huyo, wewe utakuwa katika hali gani?

Wewe ambayo matumaini yako yapo kwenye vitu, furaha yako hutegemea vitu, wakati vikiondoka utakuwa katika hali gani?

 Ndugu yangu, mtumainie Mwenyezi Mungu, jiweke chini ya kivuli chake, yeye ndiye mwanzo na mwisho. Kila kitu unachokiona kwa macho ukifika Wakati wa kuondoka vitaondoka. Hata sahani ikifika wakati wa kuondoka itaondoka.

Jiweke chini ya haki ya Mungu daima, ufurahie maisha daima. Alaaniwe amtumanie mwanadamu.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Dalili Za Mabadiliko.

 Sadick Kilasi     December 24, 2018     No comments   

Dalili Ya Kuelekea Mabadiliko Ya Asili.

Dalili ya tawi kukauka ni jani kudondoka. Dalili ya tawi kukauka ni shina kukauka. Dalili ya shina kukauka ni mizizi kukauka na dalili ya mizizi kukauka ni mti kukauka.

Maisha yalikosa furaha, hutawaliwa na dalili kama hizi. Tunakufa mara nyingi zaidi kabla hatujakifikia kifo kamili.

Kwa kadili unavyokubali kuumizwa na watu, hiyo ni dalili ya mapema zaidi ya kuonyesha kwamba utakufa mapema. Kwa kadili ambavyo unakubali vitu vya dunia hii vikutawale hiyo ni dalili ya kifo.

Usikubali fikra zako zikandamizwe na zitengeneze bwawa yaani mkandamizo wa fikra. Kabla nguo haijachafuka ifue mapema, ifurahie kesho leo. Wakati wote kuwa mtu wa kitiririka.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Sunday, December 23, 2018

Sala Ya Shukrani.

 Sadick Kilasi     December 23, 2018     No comments   

Sala Ya Shukrani.

Ee Mwenyezi Mungu, Mungu wetu, tunakushukuru kwa neema yako, asante kwa haki yako.

Tunakushukuru kwa hekima zako, maana kwa hekima zako sisi tunaishi. Umeifanya mbingu na nchi na ukaumba vyote vilivyomo ndani ya bahari na nchi kavu.

Kwa hekima zako uligawa mbingu na nchi ukagawa maji ya juu na chini. Ukaweka usiku na mchana, ukafanya jua na mwezi. Umetupa watoto wako gombo la chuo, kwa chuo hicho tupate kuzijua hekima zako.

Umejifua utukufu wako kupitia uumbaji wako, ukaweka kila kitu ndani ya chuo ili wana wako tupate kujifunza na kuona hekima zako humo.

Ni nani aliye mkuu kuliko Wewe? Umefanya makao ndani mwetu ili upate kutuongoza kwa usalama. Umewaweka watumishi wako ndani nchi ili watoto wako tusipate kupotea.

Umefanya mito kwa hekima zako na kuumba mti kwa ukuu wako. Ni nani ajuaye uhai wa sisimizi ulipo? Ni nani pekee yake ajuaye juu ya kesho? Basi, sisi watoto wako tutakutumainia wewe Mwenyezi Mungu, Mungu wetu. Tutayara matunda ya kesho leo maana tunalitia nanga tumaini letu kwako wewe uliye Mkuu mwenye enzi yote.

Tunasimama kwa ujasiri maana ndani mwetu umefanya makao na umeliweka neno ndani mwetu na chuo pia kipo kwaajili yetu.

Ukimbilieni usalama enyi watu wa dunia, jificheni ndani ya utukufu wake, maana Mwenyezi Mungu ndiye pumzi ya uhai wetu. Tuamanieni haki kwa Mwenyezi Mungu maana Mwanadamu ni kiumbe dhaifu sana.

Ee Mungu wetu, ndani yako usalama tele, ndani yako furaha tele.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Tuesday, December 18, 2018

Ni Wapo Wewe Mwisho Wa Pumzi Yako?

 Sadick Kilasi     December 18, 2018     No comments   

Ni Wapi Wewe Mwisho Wa Pumzi Yako?

Mwaka huu nilianza mwaka kwa kuishi falsafa ya mti, ninashukuru nilianza kwa kuelewa mambo mchache lakini mpaka sasa kuna sehemu kubwa ambayo nimejifunza kutoka kwenye mti.

Yapo mengi sana ambayo unaweza kujifunza kutoka kwenye mti. Binafsi mimi nimejifunza kwa kiasi changu namna ambavyo mti unaweza kunielewasha nini maana halisi ya maisha. Kabla ya mwaka huu kuisha nitakushirikisha mambo ambayo nimejifunza kutoka kwenye mti lakini pia kwenye kitabu cha Dunia Mama Haimtupi Mwanae, nimeeleza mengi juu ya mti.

Unajua tunapoishi hapa duniani ni kama tumetupwa kwenye sehemu ambayo hatuijui. Na hata wale ambao wametumika kutuleta duniani wameendelea kuishi bila kutafuta uhalisi kamili wa maisha. Japokuwa wapo wengi ambao wamefanya kwa kiasi kikubwa ila nasi hatuna budi kujua zaidi na kuendeleza pale ambapo wamefikia wenzetu. Vipo vitabu vitakatifu ambavyo ndiyo msingi wa haya yote. Lakini yote kwa yote kuweka mambo wazi wazi, sifa za Mungu ni kuficha hekima na mwanadamu kufichua hekima za Mungu.

Wapi Mwisho Wa Pumzi Yako?

