JIKO LA USHAURI

Itambue Injili Ya Maji Na Roho. Ushiriki Ufalme wa Mungu, pata kitabu cha bure. Wasiliana nasi kwa sadikila65@gmail.com.

  • NYUMBANI
  • KUFURAHIA MAISHA
    • ushauri
    • KUHUSU SISI
    • MAISHA NDANI YA YESU
  • MAWASILIANO
    • NAMBA YA SIMU
      • Sub 0687000768
      • Sub Child Category 2
      • facebook
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • NJOZI
  • SAIDIA HUDUMA HII
    • Childcare
    • Doctors
  • NYUMBANI
  • KUFURAHIA MAISHA
    • Stock
  • TAFAKARI YA ROHO
    • HEKIMA ZA WAZEE
    • Games
    • AFYA
      • Office
  • MAHUSIANO
    • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI
      • Sub Child Category 1
      • Sub Child Category 2
      • Sub Child Category 3
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • USHAURI
  • TAFAKARI NENO YA SIKU
    • Childcare
    • Doctors
  • PATA BLOGU

Thursday, August 30, 2018

Nguvu Mbili Ambazo Hutawala Katika Ulimwengu Huu.

 Sadick Kilasi     August 30, 2018     KUFURAHIA MAISHA, MAHUSIANO, TAFAKARI YA ROHO     No comments   

Katika dunia hii ambayo tunaishi kuna nguvu kuu mbili ambazo watu hurusu ziwatawale katika maisha yao.  Yaani kama una hii basi nyingine utakuwa huna. Lazima mojawapo uwenayo. Nguvu hizi huwatawala kila mmoja katika maisha. Nguvu zenyewe ni;
-FURAHA NA
-WOGA.

Nguvu hizi humtawala kila mmoja kutokana na mazingira ambayo mhusika anayaishi na namna alivyochagua mwenyewe kuishi. Furaha ni nguvu ambayo inamwelekeo chanya. Furaha ni mwanga katika maisha ya mtu lakini Woga ni nguvu yenye mwelekeo hasi katika maisha. Woga ni giza nene katika maisha ya mtu.

Nguvu zote hizi mbili nimekwambia hapo juu humtawala mtu kutokana na maisha yake anavyoyaendesha. Watu wengi wamejikuta katika hali tofauti tofauti kutokana na maisha yao. Wengi tumejikuta tunafanya machaguo bila kutambua kwamba kwa sasa tunafanya machaguo ya kuleta woga au furaha katika maisha yetu. Maana yeyote ambaye amechagua maisha ya kuishi katika maisha ya kiasi hamna woga ndani yake.

Tunapitia katika hali hizi zote ili mradi tu tujifunze kuishi maisha yenye maana lakini bahati mbaya wengi huwa hatutambui nyakati na wakati maalumu kwa sababu tumekosa uwepo ndani mwetu. Mungu hutumia nyakati hizi tofauti ili tutambue utofauti wa mambo katika maisha ili tuishi kwa shukrani.


Kumbukumbu la Torati 8:1-11, Amri hii ninayokuamuru leo mtaishika na kutenda, mpate kuishi na kuongezeka, na kuingia katika nchi ile ambayo Bwana aliwaapia baba zenu; nanyi mtaimiliki. Nawe utaikumbuka njia ile yote Bwana Mungu wako alikuongoza miaka hii arobaini katika jangwa, ili akutweze, kukujaribu kuyajua yaliyo moyoni mwako, kwamba utashika amri zake, au sivyo. Akakutweza, akakuacha uone nja, akakulisha kwa mana, usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua; apate kukujulisha ya kuwa mwanadamu haishi kwa mkate tu, bali huishi kwa kila litokalo katika kinywa cha Bwana. Mavazi yako hayakuchakaa, wala mguu wako haukuvimba, miaka hiyo arobaini. Nawe fikiri moyoni mwako, ya kuwa kama vile baba amrudivyo mwanawe, ndivyo Bwana, Mungu wako, akurudivyo. Nawe uzishike amri za Bwana, Mungu wako, upate kwenda katika njia zake, na kumcha. Kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yuakuingiza katika nchi nzuri, nchi yenye vijito vya maji, na chemichemi, na visima, vibubujikavyo katika mabonde na milima, nchi ya ngano na shairi, na mizabibu, na mitini, na mikomamanga; nchi ya mizeituni yenye mafuta, na asali; nchi utakayokula mikate humo, pasina shida, hutapungukiwa na kitu ndani yake; nchi ambayo mawe yake ni chuma, na milima yake yafukuka shaba. Nawe utakula ushibe, utamshukuru Bwana, Mungu wako kwa nchi nzuri aliyokupa. Jihadhari, usije ukamsahau BWANA, Mungu wako, kwa kutozishika amri zake, ninazokuamuru leo.

