JIKO LA USHAURI

Itambue Injili Ya Maji Na Roho. Ushiriki Ufalme wa Mungu, pata kitabu cha bure. Wasiliana nasi kwa sadikila65@gmail.com.

  • NYUMBANI
  • KUFURAHIA MAISHA
    • ushauri
    • KUHUSU SISI
    • MAISHA NDANI YA YESU
  • MAWASILIANO
    • NAMBA YA SIMU
      • Sub 0687000768
      • Sub Child Category 2
      • facebook
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • NJOZI
  • SAIDIA HUDUMA HII
    • Childcare
    • Doctors
  • NYUMBANI
  • KUFURAHIA MAISHA
    • Stock
  • TAFAKARI YA ROHO
    • HEKIMA ZA WAZEE
    • Games
    • AFYA
      • Office
  • MAHUSIANO
    • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI
      • Sub Child Category 1
      • Sub Child Category 2
      • Sub Child Category 3
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • USHAURI
  • TAFAKARI NENO YA SIKU
    • Childcare
    • Doctors
  • PATA BLOGU

Tuesday, August 14, 2018

Katika Shamba La Mabomu

 Sadick Kilasi     August 14, 2018     PATA BLOGU, TAFAKARI YA ROHO     No comments   



Fikiri kana kwamba upo kwenye shamba la mabomu na unahitaji kutoka katika hatari hiyo ya mauti.

Ni ukweli usiopingika, tumaini la maisha yako litakuwa na thamani kubwa sana kwa sababu  kiwango cha uhakika wa maisha yako kitakuwa ni mdogo sana. Chochote ambacho ni adimu kupatikana huwa kikuwaga na thamani kubwa sana.

Kwa wakati kama huu wa kwenye shamba la mabomu, imani kwa Mungu itakuwa ni kubwa sana. Wakati kama huu wengi huwa tunamtegemea Mungu kwa kiasi kikubwa na huwezi kujitegemea mwenyewe. Maombi yatakuwa ni ya imani na kweli na hapa ndipo mtu anaweza kukuta anamwabudu Mungu katika roho na kweli kwa sababu ya mazingira ambayo yupo kwa wakati huo. Hivi ndivyo binadamu tulivyo hukumbuka wakati tunahisi na kuona kwa macho yetu kwamba huu ni wakati wa hatari.

Lakini pia katika mazingira hayo maamuzi ambayo mtu atakua anachukua ni maamuzi yenye tahadhari ili kulinda kile ambacho yeye anaona ni kidogo ambacho amebaki nacho.

Katika shamba la mabomu, upo katikati, ukijiona unajiona wewe tu na mabomu na unahitaji kujinasua kutoka hapo, hapo ndipo mambo hayo matatu hufanywa kwa ufasaha na uzingativu mkubwa sana.

Mpendwa msomaji, inawezekana huwa unafanya hivi ukiwa na shida, vizuri maana unapaswa kweli kumtegemea Mungu  katika hali kama hii lakini nikuambie kitu hivyo si sawa, kumtemea Mungu wakati wa shida pekee hivyo si sawa. Huwezi kumtegemea Mungu kwa matukio.

Katika maisha tunapaswa kumtegemea Mungu wakati wote, usimwabudu Mungu kwa mambo ya nje ya mwili yenye mipaka ni lazima tumwabudu Mungu katika roho.

Kama tunamwabudu Mungu katika matendo ya kusubiri mipaka, yaani mpaka jambo fulani litokee basi tutakuwa wanafiki kwani kama mtu huyu yupo katika shamba la mabomu, anachothamini pale ni Mungu ama uhai wake? Si Mungu ni bora kuliko uhai wake? Maana yeye ndiye mwenye uhai wake, anaweza kuamua kuchukua wakati wote, wakati ambao upo katika shamba la mabomu au la, upo katika hali nzuri kabisa. Yesu alisema, atakaye kuokoa uhai wake naye ataupoteza na atakayepoteza uhai wake kwaajili yangu naye yatakuwa na uhai, je maneno haya si kweli?

Unajua mara nyingi sisi hatuoni kabisa na ndiomaana tumekosa shukrani na hata kama tukitoa shukrani ni ya kinafiki kwa sababu, Mungu katupigania uhai wetu kabla hatujafika kwenye shamba la mabomu, hatujashukuru, lakini mpaka pale ambapo tutashuhudia kwa macho yetu wenyewe.

Tunasahau kwamba jambo ambalo mwanadamu huthamini ni uchomvu mtupu kwani jambo lolote ambalo ni dhaifu ndilo lenye nguvu na lenye nguvu ndilo dhaifu. Na tukubaliane hapa, je! Sehemu za siri si ndizo sehemu za aibu? Je! si ndizo sehemu ambazo tunazipa thamani kubwa? Nakuuliza swali sasa, je! kitu kichovu unaweza kulipia gharama kubwa?