Ushawahi kuiona miti, miti ambayo inakuwa chini ya miti mingine? Bila shaka ushawahi kuona.

Tunachoishi duniani ni kukua na kukua huwa kunategemea utupu yaani anga. Sasa anga lako likiwa jilani ni wazi kwamba  hakuta kuwa na uwezekano wa kukua, kwa sababu utazuiwa kwa juu ili usiendelee mbele. Miti inafokasi kuelekea juu angani, inakuwa na pumzi kubwa kwa sababu ya utupu mkubwa.

Katika maisha ya kawaida kunauwezekano mkubwa sana wa kuzuia anga na kufanya pumzi yako isifanye kazi vizuri. Na hii hufanyika katika ubongo wako namna ambavyo unaendesha maisha. Tamaa ya mambo ya dunia fedha, wanawake inaweza kukuzuia usipumue vizuri katika maisha yako, watu wanaokuzunguka wanaweza kukuzuia usipumue vizuri. Jiulize namna ambavyo unaendesha maisha yako, je, wewe ni mti ambao upo chini ya mti mwingine? Unapaswa kuona anga likiwa wazi juu na sio kuwa chini ya kivuli kingine. Tunakuwa katika hali nne, ambazo tunapaswa kupata wakati wote, kwanza, Maji, pili udongo ama kitu, tatu mwanga na nne hewa. Sasa hapa leo tunazungumzia mwanga na hewa.

Ukiwa chini ya kivuli cha mti mwingine huwezi kupata mwanga vizuri. Ukiwa chini ya mti mwingine huwezi kupumua vizuri kwa sababu unazuiwa na aliyeko juu yako.

Kutawala sio kumiliki, kutawala ni utambuzi, kumiliki ni kujimilikisha na kuweka mipaka. Kumiliki huletaa tamaa, tamaa ambayo inasababisha kuwa mtumwa wa hicho ambacho unamiliki. Unachomiliki kinakuzuia usione mbele yako wewe kitu ambacho husababisha pumzi yako isiwe huru.

Ndugu, tumebarikiwa tuwe baraka. Vitu ambavyo ni vya dunia hii huzuia pumzi yetu isifanye kazi vizuri. Chunguza kile ambacho kinakunya kila siku uamke na kufanya kazi, je? kinakupa furaha ama kinazuia pumzi yako tu! pumzi inapotoka vizuri inakufanya ujiachilie vizuri.

Elewa maisha ili uishi maisha, ni kipindi cha hakati hiki, tunaweza kujikuta tunajiingiza katika mambo ambayo sio kisudi letu kuishi.

Elewa na uishi, ishi na uelewe.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Sunday, December 16, 2018

Ulipo Hapo.

 Sadick Kilasi     December 16, 2018     No comments   

Ulipo Hapo.


Hivi ulishawahi kujiuliza ni kitu gani kwa siku hiyo ambayo ulikuwepo ama kwa leo hapo ulipo kinakufanya uwe hai? Je, vipi kuhusu uzima? Je, ushawahi kujiuliza ni kitu gani ambacho kinakufanya uwe mzima?

Kama bado hujawahi kujiuliza maswali haya kuna haja ya kujiuliza ili kujitafuta mwenyewe na kujielewa mwenyewe.

Jambo kubwa zaidi ambalo kila mmoja anahitaji na ni la muhimu ni kujikomboa mwenyewe kutoka katika kifungo cha vitu mbalimbali ambavyo vipo nje ya wewe.

Jambo la muhimu zaidi katika maisha ni kuelewa ni wapi ulipo na ni kitu gani kinakufanya uwe jinsi ulivyo. Anza kujitazama ndani ya hema yako ikisha toka nje ya kambi yako na uone ni kitu gani kinakufanya uwe hai na uwe na uzima ama ukose uzima.

Kabla ya kutaka unachotaka elewa ni kitu gani kinakuzunguka.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Friday, December 14, 2018

Kifanye Kivuli Kiwe Nyuma Yako.

 Sadick Kilasi     December 14, 2018     No comments   

Kifanye Kivuli Kiwe Nyuma  Yako.

Tukitanguliza mabaya katika mitazamo yetu kwenye mahusiano hatuwezi kuona uzuri wa mambo ambayo watu wanatufanyia.

Tukitanguliza kivuli katika mwendo kwenye maisha inatufanya tusione mambo mazuri ambayo Mungu katuandalia kwaajili yetu.

Siku zote unapoelekea kama mwanga upo mbele yako basi kivuli kitakuwa nyuma yako. Kama kivuli kikiwa mbele yako kitakuzuia usione vema. Wakati Mungu anafanya uumbaji kwanza alitanguliza nuru mbele kitu ambacho kilifanya giza liwe nyuma.

Hata macho yetu yanatufunza, kwa sababu rafiki wa macho ni mwanga, mwanga ukiwepo tunaona vyema. Nyuma yetu hakuna macho kwahiyo nyuma yetu ni giza hata kama kunamwanga.

Hata Nuhu wakati wa gharika ya maji alipomtanguliza kunguru kunguru hakurudi kwa sababu yeye asili yake ni mweusi lakini njiwa alienda na kurudi.

Kutanguliza ubaya katika maisha, ni bonge la kosa. Ni sawa na kufumba macho ili kujizuia usione mbele. Wakati umekosewa na mtu na ukatanguliza ubaya wa kumchukia ni sawa na kuwekewa sumu mbele yako, nawe unachukua harafu unainywa ukitegemea adui yako atadhurika.

Sio siri, hakuna kitu kizuri kama kuona wema kwenye kila jambo, maana ni sawa na kuchoma ubaya kwa wema.