Woga hautoki kwa Mungu, bali woga ni zao la hofu, na hofu ni tahadhari ya kuwa makini. Katika nyakati hizi zote ambazo Mungu ametumbia, mtu haishi kwa mkate tu, bali na kwa neno la Mungu, kuna wakati ambapo utajikuta katika jangwa, nchi ya ukame, nchi ambayo mambo ni magumu kwa macho ya uanadamu yaani tafsiri ya mwanadamu. Lakini wakati huu sio wakati wa kuishi kwa woga, bali unapaswa kuwa na hofu na Mungu, weka tumaini kwake, tambua kabisa ninaishi kwa neno lake. Neno lolote ambalo Mungu analituma kwako ili ulipitie unapaswa kupia, tambua kabisa anayeshuka huwa anapanda. Katika kifungu hicho Mungu anataka tuyaelewe mazingira ili baadae tuje kuishi kwa furaha.

Unapokuwa umejiingiza katika maisha ya kulaumu kila wakati tambua kwamba umejiingiz katika maisha ya woga, na woga ukikutawala umekufa, kumbuka wana Waisraeli walipokuwa wanamnung'unikia Musa kule jangwani, walishia kufa tu, Mungu aliwatuma nyoka wenye sumu, wakawagonga wakafa. Kwahiyo weka tumaini lako kwa Mungu na hutapungukiwa na lolote wala mguu, wala mavazi yako hayatachaka. Kila wakati huwa unapita, Mungu amekuandalia yaliyo mema.

Ishi kwa upendo katika wakati huu mgumu na upendo ndio huleta amani na furaha, upendo hauhesabu muda, upendo huvumilia yote,upendo hutoka kwa Mungu maana kwake ndimo yanayotoka ya upendo yaliyo mazuri bali ubinafsi huleta hofu na hofu inakupeleka kwenye woga na woga ni nguvu ya shetani sasa.

Furaha mwanzo wake upendo ni kuwafikiria wengine na kuwatendea kwa kuzingatia kiasi, na kiasi huleta amani na amani huleta furaha na furaha ni nguvu yenye mwelekeo chanya kwa wahusika.

Woga mwanzo wake ubinafsi, ubinafsi usio na kiasi na ubinafsi usio na kiasi huleta hofu isiyo na tumaini na hofu isiyo na tumaini kwa Mungu itakutupa kwenye woga na woga ni gereza la shetani la mateso.

Mpendwa mosomaji, rafiki yangu, Ndugu katika Bwana Mungu, maisha ambayo hayana shukrani ni maisha ambayo ni ya kizungumkuti ni maisha ya kupelekwa huku na huko, maisha ambayo hayazingatii kiasi  yanakosa uwepo. Mtumaini Mungu wakati wote na uishi katika nguvu zake.

Leo ni ninazawadi ya vitabu viwili kwako, kitabu ambacho nimekiandika mimi mwenyewe cha UKRISTO NA MAISHA na kitabu kilichoandikwa na JOYCE MEYER cha NISAIDIE NAOGOPA.  Hakikisha unajipatia vitabu hivi ambavyo vitakusaidia kulingana utayari wako wa kutaka kujua  Mungu anataka nini katika maisha yetu. Kwenye kitabu changu nimeeleza kwa undani juu ya Injili ya Maji na Roho ambayo ndiyo ufunguo katika Ufalme wa Mungu na kitabu cha nisaidie naogopa, mwandishi ameeleza namna ya kukabiliana na hofu, emeleza kwa undani zaidi. Hakikisha unajipatia vitabu hivi bure kabisa, nitumie ujumbe kwa namba 0687000768 au sadikila65@gmail.com. Nitumie ujumbe nami nikutumie kitabu.

Asante kwa kusoma makala hii, Mungu akubariki, mimi ni zawadi yako na wewe ni zawadi yangu mimi, Mungu amenizawadia wewe.
asante.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.

Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.
 



  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg
Email ThisBlogThis!Share to XShare to Facebook
Newer Post Older Post Home

0 comments:

Post a Comment

Search This Blog

Translate

Total Pageviews

About Me

Sadick Kilasi
View my complete profile

Followers

Kurasa

  • Nyumbani
  • Saidia Huduma Hii Kuwafikia Wengi Zaidi.

Search This Blog

Blog Archive

  • ►  2020 (5)
    • ►  January (5)
  • ►  2019 (46)
    • ►  December (4)
    • ►  October (1)
    • ►  July (8)
    • ►  June (1)
    • ►  May (2)
    • ►  March (14)
    • ►  February (11)
    • ►  January (5)
  • ▼  2018 (275)
    • ►  December (17)
    • ►  November (25)
    • ►  October (29)
    • ►  September (43)
    • ▼  August (7)
      • Nguvu Mbili Ambazo Hutawala Katika Ulimwengu Huu.
      • Kama Unayo Leo.
      • Katika Shamba La Mabomu
      • Namkumbuka Babu Yangu Babu Yangu Ni Shujaa Wangu.
      • Alipambania Tumaini Lake Na Ndoto Yake Ikawa Kweli.
      • Ona Wema Kwenye Kila Jambo.
      • Je Unataka Kuwa Bingwa Wa Kuwasamehe Watu?
    • ►  July (12)
    • ►  June (17)
    • ►  May (19)
    • ►  April (31)
    • ►  March (33)
    • ►  February (25)
    • ►  January (17)
  • ►  2017 (58)
    • ►  December (16)
    • ►  November (22)
    • ►  October (2)
    • ►  September (11)
    • ►  August (4)
    • ►  July (3)
Sadick Kilasi. Powered by Blogger.