Mpendwa msomaji, huu ndio wakati wa kubadilika, tumwabudu Mungu katika roho na kweli, Neno linasema kesheni msilale maana kwenu hakuna giza na kulala tena. Kabisa linapaswa kubadilika sasa, ondoa mipaka kwa Mungu, Mungu ni mkamirifu. Tena linasema jifungeni dirii ya haki viunoni mwenu.

Katika maamuzi sasa, maamuzi unayofanya siku zote yawe ni upendo tu, hakikisha kila jambo unalichunguza, je! linakujenga wewe binafsi? Je! Haliwaumizi watu wengine? Wakati unafanya maamuzi juu ya watu wengine jipime mwenyewe, vipi kama ingekuwa ndo mimi hapo, ukiisha pata jibu basi ndivyo unavopaswa kumfanyia mwingine.

Mpendwa msomaji, tunaishi ndani ya wakati, tupo ndani ya shamba la mabomu wakati wote ila hatuoni tu, kwahiyo hakikisha kanuni unazotumia ukiwa ndani ya shamba la mabomu unatumia wakati wote, sio mpaka uipime hatari kwa macho yako harafu uanze kufanya maamuzi mazuri, hapana, Kila wakati ni sahihi kufanya jambo sahihi.

Hakikisha imani kwa Mungu ni wakati wote, maombi yawe mengi na rahisi. Sasa simaanishi yale maombi ya udini yale, maombi yako yawe kama mtu anayekimbia mbio ndefu yaani wakati wote, ukiwa pekee yako unaomba kwa sauti kidogo, ukiona kuna watu maombi yako ni ya ndani yaani ili mradi wakati wote uwe unashugulika, neno la Mungu lidumu daima, shukrani itawale katika maisha yako. Usiwe mtu wa kulalamika sana. Fanya kwa ubora zaidi, kwa kadili ya mazingira yako.

Asante sana, Mungu akuongoze katika hatua za maisha yako.

Kitabu cha MAISHA NA UKRISTO ni kwaajili yako, kitabu hiki ni bure kabisa. Hakikisha tunawasiliana ili nikutimie kitabu hiki. Kitabu ambacho nimeandika zaidi juu ya kushiriki utukufu wa Mungu na funguo za ufalme wa Mungu. Jipatie kitabu hiki.
 Juu ya kitabu hiki, watu wengi vitu vya bure huwa hawathamini kama nilivoeleza hapo juu, chochote ambacho kinapatikana bure huwa kinashushwa thamani lakini nataka nikwambie rafiki yangu, nimeandika kitabu hiki na kukitoa bure nikiwa ninamaana kwamba kila mmoja ambaye atakutana na ujumbe huu apate kitabu haijarishi yupo katika mazingira gani? Wengine wana pesa wengine hawana lakini katika maisha wote ni sawa na wote tunahitaji uponyaji na kufurahia maisha. Ni vema kufanya maamuzi yaliyo sahihi ukitambua kwamba wakati wote upo katika shamba la mabomu. Lengo ni kila mmoja apate kwahiyo kama ni pesa unatoa kwa kadili ya shukrani yako, yoyote ile sawa. Kila mtu anapaswa kushiriki utukufu wa Mungu.

Wewe ni zawadi yangu, hakikisha unajipatia kitabu hiki. Nitumie ujumbe whatsap au kwenye email ili nikutumie kitabu.

Sadick Kilasi wa jikolaushauri.blogspot.com.


Mawasiliano ni 0687000768 au sadikila65@gmail.com.





  • Share This:  
  •  Facebook
  •  Twitter
  •  Google+
  •  Stumble
  •  Digg
Email ThisBlogThis!Share to XShare to Facebook
Newer Post Older Post Home

0 comments:

Post a Comment

Search This Blog

Translate

Total Pageviews

About Me

Sadick Kilasi
View my complete profile

Followers

Kurasa

  • Nyumbani
  • Saidia Huduma Hii Kuwafikia Wengi Zaidi.

Search This Blog

Blog Archive

  • ►  2020 (5)
    • ►  January (5)
  • ►  2019 (46)
    • ►  December (4)
    • ►  October (1)
    • ►  July (8)
    • ►  June (1)
    • ►  May (2)
    • ►  March (14)
    • ►  February (11)
    • ►  January (5)
  • ▼  2018 (275)
    • ►  December (17)
    • ►  November (25)
    • ►  October (29)
    • ►  September (43)
    • ▼  August (7)
      • Nguvu Mbili Ambazo Hutawala Katika Ulimwengu Huu.
      • Kama Unayo Leo.
      • Katika Shamba La Mabomu
      • Namkumbuka Babu Yangu Babu Yangu Ni Shujaa Wangu.
      • Alipambania Tumaini Lake Na Ndoto Yake Ikawa Kweli.
      • Ona Wema Kwenye Kila Jambo.
      • Je Unataka Kuwa Bingwa Wa Kuwasamehe Watu?
    • ►  July (12)
    • ►  June (17)
    • ►  May (19)
    • ►  April (31)
    • ►  March (33)
    • ►  February (25)
    • ►  January (17)
  • ►  2017 (58)
    • ►  December (16)
    • ►  November (22)
    • ►  October (2)
    • ►  September (11)
    • ►  August (4)
    • ►  July (3)
Sadick Kilasi. Powered by Blogger.