Je, umeokosewa sana na mtu ambaye ulimwamini? Je, maisha yako hayana matumaini unahisi uchungu wakati wote?  Leo nataka uone, uone kwa kutumia ubongo na siyo macho. Uone namna gani ambavyo huwa inatanguliza mabaya mbele yako badala ya nuru ambayo ndiyo husafisha njia yako.

Unaweka kizuizi mbele harafu unataka kwenda mbele, je, hii inaleta maana? Ona wema kwenye kila jambo. Acha kutanguliza mabaya katika maisha yako. Mtumanie Mwenyezi Mungu yeye ndiye Mfalme wa nuru, jiweke chini ya haki yake, usihukumu kwani wewe sio Mungu.

Ni bora kuzingatia mazuri ambayo adui anakufanyia kuliko kuzingatia mabaya yake. Ni bora kuona mazuri ambayo mtu anafanya kuliko kukazana kuona mabaya.

Asante kwa kusoma makala hii, msambazie na mwingine. Kuchukua hatua ni muhimu zaidi na ndiomaana kuna Agano la kufanya tohara, (kuondoa govi).

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.

Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Wednesday, December 12, 2018

Kilichofichwa Hufichuliwa. Je! Mwizi Tutamchukuliaje?

 Sadick Kilasi     December 12, 2018     No comments   


Kilichofichwa Hufichuliwa.
Je! Mwizi Tumchukuliaje?

Madini yaliyojificha chini ya ardhi hutafutwa kwa juhudi kubwa, watu huchimbua kwa juhudi kubwa ili kuyafichua chini kabisa ya ardhi. Thamani yake ni kubwa kutokana na jinsi ambavyo yanapatikana kwa ugumu.

Wezi hutia juhudi kuhakikisha kwamba nyumba ambayo imezungushiwa fenzi kubwa na yenye ulinzi mkubwa, vitu ambavyo vipo ndani ya nyumba hiyo vinafichuliwa.

Maswali magumu humfanya anayejibu kuwa mwenye akili kwa sababu ya jibu kuwa limefichwa sana.

Sehemu za siri huwa na thamani zaidi kwa sababu zimefichwa sana.

Fedha ambazo hazipatikani kiurahisi hutafutwa na kila mtu na dhamani yake ni kubwa ukilinganisha na vitu vya kawaida.

Nimekuonyesha haya yote ili nikuonyeshe dhana ya vitu vilivyojificha namna ambavyo vinakuwa na thamani kubwa sana. Lakini je, mwizi anakosa?

Tunaishi katika ulimwengu ambao tunapenda kuhukumiana kwa kuona kwamba wengine ni wabaya baada ya kuibiwa na walio waibia, tunasahau kuwa msababishi wa kwanza katika wizi ni yule ambaye anaficha. Mpanzi mkubwa wa mbegu ya wizi ni yule ambaye anaogopa kuibiwa lakini pia mtendaji mkuu wa wizi ni yule ambaye anaiba.

Ukificha kitu unamfanya mwingine atamani, usingeficha asingetamani. Kwa sababu unaubinafsi wa kutaka kujilimbikizia mali na ndiomaana unaficha. Lakini na mwizi naye, kwa sababu ya ubinafsi unaiba, unaiba ili kujilimbikizia wewe pekee lakini pia unapenda giza na ndiomaana unaiba. Unaiba na unaenda kuficha tena, bora ungeiba na kuweka wazi wazi lakini umeiba na kuficha.

Sisi sote ni watoto wa Mungu, sisi sote tumeumbwa kwa mfano wa Mungu. Je! Tufanyaje katika hili?

USIHUKUMU, HURUMIA.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Tuesday, December 11, 2018

Mungu Mfalme Wa Haki.

 Sadick Kilasi     December 11, 2018     No comments   



Mungu ndiye Mfalme wa haki, mizani yake ni ya haki. Ni nani aliye kama Mungu?

Mwanadamu ipoumbwa mawazo yake yalikuwa ni kukusudia uovu tu ndani ya moyo wake Mungu akaleta gharika ya maji lakini baadae Mungu akasema, sitaiangamiza tena dunia kwa maji kwa sababu mwadamu tangu utoto wake hujiwazia uovu tu. Ndugu, tupo tayari kufanya maamuzi kama haya ili tuushinde uovu kwa wema? Tumwige Mungu japo sisi si wakamirifu, tujitahidi katika hili.

Wakati Esau alipokuwa anataka kuchukua mibaraka yote kwa baba yake Isaka dhidi ya ndugu yake Yakobo, Mungu alifanya kwa haki, akambariki Yakobo kupitia kwa baba yake Isaka kwa sababu Isaka alikuwa kipofu  na baadae akambariki Esau wote wakawa watu wenye mali nyingi na matajiri. Tusifanye kwa upendeleo kwa sababu fulani bali tunapaswa kufanya kwa sababu tunapaswa kufanya. Tujitaidi katika hili.

Wakati Raheli alipokuwa mzuri machoni pa Yakobo na Lea alikuwa dhaifu, Mungu alimtia utasa kwa muda Raheli na kumjalia Lea watoto sita na mwisho akamjali Raheli watoto wawili. Mungu hufanya kwa haki, hakuna mwanadamu ambaye aweza kutambua mahesabu yake.