Jisajili kwa kujiunga nasi hapa

Posts
Atom
Posts
Comments
Atom
Comments
Maisha yenye maana ni yale maisha ambayo mhusika atambua nini kusudi lake la kuwepo hapa duniani. Hapandipo muhusika anapo kaa katika nafasi yake na kuwasha nuru katika sehemu aliopo kutokana uhusika wake. Jiunge na mtandao huu kupata maarifa zaidi na kwa ushirikiano mwingine kwa ujumla.

Kurasa

  • Nyumbani
  • TAFAKARI ROHO
  • Saidia Huduma Hii Kuwafikia Wengi Zaidi.

JIUNGE NASI SASA KWA KUJAZA FOMU HAPO CHINI


ANZA KUFURAHIA MAISHA NDANI YA YESU, MPOKEE ROHO MTAKATIFU KWA INJILI YA MAJI NA DAMU 0687000768

Zilizosomwa sana

  • Chukua hizi hapa nukuu za Malcolm x mtu ambaye anawavutia wengi sana.
    Ni siku nyingine tena ambayo ni mpya kabisa, karibu tena katika blogu hii ya JIKO LA USHAURI ambapo mimi mpendwa wako nimekuwa naingia jikon...
  • Ubatizo Wa Maji Mengi Na Ubatizo Wa Maji Machache, Upi Ni Sahihi?
    Ubatizo wa Maji Mengi Na Maji Machache. Kumekuwa na migongano kwa muda mrefu sana juu ya ubatizo, kati ya ubatizo wa maji mengi na ule uba...
  • Falsafa Za Maisha, Yaani Neno La Maarifa.
    Falsafa Za Maisha, Yaani Neno La Maarifa. Habari mpendwa? Natumai wewe unayesoma hapa umzima.   Karibu tena katika Falsafa Za Maisha. Ku...

Blog Archive

  • July 2017 (3)
  • August 2017 (4)
  • September 2017 (11)
  • October 2017 (2)
  • November 2017 (22)
  • December 2017 (16)
  • January 2018 (17)
  • February 2018 (25)
  • March 2018 (33)
  • April 2018 (31)
  • May 2018 (19)
  • June 2018 (17)
  • July 2018 (12)
  • August 2018 (7)
  • September 2018 (43)
  • October 2018 (29)
  • November 2018 (25)
  • December 2018 (17)
  • January 2019 (5)
  • February 2019 (11)
  • March 2019 (14)
  • May 2019 (2)
  • June 2019 (1)
  • July 2019 (8)
  • October 2019 (1)
  • December 2019 (4)
  • January 2020 (5)

JIKO LA USHAURI

Itambue Injili Ya Maji Na Roho. Ushiriki Ufalme wa Mungu, pata kitabu cha bure. Wasiliana nasi kwa sadikila65@gmail.com.

Tags

  • BIASHARA
  • HEKIMA ZA WAZEE
  • KUFURAHIA MAISHA
  • KUPATA BLOGU
  • MAHUSIANO
  • MAWASILIANO
  • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI
  • NJOZI
  • PATA BLOGU
  • SAIDIA HUDUMA HII
  • TAFAKARI NENO YA SIKU
  • TAFAKARI YA ROHO
  • UJASIRIAMALI
  • USHAURI
  • USWAZI TRICK

Kurasa

Labels

  • HEKIMA ZA WAZEE (24)
  • KUFURAHIA MAISHA (76)
  • KUPATA BLOGU (2)
  • MAHUSIANO (81)
  • MAWASILIANO (1)
  • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI (8)
  • NJOZI (94)
  • PATA BLOGU (3)
  • TAFAKARI YA ROHO (57)
  • UJASIRIAMALI (31)
  • USHAURI (78)
  • USWAZI TRICK (9)

Loading...

Fomu ya Anwani

Name

Email *

Message *

  • Napenda kusoma Biblia

About Me

Sadick Kilasi
View my complete profile
INJILI YA MAJI NA DAMU.

Search This Blog

Chapisho Lililoangaziwa

Alipambania Tumaini Lake Na Ndoto Yake Ikawa Kweli.

Kila mtu katika maisha ana tumaini lake. Msingi mkuu wa maisha ni tumaini. Nguvu kubwa ya maisha ni imani na mapito makuu ya maisha ni u...

Posts
Atom
Posts
Comments
Atom
Comments
INJILI YA KWELI NI INJILI YA MAJI NA ROHO. (MAJI, DAMU NA ROHO).
HII NDIYO KWELI YENYEWE.
YOHANA 19:34-35.

Copyright © JIKO LA USHAURI | Powered by Blogger
Design by Hardeep Asrani | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com | Distributed By Gooyaabi Templates