Jisajili kwa kujiunga nasi hapa

Posts
Atom
Posts
Comments
Atom
Comments
Maisha yenye maana ni yale maisha ambayo mhusika atambua nini kusudi lake la kuwepo hapa duniani. Hapandipo muhusika anapo kaa katika nafasi yake na kuwasha nuru katika sehemu aliopo kutokana uhusika wake. Jiunge na mtandao huu kupata maarifa zaidi na kwa ushirikiano mwingine kwa ujumla.

Kurasa

  • Nyumbani
  • TAFAKARI ROHO
  • Saidia Huduma Hii Kuwafikia Wengi Zaidi.

JIUNGE NASI SASA KWA KUJAZA FOMU HAPO CHINI


ANZA KUFURAHIA MAISHA NDANI YA YESU, MPOKEE ROHO MTAKATIFU KWA INJILI YA MAJI NA DAMU 0687000768

Zilizosomwa sana

  • Chukua hizi hapa nukuu za Malcolm x mtu ambaye anawavutia wengi sana.
    Ni siku nyingine tena ambayo ni mpya kabisa, karibu tena katika blogu hii ya JIKO LA USHAURI ambapo mimi mpendwa wako nimekuwa naingia jikon...
  • Ubatizo Wa Maji Mengi Na Ubatizo Wa Maji Machache, Upi Ni Sahihi?
    Ubatizo wa Maji Mengi Na Maji Machache. Kumekuwa na migongano kwa muda mrefu sana juu ya ubatizo, kati ya ubatizo wa maji mengi na ule uba...
  • Falsafa Za Maisha, Yaani Neno La Maarifa.
    Falsafa Za Maisha, Yaani Neno La Maarifa. Habari mpendwa? Natumai wewe unayesoma hapa umzima.   Karibu tena katika Falsafa Za Maisha. Ku...

Blog Archive

  • July 2017 (3)
  • August 2017 (4)
  • September 2017 (11)
  • October 2017 (2)
  • November 2017 (22)
  • December 2017 (16)
  • January 2018 (17)
  • February 2018 (25)
  • March 2018 (33)
  • April 2018 (31)
  • May 2018 (19)
  • June 2018 (17)
  • July 2018 (12)
  • August 2018 (7)
  • September 2018 (43)
  • October 2018 (29)
  • November 2018 (25)
  • December 2018 (17)
  • January 2019 (5)
  • February 2019 (11)
  • March 2019 (14)
  • May 2019 (2)
  • June 2019 (1)
  • July 2019 (8)
  • October 2019 (1)
  • December 2019 (4)
  • January 2020 (5)

JIKO LA USHAURI

Itambue Injili Ya Maji Na Roho. Ushiriki Ufalme wa Mungu, pata kitabu cha bure. Wasiliana nasi kwa sadikila65@gmail.com.

Tags

  • BIASHARA
  • HEKIMA ZA WAZEE
  • KUFURAHIA MAISHA
  • KUPATA BLOGU
  • MAHUSIANO
  • MAWASILIANO
  • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI
  • NJOZI
  • PATA BLOGU
  • SAIDIA HUDUMA HII
  • TAFAKARI NENO YA SIKU
  • TAFAKARI YA ROHO
  • UJASIRIAMALI
  • USHAURI
  • USWAZI TRICK

Kurasa

Labels

  • HEKIMA ZA WAZEE (24)
  • KUFURAHIA MAISHA (76)
  • KUPATA BLOGU (2)
  • MAHUSIANO (81)
  • MAWASILIANO (1)
  • NENO KUTOKA KWA SADICK KILASI (8)
  • NJOZI (94)
  • PATA BLOGU (3)
  • TAFAKARI YA ROHO (57)
  • UJASIRIAMALI (31)
  • USHAURI (78)
  • USWAZI TRICK (9)

Loading...

Fomu ya Anwani

Name

Email *

Message *

  • Napenda kusoma Biblia

About Me

Sadick Kilasi
View my complete profile
INJILI YA MAJI NA DAMU.

Search This Blog

Chapisho Lililoangaziwa

Alipambania Tumaini Lake Na Ndoto Yake Ikawa Kweli.

Kila mtu katika maisha ana tumaini lake. Msingi mkuu wa maisha ni tumaini. Nguvu kubwa ya maisha ni imani na mapito makuu ya maisha ni u...

Posts
Atom
Posts
Comments
Atom
Comments
INJILI YA KWELI NI INJILI YA MAJI NA ROHO. (MAJI, DAMU NA ROHO).
HII NDIYO KWELI YENYEWE.
YOHANA 19:34-35.

Copyright © JIKO LA USHAURI | Powered by Blogger
Design by Hardeep Asrani | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com | Distributed By Gooyaabi Templates