Ndugu yangu, inawezekana upo katika hali ambayo ipo nje ya uwezo wako, unapitia magumu kiasi ambacho kinakufanya ukate tamaa, usijiweke chini ya haki yako wewe mwenyewe binafsi bali jiweke chini ya haki ya Mungu. Mungu hufanya vitu vidhaifu kuwa vyenye   nguvu. Mungu humjalia kila mtu ambaye yupo tayari kumtumania .

Machoni pa mwanadamu kila kitu kinaweza kuwa sawa lakini machoni pa Mungu mambo huwa tofauti.

Yusuph aliyezaliwa wakati wa uzee kwa Raheli akiwa mtoto ambaye alikuwa na ndugu mmoja kwa mama  alipitia wakati mgumu lakini baadae alikuja kuwaokoa nduguze, huo nao ulikuwa mpango wa Mungu. Jina la Yusuph lilitukuka kwa sababu aliwaokoa ndugu zake, je! ni nani ni sawa mbele za Mungu? Ndugu zake pia wasingeokoka bila Yusuph.

Sisi wanadamu ni kitu kimoja, kila mmoja ni kwaajili ya mwingine na si kwaajili ya haki yake binafsi. Anayejua ni anajua kwa sababu ya yule asiyejua. Sisi sote kitu kimoja na tujiweke chini ya haki ya Mungu na tumwachie Mungu yeye pekee ahukumu kwa haki.

Asante.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Monday, December 10, 2018

Bubujiko lisilo isha.

 Sadick Kilasi     December 10, 2018     No comments   

Bubujiko  Lisilo Isha.

Akili ni nywele kila mtu ana zake. Unapotumia akili yako kama maarifa kwenye maisha yako ni kama nywele, hukua bila kuwa na kikomo na hata ukikata bado zitaota tu kwa sababu shina bado lipo. Hili ni bubujiko lisilo isha.

Unapotumia akili kwenye maisha kama maarifa ni kama kumimina mafuta ndani ya chombo hayaishi kirahisi. Hili nalo ni bubujiko lisilo isha.


Unapotumia akili yako kama maarifa kwenye maisha, ni kama chemichemi ya maji ambayo hububujika wakati wote. Hili nalo ni bubujiko lisilo isha.

Unapotumia akili yako kama maarifa kwenye maisha, ni kama mti kukua kuelekea mawinguni. Hili nalo ni bubujiko lisilo isha.

Bubujiko lisilo isha ni matumizi ya akili kwenye mbegu ndogo ya kitu na kuifanya kuwa kubwa zaidi na zaidi na zaidi. Bubujisha kila kitu kwenye maisha yako ili kiwe zaidi ya hivyo kilivyo.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Sunday, December 9, 2018

Wakati Wa Kujitokeza.

 Sadick Kilasi     December 09, 2018     No comments   




Tumeimaliza program yetu ya kuishi maisha yenye maana jumapili ya jana. Binafsi nimejifunza mengi namna ambavyo nililivyo na jinsi ninavyochukulia mambo. Natumai hata wewe kuna jipya umejifunza, kama tumekuwa wote katika program hii basi yawezekana umebaki kama ulivyo ama umekwenda mbele hatua kidogo. Kama umekwenda mbele hatua kidogo, hongera sana lakini kama hakuna matokeo yoyote ambayo hujapata bado hujachelewa unaweza kufanya lolote nangu sasa ili kuondoka katika hali hiyo ya mgando.

Tuna safari ndefu sana ambayo tunapaswa kwenda ili kuhakikisha injili inafika mbali. Tumeshiriki wiki hii ya kuishi maisha yenye maana tukifokasi katika tabia mbalimbali kwa wiki tofauti sasa ni wakati wa KUJITOKEZA.

Ndugu yangu, ukienda kulala usiku, usipotoka ndani ya chumba chako watu watajua umelala hata kama umeamka. Mbegu iliyopandwa chini ya ardhi isipojitokeza juu itaonekana imekufa hata kama haijafa. Martin Luther King Jr anasema, ukimya wa wapendwa wetu unaumiza sana kuliko kelele za maadui zetu. Albert Einstein anasema, dunia si mbaya kwa sababu ya watu wabaya ila ni mbaya kwa sababu ya watu wazuri ambao wamekaa kimya.

Wewe ni shaidi katika ulimwengu wa sasa kwa sababu sisi sote tunaishi katika ulimwengu huu. Matunda ya ulimwengu huu ni mabovu hayafai hata kuliwa. Tunasababu ya kuchukua hatua mimi na wewe kuhakikisha nuru inang'aa ulimwenguni.  Sisi ambao tunabahatika kusoma mafunzo mbalimbali ya kujenga tunapaswa kuenda hatua ya ziada, tunapaswa kuwa nuru ya ulimwengu.

Usifikiri wakati wote kuwa chini ya kivuli cha mti mkubwa eti kwa sababu muda wako haujafika bado.  Ukiangalia miti ambayo huwa inakuwa chini ya vivuli vya miti mikubwa huwa inaonekana kustawi wakati wote lakini huwa haifiki mbali kwa sababu haiwezi kujitegemea yenyewe. Badala ya kulishwa kila siku maarifa kanisani na kwenyeajukwaa mbalimbali ni wakati kufanyia kazi ambayo unajifunza kila siku. Usipokuwa makini kama ukijifunza kitu na usipokitendea kazi unakuwa mlevi, mlevi wa maarifa kitu ambacho kitakufanya kuona kwamba kila siku unahitaji maarifa zaidi ili kufanya jambo kumbe unapaswa kuanzia na pale ulipo. Kithamini kwanza ulichokipata ikisha kichofuata kiwe na thamani zaidi.

Ili kuweza kutumika na Mungu si jambo la ajabu sana ni jambo ambalo tunapaswa kukusudia kama tulivyokuwa tunakusudia kwenye mwezi wetu wa kuishi maisha yenye maana. Tunachopaswa kufanya ni kumrusu Mungu kutenda kazi ndani mwetu. Sisi tunafokasi katika matunda yake.
-UPENDO
-FURAHA
-UVUMILIVU
-UTU WEMA
-FADHILI
-UAMINIFU
-UPOLE na
-KIASI.

Tumesha jifunza namna ya kuendesha tabia mbalimbali kupitia program yetu ya mwezi na sasa hizi ndizo tabia ambazo ni matunda ya Roho wa Mungu ndani mwetu, inamaana kama kila siku tukiamka na kukusudia kuishi tabia hizi tutakuwa tunaishi kwa kutumika na Mungu.

Andika hizi tabia na uweke mahala peupe na kupitia kila siku. Ni mtu yeyote ambaye anapaswa kufanya hivi haijarishi ni mtumishi ama si mtumishi. Ikiwa tu unamwamini Yesu utapikea Roho yake na kwa mwongozo wake utaonyesha matunda hayo.

Jitokeze ili kuirutubisha dunia. Hata kama hupendi namna ambavyo dunia inafanya usipojitokeza hakuna lolote ambalo linaweza kubadilika. Siku zote mambo ya Mungu yapo automatic, mwanadamu ndiye haaminiki na ndiomaana meno ya juu hachezi lakini ya chini yanachezacheza. Ukitoka nje utakutana na jua. Chochote unachohitaji unahitaji kukiendea na kukifanya.

Anza sasa huu ndio wakati wako.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Sababu Nne (4) Kwanini Unapaswa Kusamehe Watu.

 Sadick Kilasi     December 09, 2018     No comments   



Moja ya kitu kikubwa zaidi ambacho nimekuwa napenda kuona mtu anajikwamua na kwenda hatua ya juu zaidi katika maisha yake kwenye mahusiano ni jinsi ya kuachilia msamaha kwa wale ambao wanamwumiza. Jinsi ambavyo unaweza kujiachilia wakati mgumu na kutokupoteza furaha yako hata kwenye jambo ambalo isingewezekana kabisa kuachilia msamaha.

Na kama tunavyojua, kinachotutesa watu wengi ni hali ya ubinafsi iliyopo ndani mwetu na hii ndio ilisababisha Kaini amwue ndugu yake, ilisababisha Mafarisayo na waalimu wa sheria wamkatae Yesu, na hii pia ndio inasababisha watu sasa hivi tuishi kama tunavyoishi. Kama kuna eneo ambalo halipo sawa basi chanzo kikubwa ni ubinafsi.

Ili kuishi maisha ya furaha na kutokurusu kuumizwa na wengine ipo sababu ya kujifunza namna ya kuachilia msamaha. Kuna kitabu ambacho Deo Kessy amekiandika kinaweza kukusaidia zaidi jinsi ya kuachilia msamaha, wasiliana naye kwa 0717101505. Jipatie kitabu hichi ni kizuri sana.

Lakini leo napenda tuangalie, kwanini unapaswa kuwasamehe watu walio kukosea. Unajua kwenye hii dunia utambuzi ndio unatufanya tuendeshe maisha na ndiomaana ni muhimu kujifunza hata jinsi ya kuwasamehe watu. Mtu hawezi kusamehe asipokuwa na Roho njema ambayo ni Roho ya Kristo ambayo tunaipata baada ya kujifunza neno la Mungu na kuua kabisa tabia za nafsi na tunabaki tukiendeshwa na Roho badala ya kuishi kawaida na kutafsiri mambo kimwili.

Sababu Kwanini Usamehe.


1.Uwepo wako mbele ya macho ya huyo ambaye amekukosea ni sababu ambayo imesababisha hiyo migogoro. Ni rahisi kuona makosa kwa wengine lakini ni ngumu kuona makosa yetu. Kila mgogoro unapokuja huwa unakuja kwa chanzo, kuna mbegu ambayo ilipandwa. Ikiwa upo katika eneo la migogoro basi hata wewe umeingilia ufalme wa mwingine. Usingekuwepo hakuna jambo ambalo lingetokea. Kuwa tayari kujiadhibu badala ya kuwasingizia wengine kwenye kila kitu.


2.Mbegu ya chuki inatoka wapi? Kama ukiona mwingine amekukisea, jiulize, nimejuaje kwamba amenikosea kama sio tafsiri ya uovu uliopo ndani mwangu? Mtu anayeweza kuonyesha uovu naye ni mwovu. Kila mtu anamakosa yake ambayo alishakosea, je! ulishawahi kujiuliza ni kwa kiasi gani yule uliye mkosea aliumia kiasi gani hapo nyuma? Kila mtu hupokea jambo kwa uzito wake. Hata kama uliomba msamaha, huwezi jua kovu ambalo umeliacha linamwumiza kiasi gani. Achilia msamaha kwa Sababu unajua kukosewa kwa sababu hata wewe umewakosea watu. Watoto wadogo hawana uovu ndani mwao na ndio maana utakuta mtoto mdogo haoni ubaya wowote, anapofanya jambo yeye hufanya tu, ila wanajua uovu utasikia huyu, mwizi, huyu ni mbaya, huyu ni malaya na mengine kama hayo. Usihukumu penda huruma.

3. Kila mtu yupo bize na hema yake. Kila mtu anamapungufu yake, kila mtu yupo bize na kile ambacho ataka kuwaza. Huwezi kumlazimisha mtu muendane kimawazo ni jambo ambalo haliwezekana. Kila mtu anamtazamo wake juu ya mambo fulani na ndio maana tumesema huwezi kusamehe kama hujui nini maana ya msamaha na kama huna Roho ya Mungu ndani mwako. Ikiwa mtu hajajifunza juu ya msamaha hawezi kusamehe kwa Sababu hana elimu hiyo. Hatuwasamehe wengine kwa sababu wametukosea tunawasamehe wengine ili tujisamehe wenyewe. Hakuna mtu anayeweza kumsame mwingine isipokuwa waweza kujisamehe mwenyewe. Kutokujisamehe mwenyewe ni sawa na kunywa sumu mwenyewe na kutegemea mwingine atakufa kwa sumu uliyokunywa wewe. Kwa hiyo anza kubadili mtazamo, toka nje ya hema yako na ndipo ulalamike mvua. Wakati mwingine unapaswa kujua nini mwenzako anafikiria, ingia ndani ya hema yake ili ujue ni kitu gani hakipo sawa.

4.Mtu siyo kosa, yeye ni tofauti na kosa. Mara nyingi kinachotuumiza ni kile ambacho tayari kimefanywa na wala si kile ambacho kinafanywa au ambacho hakijafanywa. Watu huwa wanabadilika, watu huwa wanajirekebisha. Sisi ni watu ambao tunamapungufu lakini sifa ya mwanadamu ni kwamba anauwezo mkubwa wa kubadilika na kukua kwa chochote kile. Ukiona unazingitia sana mambo ambayo umefanyiwa inamaana umekosa uwepo, huishi sasa hivi, mwili wako upo hapo lakini fikira zako bado zimetekwa na tukio la nyuma. Kunautofauti mkubwa kati ya kosa na mtu, kunautofauti mkubwa kati mtu na anachokifanya. Jitaidi kuishi sasa na kuyapa thamani mambo ambayo unafanya saizi.


Kujiondoa katika kila kifungo inahitaji utayari, utayari wa kufanya. Nimekupa harufu ya matumaini ya kuwasamehe watu ili uishi maisha ya furaha, unahitaji kufanya mchakato nawe utashiba amani na furaha.

Tafakari;
6:1, Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lolote, ninyi mlio wa Roho  mrejezeni upya mtu huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe.

Ndugu yangu, nisaidie kusambaza makala hii ili iwafikie wengi zaidi. Asante.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.


Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Saturday, December 8, 2018

Katika Wiki Ya Hamasa, Nakuandikia Wewe Uliye Mkubwa.

 Sadick Kilasi     December 08, 2018     No comments   



Mara nyingi tumezoea kufanya vitu kimazoea. Kama ni kusoma tumekuwa tukisoma kimazoea kama watu ambao tunajua kusoma. Kama ni kufanya jambo lolote tunafanya kama watu ambao tunajua. Na hii siku zote nimekuwa nikisema, kujiaminisha kuwa kivuli ndio uhalisi wenyewe. Tunatembea kama vivuli tukiwa tunajua ndio ukweli kumbe ni kivuli cha ukweli.

Na kwa hili nimeona nikuandikie wewe uliye mkubwa, ambaye unajiona mkubwa, unayetembea na vivuli ukijua ndio ukweli.

Inawezekana wewe ni mchezaji wa mchezo fulani, inawezekana wewe ni mwandishi kama mimi, inawezekana wewe ni msomaji wa vitabu, lakini yote kwa ujumla nataka nikwambie unaweza kufanya zaidi ya unavofanya saizi. Hakuna mipaka kwenye kufanya. Watu wazima sisi ambao tunajiita watu wazima ndio tumekuwa tunajidanganya sana, tukiwaangalia watoto wadogo tunaona ni kama sisi hatuwezi kukua zaidi na tumefika mwisho na hata watoto wetu wanapaswa kufikia angalau viwango vyetu, wakue kama sisi. Tunatengeneza mipaka ambayo inawaandaa watoto kuwa kama sisi, tunataka waige vivuli vyetu vya mambo. Mwisho utakuta ukoo ama jamii fulani wanafanana kwenye kila kitu, kimafanikio na hata kifikra. Yote hii ni kwa sababu ya watu wanaojiona wakubwa, watu ambao kufanya kila kitu kwa mazoea na kuona kana kwamba haiwezekani kufanya zaidi ama kwa njia ya tofauti na jinsi ambavyo hufanya.

Tunaweza kuwaangali watoto wadogo wanapokuwa huwa wanakuwaje?  Na hivi ndivyo inavyokuwa, inapaswa tuwe kama watoto wadogo, kuchukua hatari kama watoto wadogo, kupenda kujifunza kama watoto wadogo, kuwa watu wa haraka kuachilia msamaha kama watoto wadogo, ukishindwa kurudia kufanya kama watoto wadogo, unapaswa kukua kama watoto wadogo, kila kitu ambacho unakifanya fanya kama mtoto mdogo. Tunasafari ndefu sana, safari yetu ni kama kutoka chini ya ardhi kwenda mawinguni kwa miguu.

Usijione kama wewe ni mtu ambaye unaweza kila kitu, ujione kana kwamba unahitaji kufanya kitu bora. Usitundike kitu kwenye ubongo wako katika kufanya kitu. Kama nikikisea nikijua kwamba nimekosea na nikatubu basi ni bora kuliko kutokukosea harafu nikabaki katika hali ya kawaida na nisiadhiri chochote ama kuleta jambo jipya. Kufanya kawaida ni sawa na kubaki kawaida. Kawaida ni kitu ambacho tayari kimekufa.

Kama ni mtu mkubwa na unajiona kama ni mtu mkubwa acha kufikiri kimipaka. Anza kufikiri tofauti. Kile ambacho unapaswa kuishi tangu sasa ni kuipa thamani sasa kwa kufanya sasa kwa ubora wa hali ya juu.

Yesu Kristo alisema, msipoongoka na kuwa kama watoto wadogo, hamwezi kuuuona ufalme wa Mungu.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Monday, December 3, 2018

Katika Wiki Ya Hamasa

 Sadick Kilasi     December 03, 2018     No comments   




Kuna wakati mazingira yanayokuzunguka yanaweza kukufanya ukashusha hamasa yako na kujikuta upo katika hali ya kujiona huwezi lolote. Kuna wakati maneno ya mtu yanaweza kukufanya ukajihisi wewe si mtu wa kuzinguzia vitu vikubwa. Kuna wakati ukikumbuka mapito yako yanaweza kukufanya ukashusha hamasa yako ya kusonga mbele, baada ya kukumbuka tu udhaifu wako wa hapo nyuma.

 Usikubali, usikubali ndugu yangu, usikubali mazingira, maneno ya watu, kumbukumbu mbaya zikutoe katika mstari wa hamasa. Adui anakuja kiujanja kukuonea kiujanja lazima uwe mjanja. Ulicho kidhamiria hakikisha kinakupa matokeo makubwa hata kama unahisi nguvu hasi inaingia kwako. Ushinde ubaya kwa wema.


Wako akina Yezebeli mpaka sasa ambao hutishia maisha yako. Usikibali kukaa kwenye mti wa mretemu kama Elia ukajionea huruma mwenyewe.


Shetani hutumia watu kama alivyomtumia Petro kufanya Yesu asifikie malengo yake. Mara nyingine watu hutumiwa ili kukukatisha tamaa lakini wewe usikubali, baki katika njia kuu.

Sifa ya kwanza ya shetani ni mwelevu, sasa wewe kuwa mjanja zaidi, usikubali kudanganywa.

Tia juhudi, usijikinai, ushindi upo kwaajili yako.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg

Saturday, December 1, 2018

Katika Wiki Ya Kukua, Unahitaji Kupalilia.

 Sadick Kilasi     December 01, 2018     NJOZI     No comments   



Mpanzi anayepanda mbegu na akaacha ikue yenyewe bila yeye kupalilia kuna uwezekano mkubwa wa kupoteza tumaini lake ambalo alikuwa anatumainia kuvuna.

Inahitaji kupalilia, ndiyo palilia kile ambacho unahitaji kikupe na kilete mafanikio yako. Kile ambacho unataka kikupe matokeo makubwa na si ya kawaida. Unahitaji kupalilia.

Wakulima wa mahindi hupalilia mahindi ili yakue katika kiwango kikubwa ambacho wao wanataka kuvuna. Huweka mbolea na madawa na kila kitu ambacho kitafanya mazao yakue katika ubora na kuleta mavuno bora. Chochote kile ambacho unapenda kikupe matokeo makubwa unahitaji kupalilia.

Mungu alipotumba hakutuacha hivi hivi bali bado anaendelea kutupalilia kupitia neno lake na Roho Mtakatifu. Anataka tukue tufike kiwango cha juu kabisa na tulete matokeo ya juu kabisa duniani.

Palilia ndoto yako, wekeza muda katika ndoto yako, ongeza maarifa katika ndoto yako, palilia mahusiano yako, weka muda katika kuhusiano na watu, na uweke kipaumbele cha muda katika hilo.

Mbegu yoyote ile ambayo umeipanda na unataka ikue na ifike katika viwango vya juu, Unahitaji kupalilia, unapalilia kwa kuongeza viungo katika mbegu yako. Chochote kile ambacho unataka kiufikie upana mkubwa zaidi kinahitaji manjonjo ndani yake, asili ya dunia inaruhusu hivo, na ndivyo mambo yalivyo.

Kama ukipanda mbegu na ukaondoka zako bila kupalilia kuna hatari ya kuvuna magugu ama kuvuna kwa uchache ambao hukutarajia.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
Read More
  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg
Newer Posts Older Posts Home

Search This Blog

Translate

Total Pageviews

About Me

Sadick Kilasi
View my complete profile

Followers

Kurasa

  • Nyumbani
  • Saidia Huduma Hii Kuwafikia Wengi Zaidi.

Search This Blog

Blog Archive

  • ►  2020 (5)
    • ►  January (5)
  • ►  2019 (46)
    • ►  December (4)
    • ►  October (1)
    • ►  July (8)
    • ►  June (1)
    • ►  May (2)
    • ►  March (14)
    • ►  February (11)
    • ►  January (5)
  • ▼  2018 (275)
    • ▼  December (17)
      • Jani Lilojiachilia.
      • Je, Unaweza Kula Chakula Harafu Na Kufuta Mdomo Na...
      • Je! Andazi Laweza Kupita Mikononi Mwako Harafu Lis...
      • Je! Itapona?
      • Dalili Za Mabadiliko.
      • Sala Ya Shukrani.
      • Ni Wapo Wewe Mwisho Wa Pumzi Yako?
      • Ulipo Hapo.
      • Kifanye Kivuli Kiwe Nyuma Yako.
      • Kilichofichwa Hufichuliwa. Je! Mwizi Tutamchukuliaje?
      • Mungu Mfalme Wa Haki.
      • Bubujiko lisilo isha.
      • Wakati Wa Kujitokeza.
      • Sababu Nne (4) Kwanini Unapaswa Kusamehe Watu.
      • Katika Wiki Ya Hamasa, Nakuandikia Wewe Uliye Mkubwa.
      • Katika Wiki Ya Hamasa
      • Katika Wiki Ya Kukua, Unahitaji Kupalilia.
    • ►  November (25)
    • ►  October (29)
    • ►  September (43)
    • ►  August (7)
    • ►  July (12)
    • ►  June (17)
    • ►  May (19)
    • ►  April (31)
    • ►  March (33)
    • ►  February (25)
    • ►  January (17)
  • ►  2017 (58)
    • ►  December (16)
    • ►  November (22)
    • ►  October (2)
    • ►  September (11)
    • ►  August (4)
    • ►  July (3)
Sadick Kilasi. Powered by Blogger.

Jisajili kwa kujiunga nasi hapa

Posts
Atom
Posts
All Comments
Atom
All Comments
Maisha yenye maana ni yale maisha ambayo mhusika atambua nini kusudi lake la kuwepo hapa duniani. Hapandipo muhusika anapo kaa katika nafasi yake na kuwasha nuru katika sehemu aliopo kutokana uhusika wake. Jiunge na mtandao huu kupata maarifa zaidi na kwa ushirikiano mwingine kwa ujumla.

Kurasa

  • Nyumbani
  • TAFAKARI ROHO
  • Saidia Huduma Hii Kuwafikia Wengi Zaidi.

JIUNGE NASI SASA KWA KUJAZA FOMU HAPO CHINI


ANZA KUFURAHIA MAISHA NDANI YA YESU, MPOKEE ROHO MTAKATIFU KWA INJILI YA MAJI NA DAMU 0687000768

Zilizosomwa sana

  • Chukua hizi hapa nukuu za Malcolm x mtu ambaye anawavutia wengi sana.
    Ni siku nyingine tena ambayo ni mpya kabisa, karibu tena katika blogu hii ya JIKO LA USHAURI ambapo mimi mpendwa wako nimekuwa naingia jikon...
  • Ubatizo Wa Maji Mengi Na Ubatizo Wa Maji Machache, Upi Ni Sahihi?
    Ubatizo wa Maji Mengi Na Maji Machache. Kumekuwa na migongano kwa muda mrefu sana juu ya ubatizo, kati ya ubatizo wa maji mengi na ule uba...
  • Falsafa Za Maisha, Yaani Neno La Maarifa.
    Falsafa Za Maisha, Yaani Neno La Maarifa. Habari mpendwa? Natumai wewe unayesoma hapa umzima.   Karibu tena katika Falsafa Za Maisha. Ku...

Blog Archive

  • July 2017 (3)
  • August 2017 (4)
  • September 2017 (11)
  • October 2017 (2)
  • November 2017 (22)
  • December 2017 (16)
  • January 2018 (17)
  • February 2018 (25)
  • March 2018 (33)
  • April 2018 (31)
  • May 2018 (19)
  • June 2018 (17)
  • July 2018 (12)
  • August 2018 (7)
  • September 2018 (43)
  • October 2018 (29)
  • November 2018 (25)
  • December 2018 (17)
  • January 2019 (5)
  • February 2019 (11)
  • March 2019 (14)
  • May 2019 (2)
  • June 2019 (1)
  • July 2019 (8)
  • October 2019 (1)
  • December 2019 (4)
  • January 2020 (5)

JIKO LA USHAURI

Itambue Injili Ya Maji Na Roho. Ushiriki Ufalme wa Mungu, pata kitabu cha bure. Wasiliana nasi kwa sadikila65@gmail.com.

Tags

  • BIASHARA
  • HEKIMA ZA WAZEE
  • KUFURAHIA MAISHA
  • KUPATA BLOGU
  • MAHUSIANO
  • MAWASILIANO
  • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI
  • NJOZI
  • PATA BLOGU
  • SAIDIA HUDUMA HII
  • TAFAKARI NENO YA SIKU
  • TAFAKARI YA ROHO
  • UJASIRIAMALI
  • USHAURI
  • USWAZI TRICK

Kurasa

Labels

  • HEKIMA ZA WAZEE (24)
  • KUFURAHIA MAISHA (76)
  • KUPATA BLOGU (2)
  • MAHUSIANO (81)
  • MAWASILIANO (1)
  • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI (8)
  • NJOZI (94)
  • PATA BLOGU (3)
  • TAFAKARI YA ROHO (57)
  • UJASIRIAMALI (31)
  • USHAURI (78)
  • USWAZI TRICK (9)

Loading...

Fomu ya Anwani

Name

Email *

Message *

  • Napenda kusoma Biblia

About Me

Sadick Kilasi
View my complete profile
INJILI YA MAJI NA DAMU.

Search This Blog

Chapisho Lililoangaziwa

Alipambania Tumaini Lake Na Ndoto Yake Ikawa Kweli.

Kila mtu katika maisha ana tumaini lake. Msingi mkuu wa maisha ni tumaini. Nguvu kubwa ya maisha ni imani na mapito makuu ya maisha ni u...

Posts
Atom
Posts
All Comments
Atom
All Comments
INJILI YA KWELI NI INJILI YA MAJI NA ROHO. (MAJI, DAMU NA ROHO).
HII NDIYO KWELI YENYEWE.
YOHANA 19:34-35.

Copyright © JIKO LA USHAURI | Powered by Blogger
Design by Hardeep Asrani | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com | Distributed By Gooyaabi Templates